Extrovert
JF-Expert Member
- Feb 29, 2016
- 70,785
- 186,690
Mkuu guiness baridi haitodhuruUnakunywa bia 🍺 au soda? Nipe namba ya lipa👏👏👏👏
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mkuu guiness baridi haitodhuruUnakunywa bia 🍺 au soda? Nipe namba ya lipa👏👏👏👏
Mkuu umenena vyema sana. Hata Hashimu Rungwe aliona mbali sama kuweka hili katika ilani yakekwa wale waliowahi kuishi America. ulitakiwa unapojumuisha watu weusi ujumuishe na African Americans. wale jamaa wapo ambao mzungu hata akiwa genius hatii mguu, kina Obama, Kina Condoresa Rise, na wengine wengi, isipokuwa ni wale tu wanaotoka familia yanye kipato, na wengi wao utakuta ni mchanganyiko wa mzungu na mweusi. nimesoma na African Americans, wapo vizuri sana kichwani kwa wale wanaoenda shule na wapambanaji balaa.
kwa utafiti ambao tayari ulishafanywa, ili mtu awe na uwezo wa akili kiwango cha juu pamoja ambavyo pia vinaendana na ustaarabu, ipo determined na aina ya maisha aliyokulia tangu akiwa tumboni mwa mama yake.
kwa kifupi, aina ya vyakula tunavyokula ndivyo vinavyodetermine development ya ubongo. mtoto tangu akiwa tumboni anatakiwa kula vyakula vitakavyoboresha ubongo wake, na vyakula hivyo vingi ni vile vyenye omega3 inayopatikana kwenye ndizi, mafuta ya samaki na parachichi na kiini cha yai. sio hivyo tu, wakati anakua, anatakiwa kula chakula bora, omega3 isipungue pamoja na proteins za kutosha kwasababu ndizo zinamfanya akue.
wakati anaendelea kukua, usimbanie, kila anachotaka kufanya unamchapa, akitaka kucheza michezo fulani unamkataza, etc, kwa watoto wa kibongo, wengi wanalelewa na housegirls na mzazi atamwangalia mtoto akirudi, ukimpatia chakula housegirl anakula chote anampa mauji anashiba, uji usio wa lishe hauna faida na haumfanyi akue wala kudevelop ubongo wake. ubongo ukilishwa vyema kwa vyakula bora ukakua vizuri mtoto IQ inakuwa juu sana.
kwa Africa, wengi tunakula ili tuishi, nilijifunza kitu kimoja, ukiishi na wachina, utajua kuwa wee unakula tu ili uishi lakini hauulishi mwili wako. jamaa wanaweza kula nyama na samaki ambayo wangekula watu wawili, piga maziwa, piga matunda, tandika tandika balaa, na hata akila kidogokidogo anakula mara nyingi. breakfast yao ya ajabu. na vyote hivyo VINATOKANA NA KIPATO, ukiwa na kipato kidogo hautakula vyakula bora na ubongo wako utadorora. wazungu wengi wana uwezo kununua chakula bora kwa watoto everyday na wanawapa nafasi ya kujaribu kufanya mambo mbalimbali, hawachapi watoto na kuwatia hofu kama sisi huku, huku kwetu mtoto anaishi kwa hofu ya kuchapwa tu muda wote na hofu hiyo anakuwa nayo hadi ukubwani. nyumbani, mtaani, shuleni etc anakuwa na hofu tu na kufokewa na kuchapwa hivyo na ubongo wake pia unakuwa hivyohivyo,
vijijini kwetu tulikozaliwa huko unaamka asubuhi unakula viazi au ugali unaenda shamba. kitu pekee utakachofaidika ni mboga za majani ila ugali/viazi ni wanga haujengi mwili, kwahiyo ubongo haulishwi ndio maana vichwa vigumu kuelewa.
tafiti zilifanywa kwenye mikoa ambayo watu wanaishi milimani, uwezo wa kufikiri ni mdogo kwasababu ya weathering ya udogo kwenye mazao wanayolima, madini ya chuma yanachukuliwa na mvua na kupelekwa kwenye mto hadi mabondeni huko, wenyewe kile wanachokilima kule juu hakkina madini ya chuma ambayo pia yanasaidia development ya ubongo. labda kwa siku hizi chumvi wamelazimisha lazima iwekwe madini ya chuma sio kama sisi zamani tulikuwa tunakula ile ya mawe.(wahenga tu wataelewa hapa).
