Kwanini Yesu Kristo hakuoa, hakuwa na mwanafunzi wa kike, pia Yesu hakuwa na ukaribu wala urafiki na wanawake? Kuna nini nyuma ya pazia ?

Kwanini Yesu Kristo hakuoa, hakuwa na mwanafunzi wa kike, pia Yesu hakuwa na ukaribu wala urafiki na wanawake? Kuna nini nyuma ya pazia ?

Chunguza kwa makini, Mary Mardalena alikuwa na uhusiano gani na Yesu. Kwa kuwa Yesu alikuwa Mungu na binadamu, alitumia ubinadamu katika uhusiano wake na huyo mwanamke. Ila kuhusu mitume, hakutaka kuchukuwa wanawake kwa sababu zake mwenyewe. Alitumia ubinadamu katika kuwabagua wanawake.
 
Shalom,

Habari kwenu nyote wadau wa jukwaa hili, nimekuwa nikijiuliza sana haya maswali kwanini Yesu hakuoa, Kwanini Yesu hakuwa na mwanafunzi wa kike, kwanini Yesu pia hakuwa na ukaribu wala urafiki na wanawake?

Hili fumbo linatupatia Mtihani gani ?
Tusaidiane kufikiria, karibu kwa rejea nyingi na majibu.

Wadiz
Jiulize na hili, yesu alikufa kwa, siku tatu, na tunaambiwa Yesu ni Mungu, swali kwa siku alizokuwa amekufa, na ni alikuwa Mungu wa dunia/ulimwengu? Au, dunia kwa muda huo ilikosa Mungu!
 
Jiulize na hili, yesu alikufa kwa, siku tatu, na tunaambiwa Yesu ni Mungu, swali kwa siku alizokuwa amekufa, na ni alikuwa Mungu wa dunia/ulimwengu? Au, dunia kwa muda huo ilikosa Mungu!
Mbona nyie washamba Yesu alifunga na kuomba kamamwanadamu! Mambo mengine mnayaongeza wenyewe.
 
Yesu ndie Mungu kwa roho ukristo unamtambua Yesu kristo aliehai hakuna mwingine..ukiwa katika kundi la wachawi ukipiga maombi pasipo kulitaja jina la uyu mwamba utafeli,ila ukitamka tu kwa jiiiiina la yeeesuuuu!!!majini,vibwengo,shetani mwenyewe na vikalagosi vyake wanakimbia
 
Umenena kweli biblia imekataza mwanamke kuwa kiongozi wala kusimama mbele ya wanaume kuwafundisha,lakini

Watu wamepotoka kweli kweli,siku hizi hadi kuna manabii wanawake,yupo mmoja clouds jumapili,yupo serious kabisa na anachokifanya!!! Inashangaza Sana!
kuna andiko linakataza wanawake kuwa viongozi au manabii?
 
kwa mafundisho yap?
Gospel of Philips 1:32..
Screenshot_20240527_152516_Adobe Acrobat.jpg
 
Shalom,

Habari kwenu nyote wadau wa jukwaa hili, nimekuwa nikijiuliza sana haya maswali kwanini Yesu hakuoa, Kwanini Yesu hakuwa na mwanafunzi wa kike, kwanini Yesu pia hakuwa na ukaribu wala urafiki na wanawake?

Hili fumbo linatupatia Mtihani gani ?
Tusaidiane kufikiria, karibu kwa rejea nyingi na majibu.

Wadiz
Katika Biblia kuoa au kuolewa sio lazima, kuhusu wanafunzi wa kike yesu alikuwa nao wengi sana labda useme mitume, lakin kwa kuzingatia jamii aliyoish nayo isingekuwa rahisi kuwa na waandaman wa jinsia tofauti, ila marafiki wa kike alikuwa nao mfano Martha na Maria wale dada zake Lazaro
 
Wanawake ni matapeli mkuu simple tu, ukitaka kuishi kwa amani kaa mbali nao unless ukubali kuwa fala
 
Unatak awe krbu na mashetan
"Ikimbien zinaa kwa gharama yoyote
 
Jiulize na hili, yesu alikufa kwa, siku tatu, na tunaambiwa Yesu ni Mungu, swali kwa siku alizokuwa amekufa, na ni alikuwa Mungu wa dunia/ulimwengu? Au, dunia kwa muda huo ilikosa Mungu!
Yesu alikuwepo kabla ya kuumbwa ulimwengu.

