Kwanini UWT ni taasisi ya CCM? Kwanini isiitwe Umoja wa Wanawake wa CCM (UWCCM) halafu UWT ikawa umoja wa wanawake wote Tanzania?

Kwanini UWT ni taasisi ya CCM? Kwanini isiitwe Umoja wa Wanawake wa CCM (UWCCM) halafu UWT ikawa umoja wa wanawake wote Tanzania?

fazili

JF-Expert Member
Joined
Jun 10, 2011
Posts
16,427
Reaction score
22,418
Inashangaza kuona kwamba UWT ni taasisi ya CCM. Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) unapaswa kuwa umoja wa wanawake wote Tanzania bila kujali itikadi ya vyama. Wanawake wa CCM waanzishe umoja wao kama ilivyo BAWACHA kwa CHADEMA, n.k.

CCM kiache kupora taasisi na mali nyingine za umma na kuzifanya kuwa mali au taasisi za chama. Kuna viwanja vya mpira kama CCM Kirumba, majengo kadhaa ya umma, n.k. vimefanywa kuwa mali za CCM! Huu ni uporaji wa mali za umma kwa faida ya vyama vya siasa.

Umoja wa Wazazi na Umoja wa Vijana Tanzania pia hazipaswi kuwa taasisi za CCM.
 
Inashangaza kuona kwamba UWT ni taasisi ya CCM. Umoja wa Wanawake Tanzania (UWT) unapaswa kuwa umoja wa wanawake wote Tanzania bila kujali itikadi ya vyama. Wanawake wa CCM waanzishe umoja wao kama ilivyo BAWACHA kwa CHADEMA, n.k.

CCM kiache kupora taasisi na mali nyingine za umma na kuzifanya kuwa mali au taasisi za chama. Kuna viwanja vya mpira kama CCM Kirumba, majengo kadhaa ya umma, n.k. vimefanywa kuwa mali za CCM! Huu ni uporaji wa mali za umma kwa faida ya vyama vya siasa.
Wazo zuri, isomeke hivi kwa sasa UWCCMT
Umoja wa wanawake wa ccm Tanzania
 
Kama mpaka JWTZ nayo inajiona ni taasisi ya CCM, itakuwa hiyo UWT? Bila machafuko au serikali kupinduliwa athari za mfumo wa chama kimoja zitaendelea kuwepo, na kibaya zaidi hali hiyo inazidi kushamiri sasa. Sasa hivi sio mahakama au bunge zilizojiwekea mbali na ccm kama chama.
 
Umoja wa Wanawake Tanzania, Umoja wa Wazazi Tanzania, Umoja wa Vijana zote za CCM lakini zinabeba sura ya kitaifa. Tafsiri yake ni kwamba bado ina mizizi migumu sana ndani ya nchi
 
Back
Top Bottom