kiujumla, watu weusi kwenye nchu ulizotaja za carrebeans na africa, utaona uchumi wao upo chini sana, hawana kipato cha kuwafanya wale balanced diet, na balanced diet ndio inafanya watu wawe na afya ya akili na ustaarabu.
chukua mfano wa Nigeria, kule kuna vyakula vingi (ni kama tukuyu na bukoba), walipima watu duniani iq, mwaka juzi kuna mtoto mmoja toka nijeria aliibuka kinara. wanachofanya wenzetu wanaiba sana nchi za watu wanatajirika na kurudi kwao. nchini kwao pia kuna matajiri wa kufa mtu kwasababu wanafanya sana kazi, hivyo ukiamua kuchukua sampuli za vipimo, chukua waafrica toka familia mambo safi, waamerica weusi na wanijeria utapata jibu.
on the other side, kuan mambumbumbu ulaya mashariki huo kwenye umasikinini huko, ile former USSR kuna baadhi ya nchi ni maskini kidogo, huko aisee kuna mambumbumbu bora hata waafrica. same applies to Arab countries wale masikini wanajua tu kuswali akili zingine hawana kabisa. tulishe watoto vyakula bora ili wasihangaike baadaye.
Tuna maprofesa na wahandisi wasomi lakini wanashindwa kurekebisha majina tu ya sehemu au vitu kwa mfano Bagamoyo (Bwagamoyo), Tabora (Nnobola), Dar es Salaam (Mzizima), Dodoma (Idodomya) na kadhalika.Sorry kwa watakao feel offended
Africa kuna nchi 54. Nje ya Africa nchi ambazo zina jamii ya watu weusi
Ni za visiwa vya Careebian kama Jamaika , Haiti Buhamas.
Lakini zooteee hizo hamna hata nchi ambayo ni developed nation hata moja!!
Matatizo ya Tanzania , Zimbabwe Congo Namibia sijui Africa ya kati ni yale yale na ya Haiti ni yale yale.
Itoe South Africa ambayo waanchi wake weusi hawamiliki asilimia 80 ya uchumi!! Ukiwa umehodhiwa na wazungu.
Jibu kama mtu usie na mihemuko!!
Umeyanena ya kweli kabisa.Matatizo ya mwafrika chanzo ni mwafrika mwenyewe, nadharia ya kuwatupia lawama wazungu ilianza miaka ya 70 na wajamaa hasa kupitia watawala wa kiafrica waliposhindwa kuwaletea waafrika maendeleo baada ya hadaa ya kuwaaminisha wananchi kwamba tushikamane tumfukuze mkoloni Ili sote tule matunda ya UHURU baada ya wananchi kudanganywa matokeo waliyotegemea hayakuwa,Ili watawala kujikosha juu ya kushindwa kwao wakaja na propaganda za kuwatupia lawama wazungu juu ya kushindwa kwao kutimiza ahadi za maendeleo,wakawatumia waandishi kama kina walter rodney na akaandaa kitabu how europe underdevelope afrika,nk vikaingizwa mashuleni Ili kuwafichia aibu watawala wa kiafrica juu ya kushindwa kwao, awamu iliyopita tumeshuhudia tbc ikitumika kuwaalika maprofesa wa vyuo tena waliosoma silabus zile za zamani zilizojaa chuki wakiwatupia lawama wazungu mwanzo had mwisho wa kipindi Ili liliendana na aina ya Utawala uliopita ,Maana alipotoka mkoloni mweupe akaingia mkoloni mweusi ambae nae akiendeleza ukoloni hata sasa kuwatumikisha waafrika wenzake.Tumeshuhudia watawala wa kiafrica wakijilimbikizia mali ikiwemo kujenga makasri mfano gabolite,mugabe, zuma, Chato,Kabaraki (Moi),nk huku wakizifukarisha nchi zao kwa kushindana kuficha pesa benk za nje,wakisomesha nje,jenga ma kasri nje, wakitibiwa nje badala ya kuboresha huduma za afya nchini mwao.Upo msemo african leaders always die in foreign check habit ya wazulu Zuma ni mwizi kakamatwa,nao wanaingia barabarani kusapoti wizi.Kwa hiyo waafrika wana dini ipi inayofanana.?
