Kwanini Wakristo tunashinikiza kufunga macho tunapoomba wakati siyo takwa?

Kwanini Wakristo tunashinikiza kufunga macho tunapoomba wakati siyo takwa?

NetMaster

JF-Expert Member
Joined
Sep 12, 2022
Posts
1,454
Reaction score
4,925
african-american-man-praying-and-reading-the-bible.jpg

hata Yesu alivyoomba alifumbua macho huku akiangalia juu mbinguni .. YOHANA 17:1
Usiku wa juzi nikiwa nikiwa kwenye maandalizi ya kulala, kama kawida yangu huwa ni lazima nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya, utimamu na amani aliyonipa. Kwa siku hio kabla ya kulala nikajiuliza swali kwanini huwa tunafumba machoo wakati runaomba? Binafsi imekuwa ni utamaduni kabisa ni lazima nifumbe macho nikiwa naomba kabla ya kulala, kabla ya kula, kuanza na kumaliza safari, n.k.

Nimefanya uchunguzi na kubaini kwamba hakuna sehemu yoyote kwenye Biblia iliyotutaka tufunge macho bali tuelekeze imani yetu kwa muumba wetu pale tunapomuomba.

Nadhani kufunga macho iwe ni pale tu ambapo mtu yupo mazingira yanayomuondoa umakini akifungua macho na ikibidi azibe pia masikio endapo kuna makelele yanayomtoa umakini, lakini katika sehemu iliyo na utulivu hasa tunapoomba vyumbani usiku tulivu wakati wa kulala na kanisani mda wa kuomba ambao panakuwa kimya iwe hiari tu.

Hadi sasa naomba kwa kufungua macho na wala sijaona tatizo lolote, haya mambo ya kuomba kwa kufunga macho yawe ni uchaguzi tu wa mtu mfano kwa wale wanaoshindwa kuweka umakini wanapoomba hasa wakiwa sehemu ambazo hazina utulivu.
 
Lengo la kufunga macho wakati wa kuomba ni kuweka umakini kwa kuongea na Mungu. Si jambo zuri watu wanaomba umekodoa macho haileti maana ya kuomba.

Wanaomba bila kufumba macho ni mashemasi tu wanaoangalia usalama asitokee wa kuharibu maombi kama mtu asiyefahamika kuingia ibadani kwa nia mbaya au yeyote aliyepagawa na mapepo.

Hata hivyo kuna madhehebu wasiofumba macho wakati wa maombi katika ibada zao
 
Lengo la kufunga macho wakati wa kuomba ni kuweka umakini kwa kuongea na Mungu. Si jambo zuri watu wanaomba umekodoa macho haileti maana ya kuomba...
Hizo ni sheria ambazo makanisa yalijitungia na wala hazipo kwenye biblia hivyo hakuna haja ya kuzilazimisha,

kuhusu umakini pia nimeshasema hapo kama mtu yupo kwenye mazingira yanayomtinga umakini akiomba kwa kufungua macho basi anaweza kufunga macho, lakini katika sehemu iliyo na utulivu hasa tunapoomba vyumbani usiku tulivu wakati wa kulala na kanisani mda wa kuomba ambao panakuwa kimya iwe hiari tu.
 
Kaka unamjua shetani, unadhani ni kadudu flani tu.

Ukifungua macho wakati unaomba anaweza akapita nzi tu ukamuona, jamaa atakuchambulia nzi mawazoni, ww utajiona unawaza
 
Haijaandikwa ila kiuhalisia tu ni kuswitch kimwili na kiroho kutoka mazingira yanayo onekana kwenda mazingira ya rohoni.

Unamwomba Mungu huku mbele yako unatizama mambo mengine
 
Mkuu umejitekenya mwenyewe na kucheka mwenyewe kwa namna ulivyoandika kwa kujiuliza na kujijibu!

Kufumba macho wakati wa sala ni kuiweka nafsi yako katika falagha, ni sawa na kushusha pazia.

Usali huku umekodoa macho wakati kanisa limejaa pomoni kamchanganyikeni na kuna wadada wenye sura za kukonyeza, kuna consentration ya kusali hapo kweli?

Maana kanisani usidhani kila mtu huingia kwa malengo yenye kufanana!

Hata kama unasalia kwako, vitu vya kukutoa kwenye reli ni vingi mno katika mazingira yako kuliko unavyidhania.
 
