Kwanza mwanafunzi asichapwe, pili akipata mimba arudi shuleni, tatu kama ana utovu wa nidhamu pia arudi shuleni. Waoneeni huruma walimu

Kwanza mwanafunzi asichapwe, pili akipata mimba arudi shuleni, tatu kama ana utovu wa nidhamu pia arudi shuleni. Waoneeni huruma walimu

Wewe bana,hapa Tz mtoto atakula fimbo hutaki shika bango,mama samia akipita andamana.au anzisha shule yako.walimu wasiache kutumia fimbo

Tz mtoto analelewa kimaadili ya kitanzania.
Wewe piga fimbo kwani umekatzwa, tumeona wanao piga watoto wengine watoto walikuwa sugu na jeuri zaidi. Hayo ni machaguzo yako
 
Mkuu, sipingani na wewe.. tumeachana njia ya tunavyotaka kupita, ila mwisho wa siku jibu linaenda kuwa moja. Mimba inawekwa wakfu kwa ajiri ya usalama wa mtoto toma akiwa tumboni na kumtenganisha na kila kisicho cha Mungu, mtoto anazaliwa anawekwa wakfu kwa Mungu akue katika kimo na hekima akimcha Mungu na kumpendeza Mungu na wanadamu.. usikivu ukikomaa katika kumtii Mungu zaidi kwa huyo mtoto kiwango kikubwa cha utii kitakuwa kwa wazazi pia huto hitaji kiboko but ni chaguo naweza nisipige kiboko nikamyima chakula au uhuru flani na ikawa adhabu kali zaidi yenye kumfanya kuwa nidhamu
Nakwambia wewe mjuzi fanya hivo kwako! Lakini kwangu hapana!
 
Basi lea wa kwako hivo usitulazimishe jjinga unaouamini watu wote tuamini hivo! Ngoja sie tufate maandika yanavo sema tukiwalea watoto kwa kuwafundisha kiroho na wakizingua kimwili tunawachapa kwa lengo la kuwekana sawa sio kuumizana! Hao watoto wa kota za jeshi au polisi sio kigezo cha kuwafanya watu waache kuwakanya watoto wao! Hapo umefeli!
Kwani wapi nimelazimisha uamini ninacho amini? Alafu kwanza wewe ndio wa kwanza kuni quote
 
Uoga wako tu. Wewe unadhani kumomonyoka maadili ni watu kujamiana tu? Iwe jamii tofauti au jamii moja. Hauoni dhulma, ubakaji wa watu wazima na watoto, uuaji wa vikongwe, uuaji wa albino, unyang'aji, uvunjaji wa nyumba ( grili zinathibitisha hiyo), ufisadi, ubamizaji wa kutisha wa wake zetu na watoto wetu, rushwa iliyokithiri.

Kutiwa ndani kwa kuonewa, kupigwa na kuwekwa ndani kwa sababu una jog asubuhi au umevaa fulana fulani, kufa kwa sababu huna hela ya kuhonga, kufa kwa sababu hamna dawa hospitali, kufa kwa sababu umeshindwa kufika hospitali, kufa kwa sababu hospitali haina vifaa, baada ya kufa maiti yako kuzuiwa kwa sababu huna pesa, watu kuvunjiwa vibiashara vyao bila compesation na kadhalika na kadhalika. Watu mnatembea na vibameidi na mabinti wa kazi wenye miaka 13 na mnajiona mashujaa!

Wewe unaona tatizo kubwa ni binti kuruhusiwa kuendelea na masomo baada ya kupata mimba kutokana na kubakwa! Au watu wazima wa jinsia moja kujamiana kwa hiari yao? Kitu ambacho kipo miaka yote, hata kabla hao mabeberu kuanza kututembelea. Mnafik mkubwa wewe.

Amandla....
Tatizo sio kama unavyotafasiri hapo , tatizo kubwa kwenye issue ya maadili ni pale inapoleta picha akilini mwa watu kuwa zile kamba za maadili sasa zimelegezwa , picha hiyo inafanya kazi na kuleta madhara automatically kwenye maadili yote kwa ujumla, hilo la kwanza
La pili , ni kwamba ukichunguza hao wanaoua albino, wezi, vibaka n.k ni wale walioshindikana hata shuleni wakivuta bangi, je tunataka kundi lote liwe kama hao? Shuleni ndio mahala pekee panaposaidiana na dini kutunza maadili katika vijana wanaokaribia kuacha familia zao na kuingia mtaani, je ndio waandaliwe kwa style kama hizo , wajifunze kuwa huko kwenye jamii ni ovyo tu hakuna morals/ maadili hayazingatiwi? Unategemea nguvu waliyonayo kama itaachwa bila maadili vijana wanaweza kutenda matendo gani kwenye jamii?
" BADO JAMII HAIJAFIKIRI VIZURI JUU YA HILI"
 
Back
Top Bottom