Kwanini wakatoliki wanamuomba Mungu awajalie moyo wa ufukara na siyo ya utajiri kama vile Mungu alivyosema atatubariki?

Lakini biblia ipo wazi siyofumbo gumu kulicompare na maisha kama mnavyotuaminisha .

Ufukara haujawahi kutajwa kwa maana hiyo unayoisema kwenye biblia mkuu.., maandiko yamefafanua kabisa ufukara ni nini
Biblia ni falsafa ngumu:

Rejea swali lako, utasemaje kuhusu Yesu kuwaambia watu,
Mt 5:3-12
Heri walio maskini wa roho; Maana ufalme wa mbinguni ni wao. Heri wenye huzuni; Maana hao watafarijika. Heri wenye upole; Maana hao watairithi nchi.

Je, Mungu anataka tuwe wenye huzuni? Mbona andiko jingine linasema, "furahini katika Bwana"?

Katika falsafa ya kiimani ufukara au umaskini unaozungumziwa ni ule wa Roho, siyo mali. Na ufukara wa Roho, ni ile hali ya kujiona wakati wote umepungukiwa, na hivyo kuishi kwa kumtegemea Mungu. Utajiri wa Roho humaanisha kuwa umejitosheleza kila kitu, na hivyo Mungu hana nafasi katika maisha yako.
 
Lakini biblia ipo wazi siyofumbo gumu kulicompare na maisha kama mnavyotuaminisha .
. Sisi wakatoliki hatuamishi mtu yeyote kuhusu masuala ya dini, bali yeye mwenyewe inabidi aamini kwa moyo wake mkunjufu,

. Ingawa nyinyi waislam suala la kuaminisha mtu dini ndo mmeweka kipaumbele zaidi na kufikia hatua ya kutukana matusi dini za upande wa pili.

Ufukara haujawahi kutajwa kwa maana hiyo unayoisema kwenye biblia mkuu.., maandiko yamefafanua kabisa ufukara ni nini
Yesu alizaliwa katika mazingira duni huko Bethlehemu, akionyesha unyenyekevu na ufukara( hakuwa na kitu bali kilichopatikana walikula kwa pamoja) , jambo ambalo Wakristo wanaalikwa kuliiga. Ndiyo maana katika sala hii, waumini tunaomba "moyo wa ufukara," roho ya unyenyekevu, ukarimu, na kutokufanya mali kuwa kipaumbele cha maisha..
 
Hawa watu Tangu nimesikia wakisema "bikira mariamu utuombee sisi wakosefu" ndipo nilipowadharau!
Kwani walikuambia uwatukuze au uwaheshimu? Hawaombi ili wewe uwaheshimu. Tena ukiwadharau katika jambo jema, ni baraka kwao.q
 
Kuna jamaa yuko mtandaoni amewananga sana anasema wanaabudu mfuko wa cement na hawajajitokeza kukanusha
 
Ninahisi ww ni mmojawapo wa kwenye lile kundi la "7to" ambao wamebobea kila siku na kila wakati kuelekeza mashambulizi uchwara kwa Wakatoliki. Kwani usipofanya hivyo unapungukiwa na nini?
Nakushauri hivi: Keti chini,tulia halafu anza kusema"Nasadiki kwa Mungu mmoja.... ....nasadiki kwa kanisa moja takatifu katoliki la Mitume.....Naungama ubatizo mmoja kwa.......... uzima wa milele Amina." Ukimaliza hapo; kunywa maji kidogo halafu endelea na mishe zako. Achana na Wakatoliki.
 
Atukuzwe baba mwana na Roho Mtakatifu kama mwanzo na sasa na siku zote milele Amina!

Bwana utuhurumie,

Bwana utuhurumie,

Utuhurumie

Kristo utuhurumie

Kristo utuhurumie

Utuhurumie

Bwana utuhurumie,

Bwanaa utuhurumie

Utuhurumie

Kristo utusikilize,

Kristo utusikilize,

Utusikilize,
 
Atukuzwe baba mwana na Roho Mtakatifu kama mwanzo na sasa na siku zote milele Amina!

Bwana utuhurumie,

Bwana utuhurumie,

Utuhurumie

Kristo utuhurumie

Kristo utuhurumie

Utuhurumie

Bwana utuhurumie,

Bwanaa utuhurumie

Utuhurumie

Kristo utusikilize,

Kristo utusikilize,

Utusikilize,
 
Kama hutuelewi sisi wakatoliki...tafadhali endelea na maisha yako.. hatujivuni wala hatuhubiri miujiza ya utajiri..
 
Na Nyerere alipita humohumo na kuweza kutawala kwa miaka 30
huku akiwaita wanyonge
 
Tabia za mtu fukara zikoje? Unyenyekevu, kutii amri na mengine mengi
 
Kwanza kabla yakujadili yakupasa ujue maana ya neno MOYO WA UFUKARA hapo ndipo ujumbe halisi utapatikana
 
Kuna jamaa yuko mtandaoni amewananga sana anasema wanaabudu mfuko wa cement na hawajajitokeza kukanusha
Alichokuwa anaongelea ni kile kuwa wanachukua simenti na nzege wanachanganya wanatengeneza sanamu ya bikira maria halafu wanaisimamisha wanaanza kusali mbele yake ndio akasema wanaabudu simenti na nzege
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…