Haijaandikwa ila kiuhalisia tu ni kuswitch kimwili na kiroho kutoka mazingira yanayo onekana kwenda mazingira ya rohoni.

Unamwomba Mungu huku mbele yako unatizama mambo mengine
Tunasikiliza mahubiri ya kiroho kwa umakini tukiwa tumefungua macho, sembuse kuomba ?
 
Sio kila kitu kipo kwenye biblia/maandiko mkuu, kuna kujiongeza.
Muwe mnasoma hata biblia basi, kwa hii comment yako sidhani hata kama umesoma hata nusu ya maisha ya yesu, kumbuka yeye aliomba kwa kutizama juu akiwa kafungua macho tena katika matukio mawili tofauti
 
Kaka unamjua shetani, unadhani ni kadudu flani tu.

Ukifungua macho wakati unaomba anaweza akapita nzi tu ukamuona, jamaa atakuchambulia nzi mawazoni, ww utajiona unawaza
Ishara ya imani dhaifu hio
 
Concentration. Usipofunga macho linaweza kupita jimama limefungasha kisawasawa likakufanya hata usahau ulikuwa unaomba nini.
Ni ishara ya imani dhaifu kabisa uliyonayo kama imani yako kwa Mungu inaweza kutetereshwa kirahisi
 
african-american-man-praying-and-reading-the-bible.jpg

hata Yesu alivyoomba alifumbua macho huku akiangalia juu mbinguni .. YOHANA 17:1
Usiku wa juzi nikiwa nikiwa kwenye maandalizi ya kulala, kama kawida yangu huwa ni lazima nimshukuru Mwenyezi Mungu kwa afya, utimamu na amani aliyonipa. Kwa siku hio kabla ya kulala nikajiuliza swali kwanini huwa tunafumba machoo wakati runaomba? Binafsi imekuwa ni utamaduni kabisa ni lazima nifumbe macho nikiwa naomba kabla ya kulala, kabla ya kula, kuanza na kumaliza safari, n.k.

Nimefanya uchunguzi na kubaini kwamba hakuna sehemu yoyote kwenye Biblia iliyotutaka tufunge macho bali tuelekeze imani yetu kwa muumba wetu pale tunapomuomba.

Nadhani kufunga macho iwe ni pale tu ambapo mtu yupo mazingira yanayomuondoa umakini akifungua macho na ikibidi azibe pia masikio endapo kuna makelele yanayomtoa umakini, lakini katika sehemu iliyo na utulivu hasa tunapoomba vyumbani usiku tulivu wakati wa kulala na kanisani mda wa kuomba ambao panakuwa kimya iwe hiari tu.

Hadi sasa naomba kwa kufungua macho na wala sijaona tatizo lolote, haya mambo ya kuomba kwa kufunga macho yawe ni uchaguzi tu wa mtu mfano kwa wale wanaoshindwa kuweka umakini wanapoomba hasa wakiwa sehemu ambazo hazina utulivu.
Kanisani kwako lbda, hushinikizwi kufunga macho nihiari yako... mimi tukiomba nautizama msalaba.
 
Muwe mnasoma hata biblia basi, kwa hii comment yako sidhani hata kama umesoma hata nusu ya maisha ya yesu, kumbuka yeye aliomba kwa kutizama juu akiwa kafungua macho tena katika matukio mawili tofauti
Bado nnarudia kauli yangu "sio kila kitu kipo kwenye maandiko".
 
Nadhani kufunga macho iwe ni pale tu ambapo mtu yupo mazingira yanayomuondoa umakini
Ulishajijibu mkuu.
Hakuna ulazima wa kufumba macho ila waswahili wsnasema 'macho hayana pazia'. Usipofumba macho unaweza kuangalia juu ya board ukakuta kuna uchafu, badala ya kuweka mkazo kwenye maombi utaishia kuwaza kuondoa uchafu.
 
Ulishajijibu mkuu.
Hakuna ulazima wa kufumba macho ila waswahili wsnasema 'macho hayana pazia'. Usipofumba macho unaweza kuangalia juu ya board ukakuta kuna uchafu, badala ya kuweka mkazo kwenye maombi utaishia kuwaza kuondoa uchafu.
Tunaposikiliza neno takatifu vp?
Tunapoimba vipi?
Tunapobatizwa vipi?

Sembuse tunapoomba
 
Back
Top Bottom