Mana kila kabila lilikua na dini yake na mila zake.
Na kabla ya dini za leo waafrika walibaguana sana.
Walidhulumiana sana.
Waliibiana sana.Mpaka leo Wafugaji na wakulima hawaelewani . Mpaka leo wafugaji wanaibiana sana.
Wazungu walikua hivyo hivyo kwa karne nyingi lakini waliketi chini na kurafakari juu ya haki wao kwa wao baada ya kutandikana sana.
Waafrika tuna ubinafsi mkubwa sana.
Dini sio tatizo tatizo ni ule ubinafsi tulio nao. Watu wana roho mbaya Mpaka wanatamani waende peke yao huko Mbinguni. Yaani MTU ameshasikia kuwa Mbinguni ni mahali pazuri anaanza kupigania nafasi ya huko kwa kuua wengine wakati hata hajawahi kufika.
Madaraka watu wanauana kuyatafuta kwa ajili ya kupata maisha mazuri.
Kumbuka Alfonce Mawazo aliuawa na makada wa CCM kwa sababu ya Ubunge. Ubunge ungekua hauna chochote watu wasingeua wengine kwa sababu ya Ubunge.
Waafrika karne hii bado wanauana ndugu kwa sababu ya vyama vya siasa ambavyo havina nafsi wala roho. Ni jina tu KANU. MTU unamuua mwenzako au unamfunga gerezani kwa kesi za uongo na kuumiza familia yake kwa sababu ya neno KANU au CCM. Wenzetu walishaondoka kwenye huo ujinga wa imani Kali za kisiasa kwa watawala ndio maana wanawaza maendeleo zaidi.
Dini ni imani na ni asili ya binadam wa kila taifa. Dini zetu hazikujipambanua juu ya kesho ya mwanadam ndio maana hazikuweza kufua dafu mbele ya dini za Mashariki ya Kati.
Warumi na wagiriki na wamisri ni jamii zilizokuwa zimeendelea na kuelimika sana na zilikua na dini zao lakini walizipima dini za mashariki ya Kati na kuzikubali mana zilizungumzia haki.
Huwezi kuendelea kama hauna jamii inayotenda haki.
Haki ni msingi wa maendeleo kwenye jamii.
Ukipita kwenye shule za serikali baada ya Uhuru utaona vichekesho vitupu. Shule imejengwa ina mwaka mmoja ina nyufa kila mahali. Lakini shule iliyojengwa miaka mia moja iliyopita ipo imara. Ina vyoo vya maji ,n.k. Hapo mzungu na mwafrika anajipambanua wazi kuwa mwafrika ana ubinafsi na roho mbaya.
Dini inakatazo hayo yote.
Watawala wanatumia muda mwingi kulimbukiza Mali kwa ajili ya familia zao bila kujali kundi kubwa la waafrika maskini wanaozaliwa na watakaohitaji vitu kama Afya, makazi,elimu na ajira. Ukiwauliza wanakuambia wazungu wanatuibia. Mtu huyo huyo ni kada wa Chama tawala. Alikua meneja wa chama cha ushirika akaiba na kujenga hoteli. Kwa sababu ni mtandao wa kichama ,akaenda akagombea udiwani akawa Meya au Mwenyekiti wa halmashauri ,akawa anashirikiana na Mkurugenzi ambaye ni kada wa chama wakawa wanajipa tenda za kumwaga matope barabarani kwa kutumia kampuni zao za ujenzi wa barabara . Kila Mwaka wanamwaga vifusi na barabara inaharibika mana wamenunua magreda kwa kujua kuwa barabara wataijenga kwa kiwango duni ili kazi ya kuliibia taifa iendelee. Mzunguko unakua hivyo. Diwani anagombea Ubunge anapata kwa sababu ya rushwa na kupendelewa.
