#COVID19 Kwanini Watanzania wengi wanakataa chanjo ya Corona?

Huko mtaani umeuliza watu wangapi..usi generalize kwa kusema kila mtu!
Bro usipime sisi tunaoishi huku Mtaani tunajua

Kama huamini panda bodaboda anzisha hio Maada harafu Msikilize anasema nini
 
Watanzania wenye biashara za kuvuka mipaka watachanja chanjo. Vivyo hivyo kwa wengine wote wenye issues za kusafiri nje ya TZ pia watachanja chanjo fasta.

Sisi wa huku kajamba nani chanjo kwetu ni anasa.
 
Utasikia mtu anakuja na hoja dhaifu kabisa kuwa eti chanjo ina lenga kutumaliza waafrika wakati karibu 80% ya dawa zilixopo mahospitalini mwetu zinatoka huko, hao wazungu wakitaka kufanya hivyo si watafanya tu hata kwenye ARVs!!? Watu wamekuwa brainwashed sana na jiwe kuu la pembeni.
 
Kweli kabisa Mkuu na huu ndio upumbavu na ujinga unaoendele kutumaliza na kututesa ,na sababu kuu kutojua
 
 

Attachments

  • VID-20210521-WA0040.mp4
    8.4 MB
Yaani hawajui hata wanacholaumu.

Unalaumu wazungu kuhusu CORONA wakati Corona imeanzia China?

Huziamini chanjo: Je, huziamini chanjo zipi: Astra Zeneca, Moderna, Pfizer au Sinovac ya Mchina ?
 
Kuna watu wamekunywa maji leo hii na wamekufa.

Usishangae watu kufa kwa blood clotting walipopatiwa chanjo.
 
Walikaririshwa, wakakariri sasa wanakiimba wasichokijua...
Wengi kwa sababu ya "...ulofa na..." hawatambui wanataka nini na wanadhani Tanzania ni kubwa kuliko dunia...
serikali ndio wakati wake kuchukua Maamzi ya kitalaamu bila kujali na uzuri zaidi Mama yuko na Mawazo chanya
 
Hao wengi mnawahesabia Lumu

Ni uelewa Mkuu
 
Siyo Wa-TZ wengi wanaopinga. Ni wale waliolishwa "tango poli" na mwendazake. Mu-Tz mwelevu hawezi kupinga chanjo.
 
Shida iko wapi? Chanjo iletwe anayetaka atumie asiyetaka aache. Tusiwanyime watu fursa ya Kinga kwa hofu zetu
SAWA WALETE WASIJE WAKALETA MZIGO UTAKO EXPIRE PASIPO KUTUMIKA, NI HASARA KWA TAIFA
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…