Kwanini Watanzania hawapendi kusafiri?

Kwanini Watanzania hawapendi kusafiri?

Wasomali vipi? Hawana njaa?
Mkuu, labda niseme miongoni mwa mambo yanayomchochea mtu kusafiri ni pamoja na:
1. Shida
Hapo utakuta watu wanaotafuta ajira na makazi, mfano raia wa Somalia, Ethiopia, Libya, Sudan, n.k.

2. Mafanikio.
Hapo, watu wanaosafiri si kwa sababu ya hali ngumu, bali kipato kinawaruhusu.

Sababu za safari zinaweza kuwa masomo, utalii, biashara, n.k.
Nchi zinazoongoza duniani kwa raia wake kusafiri ni hizi hapa
1. Finland
2. USA
3. Sweden
4. Denmark
5. Norway
6. Hong Kong
7. New Zealand
8. Canada
9. Australia
10. France

😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃😃
Wazungu wamejipendelea? Mbona hakuna hata nchi moja ya Afrika?
 
Passport mkuu ni Shida,..kuipata hadi uende Kwa Sangoma.

BEB0A301-082C-4410-AD22-1DF3FD01278A.jpeg
 
Iko hivi ukiangalia wazungu wengi ni watu ambao wanafanya sana saving hata wenye vipato vya kawaida.

Wanaweza saving kwakuwa kwanza kiwango cha utegemezi kwao ni kidogo sana. Yani utakuta baba na mama wana mtoto mmoja au hawana na hamna mtu anaewaomba hela.

Hakuna sijui michango ya ukoo, sijui mtoto wa mjomba ada shule, mara rafiki anaoa, mara bibi anaumwa n.k

Birth control imesaidia wenzetu sana. Sisi huku mtu ana ndugu zaidi ya laki na akipata tu ka ajira ka kulipwa laki saba basi kila mtu anamtolea macho, vizinga visivyoisha.

Huyo mtu ata save sangapi ili aweze kutembelea nchi mbalimbali?

Kingine kwa wenzetu wa nje huko wengi wanakula generational wealth. Yani mtu anazaliwa anakuta familia iko well-off kuanzia vizazi kadhaa vilivyopita. So yeye anaendeleza kutengeneza hela tu na future ya kizazi chake so mambo kama kusafiri ni kawaida tu.

Chamwisho ni nchi yetu hii ina mifumo ya ajabu sana. Mtu kumiliki passport tu inaonekana kama vile ni jambo la ajabu sana. Ukienda uhamiaji kutaka passport inakuwa ni mchakato mgumu utadhani unataka kwenda mbinguni.

Nchi za wenzetu kuwa na passport ni kawaida na kila raia anayo kama document muhimu. Hapa kwetu passport inachukuliwa tofauti sijui kwanini CCM hawataki raia wamiliki passport?
Hakuna nchi ina gawa hati ya kusafiria kama njugu, utaratibu ufatwe

6FB84EC4-CFD3-4297-8F73-BD76FBD752E0.jpeg
 
Tupo comfortable nyumbani, Tuzurure tupate nini?
Inaonekana una kazi nzuri, mahali pazuri pa kuishi na kila kitu ni uhakika.

Wengine ramani hazisomi na hawana matumaini wanajaribu kutafuta maisha kwingineko duniani. Na sio jambo baya, dunia ni yetu na tumeamrishwa tuizunguke tuone maajabu na uumbaji wa mungu wetu muumba.

Kama umefunguliwa na umejaaliwa na mungu wako mshkuru sana!
 
Ila watanzania wako sehemu kubwa dunia kuna nchi unaweza kwenda utashanga unakutana na mbongo

Ova
 
Kusafiri ni anasa kwa mwananchi ambaye hajui kesho asubuhi atakula nini huku anadaiwa kodi ya nyumba, kurejesha kikoba, ada za watoto na gharama za matibabu ya shangazi aliyemeza panga
Hapo sasa.
 
Inaonekana una kazi nzuri, mahali pazuri pa kuishi na kila kitu ni uhakika.

Wengine ramani hazisomi na hawana matumaini wanajaribu kutafuta maisha kwingineko duniani. Na sio jambo baya, dunia ni yetu na tumeamrishwa tuizunguke tuone maajabu na uumbaji wa mungu wetu muumba.

Kama umefunguliwa na umejaaliwa na mungu wako mshkuru sana!
Hayo umesema wewe, ila mie nimekupa sababu why watanzania hatoki nje.
Japo nimeisema katika mtindo wa masihara.
Ila ni kuwa watanzania wapo comfortable na Nchi yao ukilinganisha na mataifa mengine.
Pia ukiwa mtanzania huwezi kupata ata ile hadhi ya Ukimbizi sababu kuna Amani.
 
USHAMBA

Hata watu wenye pesa hapa Tanzania wengi hawapendi Adventure au kupata Exposure hata ya kujua tamaduni za watu tofauti tofauti

Wanachojua wakishatajirika basi ni kununua magari na nyumba kisha kula pombe na Wanaaake kila siku
 
USHAMBA

Hata watu wenye pesa hapa Tanzania wengi hawapendi Adventure au kupata Exposure hata ya kujua tamaduni za watu tofauti tofauti

Wanachojua wakishatajirika basi ni kununua magari na nyumba kisha kula pombe na Wanaaake kila siku
Umenikumbusha habari niliyoisikia hivi karibuni!

Kwamba kule Arusha maeneo ya Loliondo, kuna Mmasai alimkopesha mfanyabiashara mwenye sheli za mafuta shilingi milioni mia mbili. Halafu mtu mwenyewe alikuwa akiishi kwenye nyumba ya nyasi.

Hata alipojenga nyumba ya kisasa baada ya kushawishiwa na marafiki zake, alirudi kwenye nyumba yake ya nyasi baada ya siku chache kwa madai kuwa nyumba ya bati siyo nzuri.

Sasa huyo mwenye uwezo wa kukopesha milioni mia mbili kwa mkupuo angeshindwa kutembelea alau nchi moja kwa mwaka?

Ni kweli kuwa ushamba ni sababu mojawapo.
 
Back
Top Bottom