Kwanini wanaume huwa na michepuko?

Kwanini wanaume huwa na michepuko?

hapo sasa Mgirik umeuliza swali zuri sana unajua wanaume wengi wanajisahau sana wanayoyafanya wao wanayaona sawa tu ila ngoja wafanyiwe wao,patacimbika na ikibidi talaka siku hiyo hiyo ni hatari.

siungi mkono swala la nyumba ndogo hata kidogo lakini napenda sana wale wanaume ambao wana nyumba ndogo lakini wamezipa limit kwa wake zao,yaani akijua nyumba ndogo inamsumbua mke wake au inamdharau basi ataipata fresh au hiyo ndo inaweza ikawa mwisho wa mahusiano yao.
Hata kama kutoka nje ya ndoa kupo lakin huy jamaa kazd, huwez kumdhalilisha mkeo kias hcho, na itakuweje na yeye akiamua kuishi liwalo na liwe akaanza kukuletea wanaume mbele yako?? Dah! Hiii hatareee mura ayaa!
 
Last edited by a moderator:
thanks g click na hongera kwa kubaki njia kuu,lakini unawaonaje hao wenzio ambao wanawaona nyumba ndogo kuwa muhimu zaidi hadi kuthubutu kuwapiga na kuwadhalilisha wake zao mbele za nyumba ndogo zao?em funguka walau kidogo mkuu.
baki njia kuu
 
Last edited by a moderator:
okay i have taken it from you,lakini unaweza nipa proove kwa nini is innevitable?

je kuna sababu zozote za kisayansi zilizofanyiwa utafiti zikaonyesha kuwa mwanaume kamwe hawezi kuwa na mwanamke mmoja au ni kasumba tu ambayo wanaume walio wengi wamejiwekea ili tu kuhalalisha ufuksa wao?

my babu Asprin nakurespect sana lakini kwa hili em naomba uje hapa ukiwa na facts za mwanume kuwa na mwanamke mmoja ni innevitable.

halafu hapo kwenye red nina swali moja tu kwako hivi babu unawaonaje wanawake?je unawaheshimu?
Miss Blue G kwa kuzingatia namba 6 kwa thread yako hivi unafikiri kila kitu unachokipata nje unaweza kukaa chini na mkeo kumuomba naye akupatie? Uzuri nyumba ndogo zinajua fika kabisa kuwa kwa heshima ya ndoa ilivozoeleka kuna baadhi ya vitu mke hawezi mpa mumewe. Naye ndo anavitumia ili kuziba pengo la anachokimisi mwanaume.

Mchepuko is inevitable. Take it from me.
 
Last edited by a moderator:
Miss Blue G kwa kuzingatia namba 6 kwa thread yako hivi unafikiri kila kitu unachokipata nje unaweza kukaa chini na mkeo kumuomba naye akupatie? Uzuri nyumba ndogo zinajua fika kabisa kuwa kwa heshima ya ndoa ilivozoeleka kuna baadhi ya vitu mke hawezi mpa mumewe. Naye ndo anavitumia ili kuziba pengo la anachokimisi mwanaume.

Mchepuko is inevitable. Take it from me.

naongezea tu, tena hivyo vitu adimu huwa kwa kawaida haviombwi hata kwa mpenzi unayetegemea kumuoa
 
Mke ana thamani sana kuliko nyumba ndogo ndo maana akaolewa.

Kosa la baadhi ya wanawake ni kutokuukubali ukweli kuwa mwanaume hajawahi kutosheka na mwanamke mmoja. Kosa alilolifanya huyo mwanamke ni kwenda kuvamia poozeo la mmewe linalomfariji mara anapotaka faraja mbadala.

Mwanamke mwenye busara za kutosha ahangaiki kumfuatilia mmewe, kama mmewe anamtimizia mahitaji yote ya kimwili, kikojoleo, na kifamilia. Ni kujitafutia presha bure tu.

Mpe pole huyo mama, mwambie akome kumfuatilia mwanaume rijali, atakufa bure aache wanae wanateseka.

Ndio nyie nyie
 
Mke ana thamani sana kuliko nyumba ndogo ndo maana akaolewa.

Kosa la baadhi ya wanawake ni kutokuukubali ukweli kuwa mwanaume hajawahi kutosheka na mwanamke mmoja. Kosa alilolifanya huyo mwanamke ni kwenda kuvamia poozeo la mmewe linalomfariji mara anapotaka faraja mbadala.

