Kwanini wengi wanapenda kujifanya TISS wakati kazi hii ni kada ya ulinzi kundi moja na mgambo?

Nilikuwa sifahamu kumbe wale majamaa wanaolinda viongozi wote wanafahamika kwa majina na sura, na sheria zao haijali wao kufahamika kwa umma
 
Usalama wa Taifa ni kazi ya kila mmoja wetu, kila mmoja anawajibika kwa usalama wa Taifa letu. Tofauti ni kuwa kuna waliojariwa na wana mafunzo Fulani, wewe fanya kwa lile unaloliweza, Ni kama usafi tu, wapo walioajiriwa kufanya usafi lakini kwa ujumla wake ni jukumu letu sote.
 
Hawana lolote wa kawaida sana tunawajua na tunayaona maisha yao mtaani
 
Dah jamaa anataka kufananisha walinzi wa nchi TISS na Hawa jamaa wanaopola ubwabwa wa mama ntilie na kwenda kuula wao 🀣🀣🀣🀣
 
All in all status wanayo
 
We vaa tu sutiKaunda nyoa kipara nenda kaunta kunywa WINDOKU ukiwa umesimama kaunta...macho yako yanaangaza angaaza kila kona
Utaona Wabongo wananong'onezana wengine hata kukimbia kaunta.....

MAUJIKO ..teh teh teh....yani kutisha tu watu
Shemeji yangu aliolewa na bro akidhani jamaa ni afisa usalama kumbe jobless hana kitu. Yaani kuja kushtuka tayari harusi tumekula na ana watoto mapacha. Ikabidi tu shem akubaliane na ukweli kuhusu mumewe. Bro ana mwili mkubwa na alikuwa na hizo pigo za kuvaa kaunda suti
 
Hahaha....
 
yule aliyemtishia nape yupo kule kwa dangote anasubiri kitanzi.. kumbe lilikuwa ni lijambazi!!
 
Deep down kuna kitu kinakusumbua kuhusiana na hii kada. Tafakari utajua ni nini.
Kinachonisumbua ni kuona kwamba yale wanayojihusisha nayo siyo yale ambayo ni matarajio ya wananchi wengi wa nchi ya kulinda usalama wao. Badala ya ku-deal na watu ambao kwa hakika ni hatari kwa usalama na ustawi wa nvhi na wananchi wake, wao wanahangaika ktk kuwashughulikua watu ambao ni raia wema ktk jamii. Mifano hai ipo mingi sana kuhusiana na hoja hii, naamini hata wewe binafsi baadhi yake utakuwa unaifahamu. "Injustice somewhere is the threat to justice everywhere "( by Martin Luther King Jr).
Aidha, uovu haukubaliki mahali popote pale, aidha iwe duniani au mbinguni. Uovu unakubalika na wale wenyewe watenda maovu tu lakini siyo kwa mtu mwingine yoyote yule ambaye ni raia mwema.
Hivi unataka kuniambia watu ambao wamekuwa wakijihusisha na matendo kama haya ya huyu kwenye video hapa chini ndio "wana status nzuri" ktk jamii?? Seriously??
Jaribu kutafakari kidogo tu kwamba, matendo mabaya kama haya ameweza kuyatenda hadharani kabisa mbele ya umati wa watu, Je, hayo matendo ambayo wamekuwa wakiyatenda mafichoni tena kwa Siri kubwa ni mabaya kiasi gani???????
Je, hivi ni kweli kwamba sisi Watanzania tunahitaji taasisi ya Usalama wa taifa inayofanya kazi kwa mtindo wa namna hii??Kweli??

Kuna msemo mtaani kwamba, "Chura anapenda maji, lakini siyo maji ya Moto."
 

Attachments

  • 5117362-148efa178040dfcd6b51b581965e1bf3.mp4
    25.4 MB
Duh

Ova
 
Usalama wa taifa ni Askari wa intelijensia, idara chini ya ofisi ya Rais.

Lakini Askari kanzu ni Polisi wa upelelezi asiyevaa Uniform.
Nilipokuwa mdogo nilikuwa najua Askari kanzu ni Polisi ila huwa anavaa Kanzu πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜†πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ€£πŸ€£πŸ€£πŸš¬πŸš¬πŸš¬πŸƒπŸΎβ€β™‚οΈπŸƒπŸΎβ€β™‚οΈπŸƒπŸΎβ€β™‚οΈ
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…