Mkuu maelezo yako yamenipa nguvu sana Na Ninajiona naweza kusonga mbele
ila mkuu mbali na TRA nasikia pale bandari kuna mzunguko wa malipo mengi , Ni kweli?
Kununua online kutoka kwa supplier yeyote duniani inahitaji uangalifu na kila mnunuaji ni lazima achukue tahari yeye mwenyewe mapema kabla ya kuingia mzima mzima.Alibaba imeorodheshwa ktk soko la hisa la Hongzkong ktk bara la asia ndiye mshindani mkubwa wa ebay na amazon na sasa wapo ktk IPO ya soko la hisa New York. Km pangekuwa na kashfa yeyote kubwa wasingaliruhusiwa kuwa Public Company nchini America kwani utapeli wowote utachafua soko la hisa na kuleta nyufa ktk barabara ya uchumi. Tuwe na amani na tuchukue tahadhari mapema
Kama unataka business na Huna pesa ya mtaji mwingi ingieni Alibaba tafuta small business partners .
ofcourse..ila cost zako zote we unapigiwa na TRA ambao wanakuwa na ofisi zao kila posta ilipo
huo upuuzi usioutaka humu... we kama nani :majani7:? hakuna biashara inayoendelea bila ujanja ujanja...kabla ya kuanza kushusha hizo bei TRA washanipiga sana...nikaona inatosha
endelea kulipa kodi kadiri uwezavyo mzee
ahsante Mkuu
unazungumzia posta
je kwa mzigo unaochukua nafasi kubwa kama magodoro n.k
inawezekana nisichukulie kabisa bandarini?
Alafu nasikia huwezi toa mzigo mpaka upitie kwa clearing agent, ni kweli mkuu?
Pia Mfano vitendea kazi vya usafi maofisin na majumban, makato ya kodi yakoje?
Ahsante sana mkuu
Mkuu hizi mamlaka husika na serikali ndio wanawafanya Watanzania watafute mbinu za kukwepa kodi na waichukie kodi!mfano TRA wao kodi uwa wanakadiria tu,mimi niliwahi leta mzigo wa $520 walivyo wehu wakakadiria kwa $950 nilibishana nao na nilipoteza siku nane na nika incur cost ambazo sio necessary mwisho wa siku ndio yakaja kukubaliana na gharama ile halisi,ukija kwa Serikali,wao usiku na mchana ni kuwahimiza watu walipe kodi,na kuwapandishia kodi kila budget,lakini mwisho wa siku nchi nchi inaendeshwa kwa misaada inayotugharimu Watanzania,na hata budget kuu ukiangalia,karibu nusu ya budget inaenda kwenye matumizi yao ya kawaida(yasio na tija) na nyingine ndio upelekwa kwenye mambo ya maendeleo,sasa kwa mwendo huu kweli kuna Mtanzania atakaependa kulipa kodi wakati anajua wanao nufaika kwa kiasi kikubwa ni wao wachache?
e-comerce ni moja kati ya maeneo sugu yanayoongoza kwa wizi na utapeli wa hali ya juu kabisa duniani kwa sasa...hivyo pamoja na huduma nzuri na za haraka zinazopatikana huko, mtumiaji bado unashauriwa kuwa makini....naomba nitoe mbinu nanayoitumia mimi kununua bidhaa huko....mimi ni mwanachama wa benki mbili tu hapa Tz, (nbc na crdb)...huku nbc ndiko kibubu changu kilipo hivyo nikiagiza mzigo natoa pesa nbc naingiza kwenye simu yangu (huduma za fedha kwenye mitandao ya simu) mfano laki na nusu kisha naituma crdb na wakati huo huo kitu ninachotaka kukinunua hakizidi hiyo pesa labda tuseme laki na thelasini...kisha nanunua kwa kutumia e-purchase.....niliamua kutumia mbinu hiyo ili nisiibiwe kiasi changu cha pesa kinachobaki kwenye account.
Sijawahi kuagiza bulky items kama magodoro...its easy unaweza kwenda ukaulizia info posta kwenye kitengo cha parcel wakupe procedures ikiwa unachukulia bandalini watakwambia
nimeagiza vitu vingi ila mostly ilikuwa ni elecronics devices ambazo hazichukui space kubwa...tumeagiza incubator ya mayai 200 ambayo ni silingi laki na 30 ukiulizia madukani huku ya mayai 80 tu ni laki 2 na nusu mpaka laki 3
so mzigo kama huo unaotaka kuagiza fanya inquiries ya information posta uwasikie watakwambia nini...
Sijawahi kuagiza bulky items kama magodoro...its easy unaweza kwenda ukaulizia info posta kwenye kitengo cha parcel wakupe procedures ikiwa unachukulia bandalini watakwambia
nimeagiza vitu vingi ila mostly ilikuwa ni elecronics devices ambazo hazichukui space kubwa...tumeagiza incubator ya mayai 200 ambayo ni silingi laki na 30 ukiulizia madukani huku ya mayai 80 tu ni laki 2 na nusu mpaka laki 3
so mzigo kama huo unaotaka kuagiza fanya inquiries ya information posta uwasikie watakwambia nini...
Mkuu hizo incubator hiyo price ime include shipping na gharama za kodi hapa nchini au?je hizo incubator ni automatic au?natanguliza shukrani mkuu
including gharama...ingia Ali express au alibaba utaziona kibao...tumechukua mbili majuzi tu tumezipokea...ila ukitaka agizia Hongkong post au singapore post ...china post mizigo inachelewa sana...kuna jam ya mizigo kutokea china post
including gharama...ingia Ali express au alibaba utaziona kibao...tumechukua mbili majuzi tu tumezipokea...ila ukitaka agizia Hongkong post au singapore post ...china post mizigo inachelewa sana...kuna jam ya mizigo kutokea china post
Ahsante mkuu,mizigo inakuja na ndege au meli?naomba nipatie link ya huyo seller kama hautojali!na ushuru hapa nchini wana calculate vipi?
mkuu izo icubator umezichukulia bandarin au posta
mimechukulia posta mwanza...zinakuja na ndege, unajua ukiagiza china bei inakuwa chee kwani pamoja na kununua kwa bei hiyo bado unaweza kuongea nae akashusha value ya invoice so tulilipa pesa kidogo kama kodi