Mwanamke mwenye busara za kutosha ahangaiki kumfuatilia mmewe, kama mmewe anamtimizia mahitaji yote ya kimwili, kikojoleo, na kifamilia. Ni kujitafutia presha bure tu.

Mpe pole huyo mama, mwambie akome kumfuatilia mwanaume rijali, atakufa bure aache wanae wanateseka.

General rule ndo hiyo hapo kwa red, ila mkuu kuna exceptions
 
Kuna watu wanachepuka mpak wanajisahau, ila kweli kwenye ndoa kuna mapungufu mengi, kinachotakiwa ni kuvumilia, au kifanya siri sana n kumheshimi mke wa ndoa. Asikudabganye mtu mtu kwenye huko wanaume wenye nyumba ndogo, nao pia huchepuka, atalalaje kila siku peke yake wewe ukirudi kwa mkeo?
MKE NA NYUMBA NDOGO NANI WA MUHIMU ZAIDI?

Nimepata swali hili kutokana na kisa hiki nilichokishuhudia:

Hivi majuzi kuna mwanamke alipewa taarifa kuwa mume wake alikuwa na kimada sehemu Fulani(almaarufu kama nyumba ndogo) mwanamke huyo aliamua kwenda kushuhudia ikiwa kinachosemwa ni cha kweli au watu tu wasioitakia mema ndoa yake pendwa,kufika huko alikuta kuwa kilichosemwa ni kweli mtupu tena hamna chumvi,kwa wivu wa mapenzi kwa mumewe (tena wanasema uchungu wa mume aujuae mke!) mwanamke Yule aliamua kuisogelea nyumba ndogo ya mumewe ili kuivagaa lakini kabla hajatimiza lengo lake tayari mume wake alishafika karibu yake kwa ajili ya kuilinda nyumba ndogo yake isipigwe na mama watoto wake watatu!!!!!!!!!!!!!!!!

Kibaya na cha kusikitisha mume huyo hakuishia tu kudhibiti mke wake bali pia kumpiga makofi kadhaa na kumzuia kwa hali na mali kutoisogelea nyumba ndogo yake,ambayo na yenyewe ilikuwa ikimjibu mwenye mali kwa jeuri zote,jambo lililopelekea mke kuondoka akiwa na uchungu mkali na maumivu ya mapenzi ndani ya moyo huku nyuma akifuatiwa na mumewe msaliti,ambaye mara baada ya kufika nyumbani alianza kumshambulia kwa maneno ya kejeli bila hata walau kuomba msamaha kwa usaliti alioufanya kwa siku hiyo,mke akaongezewa maumivu juu ya maumivu.(nadhani sote tunaelewa jinsi mapenzi yanavyoumiza na kwa hiyo tunaelewa vizuri kabisa jinsi mwanamke huyu alivyokuwa akihisi kwa wakati huo)!!!!!!!!!!!!!!!!!!!

Kisa hiki kilinipa maswali kadhaa kwa wanaume wenye nyumba ndogo:

1.Hivi ni nani bora zaidi kati ya mke wa ndoa na nyumba ndogo?

2.kama ni nyumba ndogo,umuhimu wake uko wapi kuushinda ule wa mke anayejua usiku umelalaje,umeamkaje na kukuzalia watoto kwa moyo mmoja licha ya uchungu mkali?

3.assume ndo wewe sasa unamfuma mkeo ana mwanamume mwingine na mkeo anaanza kukuponda na kumtetea Yule mwanaume mwingine,hiyo imekaaje?utajisikiaje?unahisi itakuwaje baada ya hapo? utachukua hatua gani mkifika nyumbani?

4.kama utaumia,unapomfanyia mkeo kisa kama hicho unafikiri yeye anahisi vipi?au unaamini kabisa hana hisia ila ni jiwe?au unaamini kuwa kwa wewe ni halali kabisa kumtenda hivyo ila sio yeye?

5.hivi nini unachokosa kwa mke na kukipata kwa nyumba ndogo?

6.kama kuna unachokikosa umewahi kujaribu kukaa chini na mkeo na kumweleza akupe unachokosa?

7.ikiwa ni wewe mwenyewe tu umejitune kuwa na mwanamke zaidi ya mmoja,hivi inashindikana kuonyesha heshima licha ya kuwa na nyumba ndogo?

8.ikiwa umeshindwa kuonyesha heshima na mambo yako kujulikana na mkeo kufika eneo husika ukiwa na nyumba ndogo yako,hivi unahisi kupungukiwa ikiwa utaamua kuwa upande wa mkeo walau mara moja?walau kuthibitisha yale maneno yako uliyoahidi ya kumpenda nyakati zote kwenye shida na raha siku ya ndoa yenu?


