Kwanini wafanyakazi wengi wa Serikali wanapenda kutengeneza mazingira ya kupewa hela katika huduma wanazotoa?

Kwanini wafanyakazi wengi wa Serikali wanapenda kutengeneza mazingira ya kupewa hela katika huduma wanazotoa?

October nilifika ofisi ya TRA kwaajili ya kufanya makadirio ya kodi. Tumefanya nikaomba kupunguziwa yule afisa akapunguza, wakati naondoka akaniambia unajua nimepunguza lakini nimejiweka kwenye risk boss wangu akisikia ataniletea shida sana, kwahiyo angalia namna yoyote na mimi niishi. Niliondoka nikalipa kodi yeye sijampa chochote. Alinipigia akaniambia nitambue tu mwezi wa kwanza na wa pili Kuna makadirio tena, nikamwambia sawa. Nahisi nikimkuta yeye atataka nilipe Kodi ya kufilisi biashara [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Hapo na wewe hukuwa mustaarabu kama umeshakubaliana jambo na mtu ulipaswa ulitende. Usijisifie kwa hilo
 
Wewe unataka tule wapi, hii nchi ilishakwenda na Maji.

Ni wapi hakuna rushwa, Askari barabarani anapokea live bila Chenga unataka sisi tufanye nini
Tatizo lenu wengine mnajipangia hadi bei kubwa kwenye rushwa, mnatakiwa kupokea chochote kile utakachopewa baada ya kazi kama shukrani tu, na kama mteja hana kitu msifanyie ubaya!!
 
Mi nilikuja kupatwa butwaa mwaka huu mwanzoni ..kuna MTU ana kesi Mahakama kuu ..lakini haiendi ..

Kila mwezi tarehe ... Sasa tukiwa kwenye sherehe flani akasikia MTU anasema nilimaliza kesi yangu miezi 6 tuu .. Ikabidi aombe maelezo kwa mhusika ..
Akaambiwa ni pesa yako ndio inamaliza kesi mapema ..

Huwezi amini pesa kwa hapa Bongo inalainisha mambo mengi hasa ofisi za Serikali kwa uharaka ..

Kuna MTU alidai pension kidogo awe kichaa ...ila alipokubali kutoa cha juu ..mwezi haukuisha hela ikaingia kwenye account.. Yaani ni mfumo ndani ya Serikali
 
Ni kutokana na mfumo wa Serikali kuu kuomba omba pesa za misaada.Watoto wakimuona baba na Mama wanapenda kuomba omba na wao hufanya hivo.KAWAIDA NI KAMA SHERIA.
 
Hao TAKUKURU hawafanyi kazi waliopewa kuwasaka waomba rushwa. Wanangoja wapewe ripoti kuwa mahali fulani kuna mazingira ya rushwa ikisha na wao wanajiunga na kuwaomba hao wapokea rushwa wawape gawio lao.
Rushwa imekua ni kitu kinachochukuliwa kama ni sawa katika jamii.
 
ACHA WATU WALE RUSHWA TU

HUKO JUU KWENYEWE WANAPIGA

HELA NDEFU, UNAFIKIRI WACHINI NAYE ATAJISIKIAJE

ova
 
ACHA WATU WALE RUSHWA TU

HUKO JUU KWENYEWE WANAPIGA

HELA NDEFU, UNAFIKIRI WACHINI NAYE ATAJISIKIAJE

ova
Sasa hawa watumishi wa chini wao wanawaumiza sana wanyonge, sasa mtu kazulumiwa shamba lake na tajiri anaambiwa atowe pesa ili apewe msaada sasa huyo mnyonge hiyo pesa atapata wapi!?
 
