Punguza chuki kwa walimu Kijana ,yaan tokea uambiwe uchangie kg10 za mchele umekuwa na dhihaka sana kwa walimu ,lakini kwa haraka haraka itakuwa kuna mwalimu kakugongea mke wako ,kama sio mke kamla demu wako ndio maana kila kukicha ww na walimu.
Kitu kingine usipende kukariri kuwa kila mwalimu ni maskini au ana njaa ,mipango ni matumizi Kijana ,mshahara wa mwalimu ngazi ya chini kabisa kwa sasa ni laki NNE na mshahara wa juu kabisa ni m2 na vitoto ,so walimu wana mishahara mizuri tu na sio kama mnavyojiaminisha mtaani.
Siku izi walimu wanaendesha magari mazuri ,wamejenga nyumba nzuri ,wengine wana biashara kubwa,wanasomesha watoto wao shule nzuri na vitu kama ivyo.
Kitu kingine ambacho hujui ni kwamba kila mtumishi wa umma anakopa sana tu ni vile walimu ni wengi sana kwa idadi basi wanaonekana wao ndio wakopaji sana ila nakwambia tena hakuna mtumishi asiekopa ,wabunge wenyew wamejaa madeni sembuse mwalimu kukopa.
Pia elewa saiz hakuna mwalimu mzembe wa kutapeliwa saiz walimu ni wasomi tofaut na zamani .
Kuna MTU kadai walimu Mara nyingi wanakuwa wamefeli masomo yao ,narudia tena acheni kukariri saiz walimu ni wasomi grade 1-3 ,walimu kibao wana division one na two za kumwaga tu na vyuo vikuu, diploma ,certificate wametoka na GPA kubwa ,,so elewa kizazi hiki hakuna ualimu wa hisani unausotea.
Mwisho kabisa punguza hasira kwa walimu najua kuna sehem wamekugusa moja kwa moja ndio maana kila cku unawapondea tu,aliekuzid kakuzid tu ,we endelea kukomaa na mpunga huko majurubani ipo cku nawe utatoboa maana Nina uhakika una maisha ya shida sana ,ungekuwa na maisha mazuri sidhan kama ungekuwa na roho ya namna hiyo kwa walimu waliokufanya ujue hata kuandika hapa jf.