Kwanini Wakenya hawajui kiswahili!!!

Kwanini Wakenya hawajui kiswahili!!!

mmmmmmmhhhh...wasije wakaweka nauli rahisi vile ngoma ikuamia jiani!!!
18765789_1559709567395087_4632006650918347915_n.jpg
 
Nikiwasikiliza wakenya matamshi yao,huwa naskia kichefuchefu,mfano siku ile watoto waarusha walipopata ajari nilimsikia raisi wao kwenye kampeni akisema "nawauliza ndugu zangu tusimame dakika moja kuwaombea watoto...." Kwa hiyo ndugu zangu jitaidini kuongea vizuri kama watz,Rwanda Burundi ,Zanzibar Nk

Huyu ni M'BONGO KUTOKA DAR

 
Ndio maana nikasema mnatia huruma, uandishi wenu kwenye lugha ya Kiswahili ni majanga.
'Hovyo' na 'ovyo' ni vivumishi na pia ni visawe.
'Jamani' na 'Jameni' ni visawe pia.
Hahahaahha haaaya we mjuaji maana unabishana na kamusi... unaambia uandike kwa ufasaha unaleta habari za vivumishi na viwakilishi... fundisha na ngeli kabisa chaaaa
 
Jamaa huwa wanajidai eti Wana swaga za kizungu hahaha!
 
Lugha tunaifaham, tatizo kubwa linalotusibu ni kutokuwa makini pale tunapotumia lugha ya maandishi (written) na lugha ya maongezi (oral/spoken).

Watanzania wengi hatuko makini kwenya written language (sio kiswahili tu, ni lugha nyingi tunapuuzia vitu vya msingi),

Lakini pia kwa sababu ya asili (mother tongue) inachagiza suala hilo! Hapa tz kuna makabila mengi sana, kuna baadhi ya makabila wao wanachezesha sana ndimi zao, hivyo "R" inatamkwa haraka zaidi kuliko L, wengine ndo hivyo hawezi kutumia R badala yake huweka L kila sehemu, iko mifano mingi!

Hata hivyo hii haiondoi dhana kwamba hatukijui hata hicho kiswahili, La hasha! Ni kukosa umakini tu kwa baadhi ya watu!

Suala la Wakenya kuajiriwa kwa wingi na makampuni makubwa ya kimataifa lina sababu nyingi!

Tuanzie kwenye ile video ya kwanza inayozungumzia maisha ya Yesu, baada ya Mkenya mmoja kuwa amepata tenda ya kuingiza maneno ya Kiswahili kwenye video ile, jamii ya kimataifa iliifahamu Kenya kama kitovu cha kiswahili na hapo ndo nyota yenu iling'aa! Lakini kiswahili kilichoingizwa kilikuwa hakijanyooka!

Baada ya hapo hao Wakenya wachache walikuwa ni kivutio kwa wenzao, zikitokea nafasi huko walikuwa wanawataarifu haraka wakenya wenzao hivyo wakajikuta wakiongezeka!

Lakini kama unafuatilia vizuri masuala, wakati Facebook wametoa tenda kwa wakenya kutengeneza Menu ya kiswahili, waliomba msaada kwa watanzania ili kuingiza kiswahili kilichonyooka! Mtu kama Prof Masamba amefanya kazi kubwa tu ya kutengeneza ile menu!



Pamoja na hayo mambo nihitimishe kwa kusema, Kiswahili sio cha Tanzania pekee, ni cha Africa Mashariki na kati! Kwa hiyo hata kama ni Mkenya au Mtanzania au Mrundi anakikuza nje ya mpaka ni jambo jema! Zaidi ni kuona kiswahili kikikua!
Lakini tukubali ukweli ya kwamba ni wakenya ambao wako katika mstari wa mbele kabisa katika harakati za kuendeleza kiswahili na kuifanya kupata hadhi ulimwenguni. Wasomi wengi wanaojihusisha katika harakati hizi kama kutafsiri programu za kompyuta ama ripoti, mfano zile za Umoja wa Kimataifa nk, wahadhiri wa Kiswahili katika vyuo vikuu vya nchi za mbali zinazofunza lugha hii ni wakenya.
Sina uhakika kuhusu ukweli wa maadai nimewahi kusikia ya kwamba hata hizi maneno zinazotumiwa katika ICT kama utandandawazi, viungambali vilibuniwa na wakenya.