Kma viongoz wanapatikana kwa mchakato wa rushwa
 
Yaani wee acha tu maana imebidi sasa nimwombe Mungu maana haki yako upati mpka utoe rushwa. Nimefuatilia hati ya kiwanja changu kwa zaidi ya miaka ishirini bila mafanikio. Huko pembeni unaambiwa bila kuto chochote upati na ni kweli kila ukienda wanakuwekea mazingira ya rushwa. . Baadaye nikaamua tu kuwaachia mpaka hapo watakapoona wenyewe kunipa au Mungu afanye ukuu wake apindue mambo na kuleta watu wanaojali watu. Kwa sasa hivi maskini anapata shida sana nchi hii maana kupata haki ni majaliwa. Mungu anawaona ninyi nyote mnaofanya dhuluma mwogopeni Mungu angalau basi. Pesa mnazokusanya hamwezi kwenda nazo kaburini na hayo majumba manayojengwa kwa rushwa hamtakaa na watoto wenu watatafunwa na laana. Ole wenu ninyi nyote mnaopindisha haki za watu maana Mungu hatakapoamua kuwaweka uchi mtakuwa uchi kwekweli.
 
Mzuka,

Hivi ni Serikali haiwalipi watumishi wake au shida ni nini?

Yaani unaenda kufata huduma ofisi za Serikali lakini mtoa huduma muda wote anatengeneza mazingira ya kupewa hela (rushwa).

Ofisi imeandikwa kabisa huduma hiyo ni bure lakini yeye anataka umpe hela akusaidie wakati hilo ndo jukumu lililomuweka pale, mfano nilifata TIN number ya kampuni ukiingia tuu kwenye ofisi zao unaona kabisa kumeandikwa TIN number ni bure lakini lenyewe lilivyo-lijinga linataka kitu kidogo RUBBISH.

Halmashauri na TRA zimejaa rushwa.

Kuna ofisi nyingine tena huko kanda ya ziwa ya TRA nilienda kufanyiwa makadirio ya kampuni mpya badala ya kunieleza jinsi ya kufanya linataka nilipe laki tano linifanyie makadirio ambayo ni kitu cha bure, yaani wakiona mtu mzee mzee umekaa ki-mbugila mbugila wanaamini huelewi kitu wanataka uwape hela wakupe huduma.

Hili jambo limenikasirisha sana itabidi nipambane familia yangu isihangaike na ajira ambazo ni kama wizi.

Swali
Serikali hamuwathamini wafanyakazi wenu hadi wamekuwa wanatamani fedha za wananchi kiasi hiki?
Kuna vitu vingine huwa nasi tunavitaka wenyewe. Sasa hapo TRA wameshaweka TIN bure mtu anakuambia nipe kitu kidogo kwanini usimuione mkuu wake hapo au hata CG wao Kidata uone huyo muomba rushwa nini kitamkuta. Bora TRA wao wamewapa somo TIN bure bango lipo na inashangaza na wewe unakubali , tatizo naliliona na sisi tunachangia kutaka vitu kwa haraka hasa unapokuta wenzako wamekutangulia kwenye foleni. Mimi Ardhi kuna mtu alitaka mazingira ya kunitoa Rushwa nikamtafuta naibu waziri mbona jamaa jasho lilimtoka kila akiniona nyaraka yangu faster mara ooooh ilikuwa haina haja ya kwenda huko tungeyamaliza nilimjibu nishamaliza. Dawa ni kuwaripoti tuu na niwapongeze TRA kwa kuweka matangazo hayo
 
alafu wanataka waende mbinguni na madhambi yote wayafanyayo...wazinzi wenyewe, wezi wenyewe, waongo wenyewe, wapenda rushwa wenyewe, n.k hovyo kabisa
 
Kuna vitu vingine huwa nasi tunavitaka wenyewe. Sasa hapo TRA wameshaweka TIN bure mtu anakuambia nipe kitu kidogo kwanini usimuione mkuu wake hapo au hata CG wao Kidata uone huyo muomba rushwa nini kitamkuta. Bora TRA wao wamewapa somo TIN bure bango lipo na inashangaza na wewe unakubali , tatizo naliliona na sisi tunachangia kutaka vitu kwa haraka hasa unapokuta wenzako wamekutangulia kwenye foleni. Mimi Ardhi kuna mtu alitaka mazingira ya kunitoa Rushwa nikamtafuta naibu waziri mbona jamaa jasho lilimtoka kila akiniona nyaraka yangu faster mara ooooh ilikuwa haina haja ya kwenda huko tungeyamaliza nilimjibu nishamaliza. Dawa ni kuwaripoti tuu na niwapongeze TRA kwa kuweka matangazo hayo
umemaanisha mimi nilikubali kutoa kitu kidogo?
 
Back
Top Bottom