Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Kwanini Utumishi wanatumia muda mrefu kuita watu kazini?

Daaaaah hakuna kipindii niliumia Sana kama kuona status NOT SELECTED FOR ORAL INTERVIEW wakatii nimetumia pesaa karibiaa lakii mbilii kusafiri na kukaa Dodoma,nimesomaa kwa zaidii ya miezii miwilii,it was so painful for me, Namuomba Mungu anisaidiee siku moja nilambe asali nisahau Yale maumivu
Ni suala la muda tu, utalamba asali na ushuhuda wako utawatia sana nguvu wengine!
 
Mbona nasikia huko kwenye Mashirika ya Umoja wa Mataifa (UNA) watu wanakula sana maisha mkuu.
Inategemea alikuwa akifanya kazi wapi...!!

Sisi wengine bado tupo tupo huku mashirikani taking some green pasture na bado mambo yananyoka kwa kiwango chake.

Binafsi niliwaza kuja kuwa mtumishi wa GoT at my 40 when everything is OK 😋 and that's what I always think of.
 
Jamani Mwifwa Twinawe na wengine na naomba kuuliza swali mwajiri anapokuambia urudi nyumbani baada ya kureport kazini alafu mwezi na wiki vinakatika bila kuitwa hii inakuwa na tafsiri gani?
Je kabla ya kuondoka ulijaza form ya taarifa zako pamoja na akaunti yako? Kama ulijaza wala usiwe na wasi wasi utakula mishahara ukiwa nyumbasni kama wakichelewa kukuita!
 
Watu hadi wanaonekana kukata tamaa kabisa humu
Ni muhimu sana kutokukata tamaa!! Kukata tamaa hakujawahi kumsaidia mtu yeyote!! Si vizuri kufanya kitu ambacho hakijawahi kumsaidia mtu yeyote!! Pitia shuhuda za watu humu waliovumilia kwa muda mrefu lakini hatimaye wakalamba asali!! Hii itakutia sana nguvu! Kumbuka pia kuwa Mungu ni mwaminifu, na ndiye mtoa riziki kwa watu wote, ni suala la muda tu!!
 
Hakuna stress mbaya utumishi kama kusubiri placement ya ajira..

Nani ameshawahi kupitia hii hali wakuu ?

Ndugu yangu pole, nakuelewa unachopitia.

Lakini umeshawahi kumuwaza na mtu aliyesoma kitu ambacho ajira zake kutoka ni ndoto!? Yani yeye hata tukio lakuona Serikali imetangaza nafasi ya alichosomea ni sherehe, anaweza kukaa mpaka miaka miwili haijawahi kutokea nafasi ikatangazwa na endapo akipishana nayo, itambidi asubiri sana.
 
Mungu ni mwema, wadau na mm leo nimelamba asali namshukuru sana mungu, nawashukuru wana uzi huu kwa faraja zenu kipindi nasubilia placement wadau msikate tamaa wakati wa mungu ndio wakati sahihi, lakn pia naamini yajayo yanafurahisha kwa upande wenu.
Hongera sana mkuu. Mungu azidi kukusimamia ktk majumu yako mapya.
 
Mungu ni mwema, wadau na mm leo nimelamba asali namshukuru sana mungu, nawashukuru wana uzi huu kwa faraja zenu kipindi nasubilia placement wadau msikate tamaa wakati wa mungu ndio wakati sahihi, lakn pia naamini yajayo yanafurahisha kwa upande wenu.
Mwamba rinyungu,hongera sanaaa aseee
 
Ndugu zangu katika mapambano na kujitafuta, mkipata mchongo msisahau kuaga😊💪, msiondoke kimya kimya maana jumbe zenu za mafanikio ni hamasa kubwa kwa ambao bado wanapambana

huu uzi pendwa umetufariji kwa kipindi kirefu katika hizi harakati zetu za kujitafuta, shuhuda yako ni muhimu sana kuwapa moyo wale ambao pengine kwa namna moja au nyingine wamekata tamaa,

pia sote tusisite kupita humu mara kwa mara hata baada ya kutoboa, kuna ufafanuzi au hata maswali mengi ambayo unaweza kujibia au kusaidia kuwapa ufahamu wengine ambao pengine kwa yale uliyoyapitia tayari una majibu nayo

Nikupe Moyo ambaye bado unapambana kuingia kwenye ajira, na wewe ambae umeshaingia tayari ila unapambana kuzoea mazingira ya kazi mpya, na wewe ambae unasikilizia majibu ya usaili uliofanya, bila kusahau na wewe ambae ndio kwanza unaelekea kwenye usaili na hujui itakuwaje huko mbeleni, na kwa yoyote aliyopo kwenye hatua yoyote ile ya kutafuta ajira,

amini kwa imani yako kuwa wakati wa Mungu ndio wakati sahihi, mtumainie Mungu nae atakupigania, siku moja utapata kile unachotafuta, na utakapofanikiwa usisahau kumrudishia shukrani kwa yale aliyokufanyia. Amen

Cc Mwifwa makofia360 lerman3x
Mkuu mie namshukuru Mungu nimepass aptitude test,na nimeitwa oral bot,nimeomba likizo ya wiki 1 job,saiv Niko chimbo najiandaa na oral,dua zenu muhimu🙏🙏🙏
 
Back
Top Bottom