Baadae anakua waziri wa Elimu. Anashirikiana na wahindi kuweka mashine za kuchapisha vitabu.
Anabadili mitaala kila mwaka ili auzie serikali vitabu. Matokeo yake wazazi kila mwaka wananunua vitabu mana vya mwaka jana havimsaidii tena mwanafunzi anayeingia darasa hilo. Waziri huyo anasomesha watoto wake nje. Anatumia fedha nyingi kulipoa ada huko ulaya. Fedha za maskini zinapotelea ulaya.
Mtoto wake anamaliza shule ulaya anakuja kuwa Mkurugenzi wa Ewura. Kampuni inayowanyonya waafrika bila kuzalisha chochote.
Tulitegemea afanye kazi huko Ulaya atuibie teknolojia lakini wapi. Anakuja anaandaliwa kuwa mbunge au mkuu wa Wilaya.
Mzunguko wa kundi la watu wanaonufaika na umaskini na elimu duni ya mwafrika linazidi kuwa kubwa.
Wanaonufaika na umaskini na elimu duni ya mwafrika ni watawala wa Wafrika zaidi kuliko wazungu.
Wazungu watabaki kuwa juu kwa sababu ya roho mbaya za waafrika.
Mfano tu miamala kwenye simu. Mzungu amegundua teknolojia ya mawasiliano lakini waafrika wanaitumia kukomoana na kuchaji pesa nyingi kuliko mgunduzi.
Gari Japan ni bei rahisi kuliko kodi wanayokamua waafrika kwa waafrika wenzao.
Dawa zinatoka India kwa bei Rahisi sana. Lakini zikishakanyaga ardhi ya Afrika zinauzwa ghali sana Mara tatu ya bei yake.Asiyeweza kununua af
Mkuu wakush si wamejivika joho la kiarabu na kuuvaa utume mambaleo na kuua kabisa taifa la kush.Hotep Wakush
Mimi Kisendi Nyanda Ntalima Mpandaligoya nasema hivii, nitarejea kuuzungumza Ukushi na Ufedhuli wa Manguruwe waliotufanyia.
Hotep
Kwanini sasa sisi ndo tusiwe watu wa mwanzo kwenda kuwatawala wazungu.. mpaka mzungu ndo aje kututawala sisi?Waafrica ni watu wenye uwezo mkubwa na wamejaliwa mali nyingi na ustahimilifu wa mazingira magumu. Sifa hizo zote kwa karne nyingi zimekuwa ni hofu kubwa dhidi ya wazungu.
Wanajua tukiweza kujitambua na kuendeleza raslmali zetu watakuwa na wakati mgumu sana, na pengine tunaweza kuwaangamiza na wakapotea, wao ni dhaifu, nchi zao hazina raslmali na hata hali za hewa kwao si rafiki.
Ili wao kuishi wanatutegemea kwa aslimia kubwa, hili liliwafanya wao kujihami mapema. Wakahakikisha wanapora mali zote na kutengeneza mazingira ambayo hatutakuwa kitu kimoja.
Mfano ni kutugawa katika nchi nyingi na kuhakikisha hatuongei lugha moja. Wao wameungana na wanaongea lugha moja, lakini Tanzania na Angola au congo mpk Cameron tuna lugha tofauti tofauti. Vile vile siasa zetu hazikubaliani. Jumuiya ya Africa mashariki tu imeshindikana.
Hivyo yote unayoyaona nchi za watu weusi ni ufefhuli wa mtu mweupe.
Alihakikisha kupitia Dini, vita na saikolojia anatutawala tusije amka na kujitambua kwa hali yoyote ile.
Alitutumikisha kama watumwa, jambo hili lilitudumaza watu weusi na kutuchelewesha kwa takribani miaka hata elfu moja nyuma dhidi yao. Ni kama unaanza mashindano ya mbio halfu mtu anakusukuma unaanguka.
Unatibiwa mpka unakuwa sawa then unaambiwa uendelee na mbio, huku mpinzani wako wakati wote huo yeye anakimbia kwa kasi kuelekea mwisho wa pambano, huku wewe ukikimbia kwa kuchechemea japo unauwezo na sifa zote za kushinda.