Yesu alikuja duniani kwa kutumia mwili wa binadamu kupitia Mariamu.

Yesu hafi, ni ule mwili aliokuja nao ndio uliteswa, ulikufa na ukafufuka na kupaa Mbingu.
Sisi Wakristo tunamwangalia Yesu kiujumla wake na sio yule mtoto wa Mariamu.


Isaya 9:6
Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
Tumepewa mtoto mwanamume;
Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;
Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa ajabu,
Mungu mwenye nguvu,
Baba wa milele,
Mfalme wa amani.

Isaya 7:14
Kwa hiyo Bwana mwenyewe atawapa ishara.
Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli.

Mathayo 1: 23
Tazama, bikira atachukua mimba, Naye atazaa mwana; Nao watamwita jina lake Imanueli; Yaani, (maana yake ni) Mungu pamoja nasi.

Yohana 10:17 Ndiposa Baba anipenda, kwa sababu nautoa uhai wangu ili niutwae tena.
18 Hakuna mtu aniondoleaye, bali mimi nautoa mwenyewe. Nami ninao uweza wa kuutoa, ninao na uweza wa kuutwaa tena. Agizo hilo nalilipokea kwa Baba yangu.

Yaa ladhiina amanu.
Hakuna Binadamu anayeweza kumwua Yesu.
Yesu mwenye uweza wa kuzifufua maiti za binadamu.
Pale alikuwa hafufui bali alikuwa anaumba upya kama alivyo muumba Adam . (maiti imeoza siku nne anaiumba upya na kuipa uhai)

Yesu alikuja dunia katika umbo la mwili. Kama alivyomtembelea Nabii Ibrahimu katika kitabu cha Mwanzo 18:1....

Mwanzo 18:1
Bwana akamtokea Ibrahimu karibu na mialoni ya Mamre, alipokuwa ameketi mlangoni pa hema yake mchana wakati wa hari.

2 Akainua macho yake akaona, na tazama, watu watatu wamesimama mbele yake. Naye alipowaona alipiga mbio kuwalaki kutoka mlangoni pa hema, akainama mpaka nchi,

3 akasema, Bwana wangu, kama nimeona fadhili machoni pako nakuomba usinipite sasa mimi mtumwa wako.

Yohana (Joh) 8:56 Ibrahimu, baba yenu, alishangilia kwa vile atakavyoiona siku yangu; naye akaiona, akafurahi.

Yohana 8:57
Basi Wayahudi wakamwambia, Wewe hujapata bado miaka hamsini, nawe umemwona Ibrahimu?

Yohana (Joh) 8:58
Yesu akawaambia, Amin, amin, nawaambia, Yeye Ibrahimu asijakuwako, mimi niko.

Kwa akili yenu Amanu, hapo mtauliza.
Hivi alipo mtembelea Nabii Iburahimu kule Mbinguni alimwacha nani ?
Inamaana sisi wa huku Mbagala Mungu hakuwepo huku kwetu ?
Mungu tunayemjua ni Omnipresence, yupo kote wakati wote.

Mbona hamu ulizi, Mungu alipomtokea Nabii Musa kwenye Bonde la Tua akiwa kama kijinga cha moto unaowaka, kama Qurani inavyosema, kule Mbinguni alimwacha nani ?
Mungu yupo pote na muda wote, zile zilizowatokea Musa na Ibrahimu ni dalili tu au ishara, na sio kwamba Mungu yote yupo pale mahali.
Binadamu hawezi kuishi kama atatokewa na utukufu wa Mungu, atakufa, hata jua litakufa na dunia kuyeyuka kabisa.

Maswali yenu ni ya kitoto sana sana.
Na tatizo mnamlinganisha Mungu wa kwenye Biblia na Mungu wa kwenye Qurani.