Sidhani hawa wakenya waliojihusisha katika kutafsiri lugha za menu za kompyuta walitafuta usaidizi ya watz eti kwasababu kiswahili chao hakikuwa sawa, bali ilikuwa tu kutafuta kuweka maneno ambayo yangekubalika na wazungumzaji wa lugha hili kutoka pande zote.

Je, umewahi kuinstall programu ya Microsoft kwenye kompyuta? Hapo.kwenye menu wanakoulizia ni lugha gani ungependa litumike, utaona English (UK), English ( US), ikija kwa Kiswahili ni (Kenya).
Kiswahili kinahusishwa zaidi na Kenya.
kwasababu wakenya ndio wapo katika kipaumbele kukiendeleza na kupata kutajika kote ulimwenguni.

Harakati zetu hizi za kuhamasisha dunia kuhusu eneo letu la Afrika mashariki ndizo zimepeleke hata mlima Kilimanjaro na Serengeti na wamasaai kuhusishwa zaidi na Kenya, huku nyinyi mkidhani tunawaibia heritage zenyu.
 
Mbona unaweka nomino mbele ya vihisishi na vivumishi ....hahahahhahaha
Sikutumia kihisishi hata kimoja, duh! Hehehehe! Kwa mwendo huu tutaogopana humu na kuishia kuandika sentensi moja moja kwa makini.
 
Mbona unaweka nomino mbele ya vihisishi na vivumishi ....hahahahhahaha
Tukianza kusisitiza ya kwamba lugha ni sharti litumiwe kwa kufuata sheria na katitika uhalisia wake, na kwamba tutashinda tukisahihishana makosa madogo madogo, basi hapo lugha itapoteza utamu wake pamoja na ubunifu.

Haya makosa madogo ni heri kuyasamehe tu.
 
kiswahili chetu badooo....mombasani hapo!!!

OFFICIAL OPENING OF UWANJA WA MBUZI MINI-STADIUM
Source

Quote:
⁠⁠⁠It was fun galore last night at the inauguration of Uwanja wa Mbuzi Mini Stadium in Kongowea as we played the maiden match between the Mombasa Legends and Team 001. The modern stadium is fitted with Astro Turf Pitch, changing rooms, flood lights and has a capacity of over 2000 people. We will continue to develop such world class facilities around the County, to nurture the sporting talents of our youth and make them be competitive globally in the sports industry.
18671306_1403717353019940_2012666020856371780_n.jpg


18670840_1403720059686336_6480047464915249918_n.jpg


18664531_1403718469686495_169981300852490664_n.jpg


18700126_1403720346352974_1069400874124842516_n.jpg


18698282_1403720496352959_2146410686082079603_n.jpg


18698261_1403717146353294_6133760889423627577_n.jpg


18765701_1403717729686569_6680491887326656158_n.jpg


18698319_1403718003019875_4523067771015220492_n.jpg
sisi tulishakijenga hichi tangu 2014 nyie ndo mmeibuka sasa hivi..
 
Wakenya kuzungumza kiswahili kizuri kama watz mtasubiri sana
 
Mimi naona sababu watanzania hawajui kiingereza
 
sisi tulishakijenga hichi tangu 2014 nyie ndo mmeibuka sasa hivi..
Kukosa elimu ni shinda.....wewe ata kupewa elimu tofauti kati gauge za standard,cape Na meter rail itakua kupoteza muda...bye
 
Sikutumia kihisishi hata kimoja, duh! Hehehehe! Kwa mwendo huu tutaogopana humu na kuishia kuandika sentensi moja moja kwa makini.
Hahahahahah jipe moyo unajua sana kiswazi... yale yale ya kusema treni imetia nanga hlf unaona umepatiiiaaa haahhahaha
 
Tukianza kusisitiza ya kwamba lugha ni sharti litumiwe kwa kufuata sheria na katitika uhalisia wake, na kwamba tutashinda tukisahihishana makosa madogo madogo, basi hapo lugha itapoteza utamu wake pamoja na ubunifu.