Najua wapo baadhi ya wanaume walio na nyumba ndogo na wasio nazo pia, kwa hiyo karibuni wote tuchangie mawazo yetu kuhusu hili suala kwa wale wenye nazo watupe majibu ya:

Ni nani bora wake zao majumbani au nyumba zao ndogo? na nini kinawapelekea kuwa na hizo nyumba ndogo?ikiwa nyumba ndogo ni muhimu zaidi,umuhimu zaidi wa nyumba ndogo unatokana na nini?

Na kwa wasio nazo pia nao wanakaribisha kutueleza

Wanawachukuliaje wanaume wenzao walio na nyumba ndogo na kuzithamini zadi nyumba ndogo kuliko wanavyowathamini wake zao?

Karibuni wana MMU.
 
NYIE NDO WALE WALE AMBAO TUNAWAPA SOMO HAMUELEWI SIJUI MMEMEZWA NA NIINI HUKO KWENYE NYUMBA NDOGO SIJUI MNA NINI NYIE WANAUME SIJUI TUWAFANYEJE ILI MBADILIKE KWANINI MNAKUWA HIVYO HALAFU MNASAPOTIANA KI😛hoto:😛hoto:😛hoto:
Mke ana thamani sana kuliko nyumba ndogo ndo maana akaolewa.

Kosa la baadhi ya wanawake ni kutokuukubali ukweli kuwa mwanaume hajawahi kutosheka na mwanamke mmoja. Kosa alilolifanya huyo mwanamke ni kwenda kuvamia poozeo la mmewe linalomfariji mara anapotaka faraja mbadala.

Mwanamke mwenye busara za kutosha ahangaiki kumfuatilia mmewe, kama mmewe anamtimizia mahitaji yote ya kimwili, kikojoleo, na kifamilia. Ni kujitafutia presha bure tu.

Mpe pole huyo mama, mwambie akome kumfuatilia mwanaume rijali, atakufa bure aache wanae wanateseka.
 
Namuhurumia huyo mke sijuhi alichukua uamuzi gani?
Wanaume wanatusema sisi mwalimu wetu kipofu sasa sijuhi wao mwalimu wao nani?
Back to topic
Huyo mwanaume ni mbulula kabisa huwezi kumtetea kimada wako na kumpiga mkeo hata kama kafanya kosa kukufuatilia...
Kifupi hapo upendo umekwisha
 
Na ni hulka za kimalaya kwa wanaume wengi kutotosheka na mwanamke mmoja tu
 
Price nimeshangazwa kidogo na response yako!!!but any way naomba nikuulize haya:
umeolewa?kama ndiyo,umewahi kuwa cheated na mmeo? kama ndiyo,umewahi kudhalilishwa au kupigwa na mmeo mbele ya kimada wake?

kama hujaolewa,unahisije kuona wanawake wenzio wanaoteseka sana ndani ya ndoa zao? unahisjie mwanamke mwenzio akipigwa au kudhalilishwa na mume wake? je unaumia na kujiuliza mara mbili mbili ndoa yako pia iakuwaej siku moja au unahisi wewe hayawezi kukupata?
Sijaolewa, tatizo ni kwamba habari ni ndefu sana n and huwa nahisi i am not wife material, cwez kuteseka coz of Man.
 
ni kweli Kongosho si vyema kuhukumu wanaume wote kwa scenario hiyo moja na kiukweli kabisa mimi sihukumu wanume wote ila tu kwa kisa hiki nilishangaa mno na nikapenda kujua maoni ya wanume wengine ikiwa wao pia wanaona mwenzao alivyofanya ni sawa tu?

unajua Kongosho inauma sana kufaniyiwa hivyo na mume wako?kama mume ndo kakufanyia hivyo,nani basi atakuwa upande wako?
Kongosho kuna wanaume ni machakaramu na hawawezi kuishi bila vimada lakini ukitaka mkosane au uhusiano wenu ufikie mwisho basi thubutu kiumgasi mkewe,hapo ndo utaujua ukali wake,sipendi na wala siungi mkono wanaume kuwa na nyumba ndogo but i prefer of this type aisee,mara mia hawa kuliko hao wenye ufyatu kichwani mwao!!!!!!!!!!!!!

Mahusiano ya kimapenzi sio pai, kuna mwingine atalinda nyumba ndogo, mwingine angeweza timuka, mwingine angebembeleza mkewe.

