Kwanini Watanzania lazima tuweke magrill kwenye madirisha?

Kwanini Watanzania lazima tuweke magrill kwenye madirisha?

Mleta mada,
Nadhani Nyumba nyingi Zinakuwa hivi kwa sababu watanzania tunaigana Sana, ukienda Kanda ya ziwa Nyumba zote paa kubwa mno

Kuna haja ya kuwapa kipaumbele Architects, tatizo serikali nayo imelala, wanapokea ada tu bila kuweka kipaumbele kwenye taaluma hii
Unadhani kanda ya ziwa wanaigana kuweka paa kubwa? Fuatilia vizuri sababu
 
Mimi mwenyewe huwa siyapendi. Hapa nchini kwetu inategemea na eneo ulipojenga nyumba yako. Isingekuwa sbb za kiusalama ningeweka nyumba yangu hapa uone ina vyumba viwili vya kulala ila nimeweka full windows floor to ceiling zenye ukubwa wa 2.4 m urefu kwa 2 m upana na sijaweka grill. Huwa watu wengi sana wakija kwangu hupata mshangao wa jinsi madirisha yalivyo makubwa na hayana grill.
Basi weka hata ya kwenye gugo kuyaone, au wewe ndio wa kwanza kuweka madirisha ya hivyo?
 
Je, ni kwanini watanzania wengi lazima tuweke magrill kwenye nyumba zetu mbona marekani ujambazi ni mwingi kuliko kwetu lakini hawawekagi magrill kwenye madirisha?

Je, unaweza kuishi kwenye nyumba isiyo na magrill?
Umeona ni Tanzania pekee? Nakushauri fanya utafiti upya!
 
Back
Top Bottom