Haya makosa madogo ni heri kuyasamehe tu.
Umeona eeee ... nimekuelewa ila watu wanajifanya kukosoa watu hlf wanaandika sentensi kinyume nyume ukiwaambia wabishi kama nini
 
'Rugha' ndio nini, jameni mnatia kichefuchefu, uandishi wenu wa Kiswahili ni ovyo, Kingereza kilishawapiga chenga, lugha zenu za asili ziliwashinda eti mnasema ni ushamba, mnaishi kama watu wasiokua na asili yaani watumwa.
Kuna posti hapo imesema kuwa mlikosa msimamo wa lugha. Kiswahili hovyo,Kiingereza hovyo kina lafudhi kama vilugha vyenu vya asili.
 
Kuna posti hapo imesema kuwa mlikosa msimamo wa lugha. Kiswahili hovyo,Kiingereza hovyo kina lafudhi kama vilugha vyenu vya asili.

Kaka, nchi yetu sasa ina umri wa miaka zaidi ya 50 tangu tupate uhuru, hivi unataka kusema tumekua tukitumia nini kuwasiliana. Leo hii tunaongoza ukanda huu wote kiuchumi, kielimu na kila kitu.
Ifahamike kwamba sisi tunajivunia uwezo wa kuongea lugha nyingi, kwanza tunaenzi lugha zetu za asili, halafu Kiswahili ambacho kilibuniwa kwenye Pwani zetu kwa ushirikiano wa Mwarabu na Waafrika, tunaongea Kingereza na kuna baadhi yetu wanatumia lugha zingine za kigeni.

Nyie hapo mumekomaa na lugha moja ya Kiswahili, halafu uandishi wenu wa Kiswahili hutia kichefuchefu, hebu pitia alichoandika mleta mada ambaye amejikita kwenye kukosoa Wakenya, ameandika sentensi chache lakini zimejaa majanga kwenye uandishi. Tatizo mnafikiria Kiswahili mnachoongea kitaa ndio fasaha, na mara nyingi ndio mnaandika huku JF, watu wa buku jeru.

Tatizo ujamaa uliwafundisha nyie kuishi maisha ya kufungiwa kwenye mfumo mmoja bila kuthubutu mapya, kawaida yenu hutiririka kwenye kitu kimoja bila yeyote kujitolea na kuthubutu chochote kipya. Mumekomaa kwenye lugha moja (ambayo uandishi wenu wa ovyo), halafu stakabadhi zenu muhimu zote zimeandikwa kwa Kingereza, na ndio maana huwa mnaibiwa kwenye hilo shamba la bibi, mna kila kitu, madini, ardhi kubwa yenye rotuba, vivutio bora vya utalii n.k. lakini leo hii bado mnatajwa kwenye nchi maskini wa kutupwa Afrika.
Naskia leo hii ndio mnashtuka eti mumekua mkiibiwa kwenye mchanga wa dhahabu....hehehehe!!
 
Lakini tukubali ukweli ya kwamba ni wakenya ambao wako katika mstari wa mbele kabisa katika harakati za kuendeleza kiswahili na kuifanya kupata hadhi ulimwenguni. Wasomi wengi wanaojihusisha katika harakati hizi kama kutafsiri programu za kompyuta ama ripoti, mfano zile za Umoja wa Kimataifa nk, wahadhiri wa Kiswahili katika vyuo vikuu vya nchi za mbali zinazofunza lugha hii ni wakenya.
Sina uhakika kuhusu ukweli wa maadai nimewahi kusikia ya kwamba hata hizi maneno zinazotumiwa katika ICT kama utandandawazi, viungambali vilibuniwa na wakenya.