Kwa hiyo, hatuwezi hukumu wanamme wote kwa sinario hii tu. Lakini nishaona mtu pia katikisa familia sababu ya kuilinda nyumba ndogo yake. Kisa? Eti nyumba kubwa ni korofi. Hii inajustify cheating? No way, kama ni korofi basi aachane nayo.
 
Last edited by a moderator:
samahani Chebe17 sijakupata vilivyo.
Kuna watu wanachepuka mpak wanajisahau, ila kweli kwenye ndoa kuna mapungufu mengi, kinachotakiwa ni kuvumilia, au kifanya siri sana n kumheshimi mke wa ndoa. Asikudabganye mtu mtu kwenye huko wanaume wenye nyumba ndogo, nao pia huchepuka, atalalaje kila siku peke yake wewe ukirudi kwa mkeo?
 
Last edited by a moderator:
najua wanaume waiokamilika wengi wao wana michepuko ...kwa hiyo ni suala la sisi wanawake kukubali tu
 
hebu sema na wewe Rapunzel?hivi kweli unafikia hatua ya kumpiga mkeo mbele za kimada?halafu na wanawake wa siku hizi nao wana roho ngumu,mtu umekutwa na mume wa mtu lakini bado unadiriki kumjibu mke wa mwezio unavyotaka kweli ?ila siwalaumu sana wanawake hao kwa ni wao wanapewa kichwa na waume zao,laiti kama wangekuwa hawapewi vichwa labda wangekuwa wana adabu,lakini bado mwanamke anzyefanya hiyvo anaona raha gani mwanamke mwenzie kutendewa kikatili hivyo?
Namuhurumia huyo mke sijuhi alichukua uamuzi gani?
Wanaume wanatusema sisi mwalimu wetu kipofu sasa sijuhi wao mwalimu wao nani?
Back to topic
Huyo mwanaume ni mbulula kabisa huwezi kumtetea kimada wako na kumpiga mkeo hata kama kafanya kosa kukufuatilia...
Kifupi hapo upendo umekwisha
 
Last edited by a moderator:
hapana ICHANA si kirahisi tu kihivyo,unjua hata wanawake nao ni watu na wana hisia pia mbona wao wakisalitiwa wanaumia?kwa nini wewe usiumie eti kwa kuwa tu ni mwanume kamili?kwani wewe sio mwanamke kamili?

sawa basi tuseme wanawake wameamua kukubali kuwa haiwezekani mwanaume kuwa na mwanamke mmoja tu,vipi kuhusu kudhalilishwa mbele ya kimada wa mumeo?hilo pia likubaliwe na kufumbiwa macho tu?

najua wanaume waiokamilika wengi wao wana michepuko ...kwa hiyo ni suala la sisi wanawake kukubali tu
 
Last edited by a moderator:
Price hapo kwenye red pole na wala sikushangai hiyo ni hulka ya sisi waafrika wote na ndo maana wanasema ukitaka kumficha jambo mwafrika mfichie kwenye maandishi!!!!!!!!!!

kwenye blue,hakuna mwanmke ambaye ni wife materila na ambaye si wife material,ila ni mtu tu anavyojitune na kujiweka kwa kuwa wewe umejitune na kujiaminisha hvyo ndo maana unaamini kuwa wewe si wife material.

kwenye kijani hakuna anayeteseka kwa aljili ya mwanamke au mwanume,ila watu huteseka kwa ajili ya mapenzi au hisia za upendo,ila as for you kama hujawahi kuteseka kwa ajili ya upendo basi hongera sana na uombe sana yasije yakakukuta,maanake unaweza kuwa kichaa Price.
Sijaolewa, tatizo ni kwamba habari ni ndefu sana n and huwa nahisi i am not wife material, cwez kuteseka coz of Man.
 
Last edited by a moderator:
If you cannot fight them join them
if you cannot convince confuse
 
ni kweli Rapunzel ni hulka zo tu na kujiaminisha ujinga wa kuwa mwanaume hawezi kuwa na mwanamke mmoja,jambo ambalo si kweli kwani hawakuumbwa hivyo na wapo wanaume japo wachache ambao wametulia tuli na wake zo tu na wala huwezi kusikia wanachepuka,sasa sijui hao waliumbwa sayari nyingine?.
Na ni hulka za kimalaya kwa wanaume wengi kutotosheka na mwanamke mmoja tu
 
Last edited by a moderator:
Back
Top Bottom