Kwanini vijana wa Diamond hawapati dili za matangazo?

Kwanini vijana wa Diamond hawapati dili za matangazo?

Ila jamaa anakunja adi sio poa..

Dili ndogo ndogo km ile ya tomato ilikuwa n ya kumpa ata raymond sio kufanya yeye kila ktu..

Huyu jamaa ni mbinafsi sana. Ni suala la muda tu

Sent using Jamii Forums mobile app
Mondi naye ni binadamu...hawezikuwa perfect kila siku kila binadamu anajiangalia yeye kwanza ata ungekuwa wewe ila kwa mahali alipowatoa kina lavalava hadi apa walipo wana ya kumshukuru mengi sana kuliko kuwaza viela vya matangazo ambayo mengi yao yana unyonyaji ndani yake
 
Yani binadamu bana... kweli hawezi ridhishwa hata kidogo. Hao kina Vanny na wenzake leo mnaongea kuwa wananyonywa na Diamond, hapo kabla hata kuwajua mlikuwa mnawajua? Hizo show wanazofanya wanafanya bure au wanapewaga milioni moja moja? Na mkataba walioingia hawakuwa wanaona yaliyomo ama?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mimi ninachowahurumia kama huyo Rayvanny kila kitu siyo chake.

Kuanzia Jina: Rayvanny, YouTube Channels, iTunes, Deezer, Tidal Accounts, Nyimbo zote na Audio alizo rekodi akiwa na WCB mpaka mashabiki ni Mali Ya Wasafi.

Siku wakimtimua ( Maana yule nguvu ya kutoka sidhani kama anayo ) anaenda kuanza upya kama KIFARANGA YATIMA.

Na Hii ni kwa wasanii wote wa WCB kama Mbosso na Lava Lava
Wakati wanasign hawakuyaona uyasemayo?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mbana anapotoa hela nyingi kulipia video za Rayvanny, Mboso na Lavalava au alipotumia nguvu nyingi kuwapa promo wasanii wake ikiwemo na yeye kujinyima kutoa ngoma zake ili ngoma za wasanii wake ziende mbona ukumwita mbinafsi?
Kama unawasaidia afu UNAWANYONYA umewasaidiaaa au UMEJISAIDIA...pale wanatengeneza MASIKINI WENYE MAJINA MAKUBWA.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu kuhusu mama ake rayvan kuna mtu aliniambia yule mama ni mtu dini sana, yani wale walokole wa itikadi kali.
Sasa Imani yake ni kwamba hela za rayvan ni za freemason, mama hataki msaada wowote toka kwa mwanae..
Jamaa msimuone vile ana stress nyingi sana, kaz yake haina baraka za mama ake.

Niliposikia hapa habar za kuuza mboga za mafungu, nikaunganisha na ile habari nikaona kuna ukweli fulani.

Japo inawezekana pia jamaa yupo majalala..

Sent using Jamii Forums mobile app
Sanaa ya bongo hailipi ki hivyo na ubaya ni kuwa wasanii hawataki kulikubali hilo wanaishi maisha ya kuigiza. Nilipata kuona nyumbani kwao Lizer, bado maisha ni ya duni bado. Unaweza kuona kuwa hawapati kipato bora na hata hicho kidogo wanachokipata hawakifanyi kizalishe.
 
Nilipaona kwao ray kwakweli panatia huruma halafu anasema mama yake karidhika kuuza mbogamboga eti hataki biashara nyingine yaani madogo wanatumikishwa wakija kufa ukifika makwao ndio unajua walikua wanaishi kwa kuigiza maisha miaka yote


Sent from my iPhone using JamiiForums
Mziki unalipa bwana!!!... ukiangalia maisha halisi ya vijana wa WCB unaweza kulia sana!!!...kilichopo kwenye mitandao na wao wenyewe ni tofauti kubwa
 
binafsi maisha ya rayvanny siyajui ila nilipata kushuhudia mjengo wa mboso uliopo pale Mbweni beach, uko vizuri sana ukijumlisha na kale kagali kake (toyota harrier). iko wazi kuna wasanii wakongwe amewapita maisha
 
Back
Top Bottom