Sidhani hawa wakenya waliojihusisha katika kutafsiri lugha za menu za kompyuta walitafuta usaidizi ya watz eti kwasababu kiswahili chao hakikuwa sawa, bali ilikuwa tu kutafuta kuweka maneno ambayo yangekubalika na wazungumzaji wa lugha hili kutoka pande zote.

Je, umewahi kuinstall programu ya Microsoft kwenye kompyuta? Hapo.kwenye menu wanakoulizia ni lugha gani ungependa litumike, utaona English (UK), English ( US), ikija kwa Kiswahili ni (Kenya).
Kiswahili kinahusishwa zaidi na Kenya.
kwasababu wakenya ndio wapo katika kipaumbele kukiendeleza na kupata kutajika kote ulimwenguni.

Harakati zetu hizi za kuhamasisha dunia kuhusu eneo letu la Afrika mashariki ndizo zimepeleke hata mlima Kilimanjaro na Serengeti na wamasaai kuhusishwa zaidi na Kenya, huku nyinyi mkidhani tunawaibia heritage zenyu.
Ukweli kuwa Wakenya ni wengi kwenye taasisi za kimataifa kuliko Watanzania unaweza usiwe na ubishi, lakini una sababu zake! Hata hivyo tofauti hiyo inazidi kupungua ukilinganisha na huko nyuma! Najua takwimu sahihi sio rahisi kuzipata lakini ukiongea na watu wanaofanya kazi sehemu hizo wanashuhudia hilo!

Watu wanatakiwa kujua kwa nini pengine wakenya wengi walichomoza na kupata tenda za kufanya tafasiri ya kiswahili,

Kwanza tujue hao wanaotaka hiyo tafsiri ni wazungu, ambao wengi wao ni waongeaji wa kiingereza! Na tujue kuwa huku Africa, ujuzi wa kwanza na teknojia uliingia na bado inaendelea kuingia kupitia lugha ya kiingereza! Kwa mantiki hiyo, hao wazungu wakati wanakitafuta kiswahili waliangalia kati ya nchi zinazoongea kiswahili ni ipi nchi yenye kuongea lugha zote walau kwa ufasaha, ndipo Kenya ilipata hiyo tenda maana watu wa pwani wako vizuri tu kwa kiswahili! Hapo ndipo makampuni yakaanza kumiminika huko kabla hayajafanya ujuzi vizuri utafiti kujua wapi kiswahili kina rafudhi nzuri!


Wewe ukitaka kujua kuwa hiyo kazi mnapewa lakini hamuitendei haki angalia tu kwenye google, yaani ukijiroga eti utoe kiingereza kiwe kiswahili utacheka uvunjike mbavu kwa sarufi utakayoiona! Angalia hata kiswahili mlichowatengenezea Microsoft kwenye window 7 hata hakijulikani, ku install ile window utalazimika kutumia uzoefu wa icons tu ili kazi iende.

Kuhusu kwenye uchaguzi wa kugha kukutana na kiswahili kimeandikwa Kenya, hicho ni kitu walichofanya wakenya wenyewe ili kuaminisha ulimwengu kuwa kiswahili kinaongelewa Kenya ili waendelee kupata soko!


Cha ajabu kabisa kinachinishangaza kwenu wakenya ni hiki,
Kiswahili kinapokuwa fursa wakenya wanaking'ang'ania kuwa ni chao, kwenye maongezi ya kawaida utaona wanaruka futi mia eti hawakitaki na hakina faida[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]


Akili zenu mnazijua tu wenyewe[emoji13] [emoji13] [emoji13]
 
Wanaoharibu kiswahili kenya ni WAKIKUYU, WAJALUO na wengine nisio wajua, wao ni kama wahindi au wasomali hata uwachape viboko wataongea maneno wanaoyajua wao lakini ukitaka kiswahili safi kilichonyooka kipo MOMBASA hata watangazaji wengi wa radio na TV program za kiswahili kenya nafikiri ni watu wa mombasa kama LULU HASSAN wa citizen
 
Back
Top Bottom