Naishia hapa, usijidharau. Tunafanyiwa rafu nyingi sana, kuhakikisha hatutoki hapa tulipo, maana wanajua tutakapotoka wao hawatakuwepo tena.
Nahisi sasa ivi Magufuli alishawaroga malaika ili wamchague yeye (Magufuli) awe kiongozi wao mkuu (wa malaika).Dini sio tatizo tatizo ni ule ubinafsi tulio nao. Watu wana roho mbaya Mpaka wanatamani waende peke yao huko Mbinguni. Yaani MTU ameshasikia kuwa Mbinguni ni mahali pazuri anaanza kupigania nafasi ya huko kwa kuua wengine wakati hata hajawahi kufika.
.
Hostel za Magufuli -UDSMUkipita kwenye shule za serikali baada ya Uhuru utaona vichekesho vitupu. Shule imejengwa ina mwaka mmoja ina nyufa kila mahali. Lakini shule iliyojengwa miaka mia moja iliyopita ipo imara. Ina vyoo vya maji.
Uwanja wa ndege ChatoWatawala wanatumia muda mwingi kulimbukiza Mali kwa ajili ya familia zao bila kujali kundi kubwa la waafrika maskini wanaozaliwa na watakaohitaji vitu kama Afya, makazi,elimu na ajira. Ukiwauliza wanakuambia wazungu wanatuibia..
Hotel ya Magufuli Chato.Mtu huyo huyo ni kada wa Chama tawala. Alikua meneja wa chama cha ushirika akaiba na kujenga hoteli.
Nyanza construction (ya Magufuli akishirikiana na wahindi).Kwa sababu ni mtandao wa kichama ,akaenda akagombea udiwani akawa Meya au Mwenyekiti wa halmashauri ,akawa anashirikiana na Mkurugenzi ambaye ni kada wa chama wakawa wanajipa tenda za kumwaga matope barabarani kwa kutumia kampuni zao za ujenzi wa barabara . Kila Mwaka wanamwaga vifusi na barabara inaharibika mana wamenunua magreda kwa kujua kuwa barabara wataijenga kwa kiwango duni ili kazi ya kuliibia taifa iendelee. Mzunguko unakua hivyo..
Tulishamshtukia Magufuli na somo lake uchwara la "Historia ya Tanzania". Alitaka kupiga pesa.Diwani anagombea Ubunge anapata kwa sababu ya rushwa na kupendelewa.
Baadae anakua waziri wa Elimu. Anashirikiana na wahindi kuweka mashine za kuchapisha vitabu..
Anabadili mitaala kila mwaka ili auzie serikali vitabu. Matokeo yake wazazi kila mwaka wananunua vitabu mana vya mwaka jana havimsaidii tena mwanafunzi anayeingia darasa hilo.
Sorry kwa watakao feel offended
Africa kuna nchi 54. Nje ya Africa nchi ambazo zina jamii ya watu weusi
Ni za visiwa vya Careebian kama Jamaika , Haiti Buhamas.
Lakini zooteee hizo hamna hata nchi ambayo ni developed nation hata moja!!
Matatizo ya Tanzania , Zimbabwe Congo Namibia sijui Africa ya kati ni yale yale na ya Haiti ni yale yale.
Itoe South Africa ambayo waanchi wake weusi hawamiliki asilimia 80 ya uchumi!! Ukiwa umehodhiwa na wazungu.
Jibu kama mtu usie na mihemuko!!
