Kwanini vibopa wengi wanapenda logistic business?

Hapo kuna watu wana fleet mpka 500+
 
Hivi ni Kwanini vibopa wengi wanapenda logistic business? Ina faida sana ama ni biashara ndani ya biashara.
Uki master Logistic unakuwa na infinite potential, unafikiri kwanini mtu kama MO ama Bakhresa akitoa bidhaa inahit hapo hapo? Wana Logistic nchi nzima kitu kikiwa produced hapo hapo kinasambaa.
 

Umewasahau Dianarose, Lema wa kibaha
 
Sina tafiti na matokeo sahihi lakini siku hizi ni janja janja tu shule nayo inasaidia kama ukijitoa.....wasomi huwa sio risk taker.
Wasomi sio risk taker hapo umesema kweli.... kuna msimu wa mbaazi wakati wa magufuli zilikosa soko kabisa ilifikia hatua hata bosi wa kununua shiling mia mbili alikosekana mbaazi zikawa zimejaa tu na serikali ikawajibu wakulima kuwa mbaazi ni mboga wale tu,sasa kuna mzee mmoja hapa mtwara anaitwa chinganalile alijilipua akanunua tani 70 kwa bei ya shiling 200 na watu walimlaumu sana na yeye wala hakujali akazitia dawa akaziweka ghalani huwezi amini alikuja kuuza kwa wahindi baada ya miezi 4 kwa bei ya 750 na kila mtu akawa anajishika kichwa...hawa ndio risk taker
 
Uki master Logistic unakuwa na infinite potential, unafikiri kwanini mtu kama MO ama Bakhresa akitoa bidhaa inahit hapo hapo? Wana Logistic nchi nzima kitu kikiwa produced hapo hapo kinasambaa.
jamaa wako njema sana nahisi pia kuwa na makampuni yao ya logistic inawapunguzia costs za kusafirisha bidhaa zao
 
shida wasomi wakitaka kufanya jambo huwa wanafanya analysis nyingi sana ambazo mwisho wa siku huwa wanaishia kukata tamaa
 
shida wasomi wakitaka kufanya jambo huwa wanafanya analysis nyingi sana ambazo mwisho wa siku huwa wanaishia kukata tamaa
Angalia hata wasomi uchwara waliopo humu ndani utasikia mtu anakuambia biashara ya duka la mahitaji ya nyumbani ni ngumu mno mara utajuaje faida mara faida yenyewe mia ....wanasahau kuwa siri ya kufanikiwa ni moja tu kuwa bahiri(kufanya mambo muhimu tu) ila sasa ukija mtaani watu kibao wanatoboa kwa biashara hizo
 
Mainline carriers ltd na ma Beiben yao wametisha sana.
 
Wasomi ni chenga sana ndio maana wanazidiwa kete nyingi....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…