Kwanini wanaume huchepuka?

Unakuta mkaka ana mke mzuri mwenye sifa zote za uzuri lakini hatulii kwa huyo mkewe, anachepuka na mdada mwingine tena wa kawaida tu.

Kwa nini wanaume huchepuka?
nadhani ni kwasabb wadada wenyewe hata kama wapo kwenye ndoa kumkataa mwanaume siku hizi kwao ni mwiko, wanahisi ni laana pia🐒

halafu utadhani wameambizana, ukigusa tu imo dah 🐒
 
Wanawake mnashida sana, kwanza mnataka mwanaume aiombe chumbani tena on ground, badala ya wewe kutengeneza mazingira aipate kwa Uhuru. Mfalme hatakiwi kusumbukia vitu vidogo kama hivyo.
Kingine ni mazoea, yaani kumzoea Mume kana kwamba ni mwanao
Uzoefu mdogo nilioupata nimegundua kuwa hata mkeo ndani ya nyumba bado unahitaji umwombe kama ndiyo unaanza kumtongoza Kwa upya. Hapo unampatia, ukifanya amri na ubabe unapoteza ladha na hamasa kwake
 
Kwenye ndoa kuna siri mno, wenye vifua ndio tunawaona kama wanaendelea Vema, So hii ya kuchepuka ni miongoni mwa siri zilizofichika, Nyie mnaoweka wazi, Hili nalo mkalione.
 

Watu wanakosea Sana kusema Mungu ameumba watu wawe Malaya. Uumbaji wa Mungu hauna uhusiano na dhambi unazofanya. Kwahiyo wezi nao waseme wameumbiwa Wizi 😅 ukitenda kosa usiongeze kosa lingine kwa kukufuru.
Tuje kwenye pwenti . Binadamu tuna tabia mbaya ya kutamani vitu ambavyo hatuna tukisha vizoea tunaona Cha kawaida. That's y mke wako Kuna mtu anammendea na wewe unayemmendea Ni wamwingine😆 halafu hili swala la kuchepuka lipo kwa jinsia zote sema linaonekana kwetu sisi zaidi kwasababu sisi hatuopi madhara yatakayotokea endapo utajulikana
 
Ni kweli mkuu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…