Yesu hajawahi kuzaliwa wala kufa.
Yesu yupo tangu enzi na enzi na atakuja kuwahukumu walimwengu siku ya mwisho.

Mlicho ona nyinyi ni umbo la mwili, mwili kama ule alio uona Nabii Ibrahimu.
Na mtamuuliza Ibrahimu.
Mungu anakula? inayumnikanaje amchinjie ndama ili kumwandalia chakula ?
Kwani chakula alikitengeneza nani? 🤣🤣🤣🤣
Mungu akiwa katika ishara au dalili ya umbo la mwili wa Binadamu, basi anaweza kufanya mambo yote mema ya Kibinadamu.

Akili zenu zinaishia hapo kwenye uwezo wa kuona kwa macho ya nyama.
Ndio maana maswali yenu yapo kimwili mwili tu.

You are out of holy spiritual reams.
Utawasikia
Inayumnikanaje Mungu ana Mwana ilhali hajaoa mke? (hana mke)
Yaani huwa nacheka hadi najikojolea maji.
 
Shalom,

Habari kwenu nyote wadau wa jukwaa hili, nimekuwa nikijiuliza sana haya maswali kwanini Yesu hakuoa, Kwanini Yesu hakuwa na mwanafunzi wa kike, kwanini Yesu pia hakuwa na ukaribu wala urafiki na wanawake?

Hili fumbo linatupatia Mtihani gani ?
Tusaidiane kufikiria, karibu kwa rejea nyingi na majibu.

Wadiz
Maisha ya Yesu mtililiko wake ndio ule ule tu wa kwenye biblia. Alizaliwa kwenye zizi la ng'ombe akahamahama na wazazi wake akiwa mtoto mchanga baada ya hapo story inaenda kuibukia akiwa na miaka 12 alipopoteana na wazazi wake kule hekaluni halafu story inakuja kuibukia ashakua mtu mzima kule kwenye miujiza harusini akabatizwa akaanza kuubiri, nje ya mtililiko huo maelezo mengine ni ya kutungwa tu kwaiyo hauwezi kupata jibu sahihi hapa. Hata ivyo kwa mujibu wa historia hakuna uthibitisho wa kwamba huyu Yesu ashawahi kuishi hapa duniani kwaiyo kuna uwezekano akawa ni fictional character tu.
Vile vile ukiwa kwenye mission maalumu ni salama zaidi kwako kukaa mbali na wanawake kwa sababu ni wasaliti, hawawezi kutunza siri na wanadanganyika kirahisi sana labda Yesu aligundua ilo mapema.
 
Yesu hayupo kwenye Historia ipi?
Historia ya Waisraeli Yesu yupo sana tu.
Ukienda Israeli utaoneshwa Yesu alipozaliwa, ndugu zake wapo hadii hii leo.
Kabila lake la Yuda bado lipo Israeli.
Mwote ambamo alifanya matendo yake Mupo.
Kaburi lake lipo hadi hii leo.
Ule mti alio upanda Zakayo upo.
Ule mti hata pale Bagamoyo Mantep na Kaole upo, una ishi zaidi ya miaka elfu nne. Pale Mantep uliza mti uliozama mnyororo, kipande cha mnyororo bado kipo mtini hadi leo, na una miaka zaidi ya elfu mbili na bado mchanga na unatoa matunda kama kawaida, nenda pale utaelezwa.

Watalii na Waumini kila kukicha wanaenda Israeli kushuhudia historia ya Yesu kiuhalisia wa Kiakiolojia.
Wewe unasoma Historia ya wapi kwani ?
Au unazungumzia Historia ya Isa ambayo haina uthibitisho wowote wa Kiakiolojia ?
Speak The Truth and The Truth will make you Free.
 
Yesu alikua rafiki mkubwa wa dada yake na Lazaro Martha,pia yesu alikua rafiki na Maria Magdalena..
Inasemekana Magdalena alikuwa manzi wa jamaa na alikuwa anampelekea moto fresh tu?

Sema ujue nini Magdalena alikuwa pisi kinyama.
 
Back
Top Bottom