Mungu akupe maisha marefu . Ikiwezekana utunge kitabu kuwaeleza watoto na wajukuu zetu ukweli.Umeyanena ya kweli kabisa.Matatizo ya mwafrika chanzo ni mwafrika mwenyewe, nadharia ya kuwatupia lawama wazungu ilianza miaka ya 70 na wajamaa hasa kupitia watawala wa kiafrica waliposhindwa kuwaletea waafrika maendeleo baada ya hadaa ya kuwaaminisha wananchi kwamba tushikamane tumfukuze mkoloni Ili sote tule matunda ya UHURU baada ya wananchi kudanganywa matokeo waliyotegemea hayakuwa,Ili watawala kujikosha juu ya kushindwa kwao wakaja na propaganda za kuwatupia lawama wazungu juu ya kushindwa kwao kutimiza ahadi za maendeleo,wakawatumia waandishi kama kina walter rodney na akaandaa kitabu how europe underdevelope afrika,nk vikaingizwa mashuleni Ili kuwafichia aibu watawala wa kiafrica juu ya kushindwa kwao, awamu iliyopita tumeshuhudia tbc ikitumika kuwaalika maprofesa wa vyuo tena waliosoma silabus zile za zamani zilizojaa chuki wakiwatupia lawama wazungu mwanzo had mwisho wa kipindi Ili liliendana na aina ya Utawala uliopita ,Maana alipotoka mkoloni mweupe akaingia mkoloni mweusi ambae nae akiendeleza ukoloni hata sasa kuwatumikisha waafrika wenzake.Tumeshuhudia watawala wa kiafrica wakijilimbikizia mali ikiwemo kujenga makasri mfano gabolite,mugabe, zuma, Chato,Kabaraki (Moi),nk huku wakizifukarisha nchi zao kwa kushindana kuficha pesa benk za nje,wakisomesha nje,jenga ma kasri nje, wakitibiwa nje badala ya kuboresha huduma za afya nchini mwao.Upo msemo african leaders always die in foreign check habit ya wazulu Zuma ni mwizi kakamatwa,nao wanaingia barabarani kusapoti wizi.
Ukweli halisi ni kwamba sisi wenyewe ndo twapaswa kulaumiwa juu ya matatizo yetu.Tuna kila kitu ambacho wao hawana lkn sababu ya kukosa uongozi bora ni ngumu kusonga, hatuna institution inayofanya Kazi ya kutoa maarifa ya watz wazione fursa zinazowazunguka na wazitumie kuboresha maisha yao.Maana umasikini tafsiri yake ni ukosefu wa maarifa ya kuziona fursa zinazomzunguka mtu Ili azitumie au kuzigeuza kuwa raslimali.Hatuwezi walaumu watu waliondoka miaka 60 iliyopita huku wakiacha KILA kitu zaidi ya kuchukua mabegi yao tu na kuacha ardhi, mashamba,migodi, viwanda,maji,nk.Kama wao waliweza kuvitumia sisi tunashindwa nini kuvitumia.Kutawaliwa hakuifanyi nchi kuwa masikini au kutokupelekwa shule na mzazi sio kigezo cha wewe kutokuwa na maendeleo,wengi awakupelekwa na Wana maendeleo.Kila nchi duniani iliitawala na nyingine mfano Japan alitawala China, UK India, UK USA,Spain Latin America, baada ya UHURU walipata viongozi sahihi wakaendelea
Fikra hasi, Mtu mweusi anajiona yeye siku zote yuko chini ya mtu mweupe huu tunaita ni utumwa ki fikra. Hakika kama mtu mweusi atabadili fikra atalitambua kusudi lake la kuwepo duniani na kuamin kuwa yeye ndo mwajibikaji wa kwanza na si kusubiri kufanyiwa. R.i.p JPM
Ubinafsi, mtu mweusi ni mbinafsi wa hali ya juu mfano mzuri ni viongozi walio na uchu wa madaraka wakiyapata wanajiangalia wao na si kwa maslahi ya wengi.
Mtu mmoja akifanikiwa katika jamii yake(ukoo) hawezi kuinua wengine furaha yake kubwa ni kunyenyekewa. Angalia matajiri wengi wa africa maisha yao ni mazuri sana lakin wanaowazunguka ni kinyume chake. Vipi huyo boss wako aliyepewa madaraka na mzungu anasimamia vyema maslahi yako ama ndo wa kwanza kukandamiza?
Ubaguzi, kibaya zaidi tunabaguana sisi kwa sisi kwa kigezo cha udini na ukabila. Hakuna kiumbe mbaguzi kama mtu mweusi na fikiri sote ni mashaidi hata maofisini tunaona.
Hakuna binadamu mwenye akili nyingi zaidi ya mwingine kinachoathirika ni fikra tu na namna ya matumizi. Acha ubaguzi, ubinafsi na badili mtazamo wako wewe ni kiumbe mwenye uwezo mkubwa sana peleka kwenye matendo.