Kwanini wengi wanapenda kujifanya TISS wakati kazi hii ni kada ya ulinzi kundi moja na mgambo?

wangekuwa USU wasingepewa jukumu la kuwalinda viongozi waandamizi...

kitengo cha jwtz unacho kihusisha na TISS kinaitwa IO....ama INTELLIGENCE OFFICER...na hii ilitokana na kipindi kile jeshi lilivyo asi Polisi walianza kunusa hatari ya Uasi wa JESHI wakauzima hapo ndipo chuki kati ya jwtz na Polisi ilipo zaliwa baada ya Uasi huo kumalizwa waliunda kikosi cha INTELLIGENCE OFFICER ili Polisi wasije wakaingia kuchunguza JWTZ maana ingeleta kisasi na ingesababisha wachapane RISASI🤣🤣🤣

INTELLIGENCE OFFICER awa kazi yao ni kuratibu na kunusa tabia za hatari ndani ya Jeshi...ni kama MP tu....MP ni MILITARY POLICE ambao kazi yao ni kutuliza nidhamu ndani ya Jeshi na MP wana mafunzo ya ziada kama ya Polisi.

IO wana mafunzo ya ziada kama ya TISS lakini taaruma hiyo ni kwaajili ya nidhamu ya Ndani ya Jeshi na sio NJE ya jeshi...

kitu cha msingi ambacho pengine wengi atukielewi ni kuwa majeshi yote tuliyo nayo yanafanya kazi kama Cheni ya baiskeli kwa kifupi yanategemeana...! ndio maana hata kule HANANG kulipo tokea mafuriko majeshi yote yamehamia huko...awajawaachia ZIMAMOTO ambao ndio wenye jukumu la uokoaji...

na kwa historia ya majeshi hapa nchini majeshi yote yamezaliwa ndani ya jeshi la Polisi,🤣🤣🤣

ila baadae lilipo undwa Jeshi la Wananchi Mkuu wa majeshi ikaamliwa atoke ndani ya JESHI la Wananchi ndio maana vazi la jeshi ukilichunguza vizuri lina Rangi za majeshi yote tuliyo nayo...

TISS kazi yao ni kunusa Hatari ndani na nje ya mipaka yetu...baada ya TISS kuwa na Taarifa zisizo na mashaka taarifa za uhakika. mfano tishio la ugaidi taarifa hiyo Tiss wataipeleka kama ilivyo ndani ya jeshi la polisi kisha polisi watashughurika nayo ikiwemo kuwatia mbaro washukiwa wa ugaidi na kuwafikisha mahakamani kama itawezekana ikishindikana watawalaza Chini...😭😭😭

TISS wakipata hatari nje ya mipaka yetu kuwa kuna nchi inajaribu kuleta fyoko fyoko... wataipeleka hiyo taarifa ndani ya Jwtz kisha JWTZ watafanya kazi yao...

kwa hiyo majesho yote yana shirikiana ila TISS tu ndio wenye uwezo wa kufanya kazi kwenye majeshi yote na sekta zote hapa nchini.​
 
Mkuu umeandika maelezo msrefu ambayo hayaeleweki kama unakubaliana na uliyemquote ama laa.

Jamaa kakupa uhalisia kwamba majeshi yetu haya yana vitengo vya inteljinsi ndani yake,intelijensi hao hufanya kazi kama za usalama ambao ni undercover.

Ukienda jeshini wapo hao intelijensi officer ambao ni undercover.

Ukienda polisi wapo hao intelijensi officers ambao ni undercover achana na hawa askari kanzu kuna intelijensi ofisaz ambao hatuwezi kuwajua wengune wapo mpaka vyama vya upinzani huko 😀😀,Hii nchi hii ina ulinzi wa kutosha sana.

ndio hata idara ya usalama yenyewe inao hao intelijinsi ambao uni undercover,sio hawa ambao hutembea kwenye misafara na raisi hapana,wapo ambao hawatakiwi kujulikana.

So anachokuelezea mdau hapo juu ni sahihi ila hatuoni maelezo ya kukubali au kukataa bado warukaruka 😁😁😁
 
Nchi hii Sasa hivi imekufa kila Kona.

Wenye akili hawaheshimiwi.

Machawa ndio wanafanya maamuzi chini mpaka juu

Wenye akili wameamua kukaa kimya tu.
Neno la Mungu lilikwishasema haya katika kitabu cha Mhubiri 10:5-7

Liko baa nililoliona chini ya jua, nalo ni kama kosa litokalo kwake yeye atawalaye; ya kuwa upumbavu huwekwa mahali pa juu sana, nao wakwasi hukaa mahali pa chini. Mimi nimeona watumwa wamepanda farasi, na wakuu wakienda kwa miguu juu ya nchi kama watumwa.
 
umesoma na kuelewa nilicho kiandika kweli...?
 
Bongo kila mtu ni TISS hadi vichaa mtaani. TISS ni pango la walanguzi
 
😅

Miaka ile polisi walikuwa wanaogopwa sana basi walikuwa na kile kiswahili chao ili aonekane polisi ,utasikia "Aroo wee ,hili lijamaa linajifanya jeurii"

Basi mtu akiongea hicho kiswahili watu wanamuogopa wanajua ni polisi.
hizo rahaja zilitokana na idadi kubwa ya wakurya katika vyombo hivyo.

ingekuwa rahisi sana ukutane na polisi mkurya kila kitengo,kutokana na maumbo yao na haiba yao ya hasira kupindukia.
 
Nimekwelewa. Tatizo ni superiority complex.
TISS mwenye akili kamili hawezi kujimwambafai hata kidogo.

Sasa unakuta mshenzi mmoja anataka anywe pombe za bure na apate wanawake wa bure wakati pesa hana mfukoni hapo ndipo utamjua ni tiss
 
kabisa,askari wa jwtz analipwa zaidi ya mtumishi wa tiss.

tiss wanabebwa na safari zilizoko ofisi ya rais.
 
Ukweli uliona uchungu ndani yake..Iko hivo kwa wengi sana.
 
Nimekwelewa. Tatizo ni superiority complex.
TISS mwenye akili kamili hawezi kujimwambafai hata kidogo.

Sasa unakuta mshenzi mmoja anataka anywe pombe za bure na apate wanawake wa bure wakati pesa hana mfukoni hapo ndipo utamjua ni tiss
hawa tiss ambao hata hutambulika ni wale PSU makumbusho,kwao hata akiunguruma bar wala sio issue kabisa,na sio sehemu ya miiko yao kutambulika ndio maana wanakaa kwenye mageti ya viongozi au nyuma yao.

wana vitengo vingi,ila kile undercover ndio mnaweza mkamuua asiseme yeye ni nani,labda awe chini ya mikono salama kama polisi,au jeshini nk.
 
hizo rahaja zilitokana na idadi kubwa ya wakurya katika vyombo hivyo.

ingekuwa rahisi sana ukutane na polisi mkurya kila kitengo,kutokana na maumbo yao na haiba yao ya hasira kupindukia.
Kumbe ndio maana wanaiga 😅
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…