Kwanza tuache kusema "Wamasai wa Ngorongoro"

Kwanza tuache kusema "Wamasai wa Ngorongoro"

May Day

JF-Expert Member
Joined
May 18, 2018
Posts
6,311
Reaction score
9,027
Nimekuwa napata ukakasi sana kuhusu matumizi ya haya maneno kwani ni dhahiri kuwa Matatizo pia yaweza kuwa yanaanzia hapa.

Kwanza sitaki kuamini ya kwamba hilo eneo ni la/au ni kwa ajili ya Jamii ya Kimasai pekee, na pia siamini kama waishio huko ni hao Wamasai pekee.

Pia kwa kutumia na kusisitiza kunasibisha eneo hili na Wamasai pekee ni kama ndio kunawapa kiburi cha kuamini hayo ni maeneo yao, kana kwamba Mungu aliwakabidhi wao tu...tofauti na ninavyofahamu mimi kwamba ardhi hii ni mali ya kila Mtanzania, na Raisi ndio Msimamizi kwa niaba ya Watanzania wote.

Ndio maana hata Viwanja tukimilikishwa tunapewa muda maalumu wa kumiliki, kwamba mkataba ukiisha Mamlaka kwa niaba ya Wananchi Wenzako wote wanaweza kukwambia hatukuongezei tena muda wa kukaa eneo hili hivyo tafuta sehemu nyingine.

Hali inapaswa kuwa hivyo hivyo kwa kila Mwananchi bila upendeleo wala umaalumu wa Jamii moja kutoka nyingine.

Kama Mndengereko wa Mtwara atatakiwa ahame Kijiji tupitishe bomba la Gesi kwa manufaa ya Wananchi wote wakiwepo wale waishio Kigoma, basi hili laweza kumkuta pia Muha aishiye Kigoma, Mhehe aishiye Iringa, Mmasai aishiye Oldonyosambu n.k.

Na mbona Wamasai hao hao kama tu Jamii nyingine wamekuwa wakihama kutoka eneo moja hadi lingine tangu kale?.. Wangoni walitokea Kusini mwa Afrika, Wa iraq wametokea Kaskazini wa Africa...vipi leo waone ugumu wakiambiwa tunataka muhamie kati kati ya Nchi?.

Sitounga mkono iwapo hili litafanywa kwa manufaa ya Wachache lakini nitaunga mkono kama litafanywa kwa manufaa ya wengi, na kwa bahati mbaya au nzuri mpaka sasa sijaona sababu za kuniridhisha kuwa kinachofanywa ni uonevu na si kwa manufaa ya Uma wote wa Tanzania.

Mimi ni muumini wa mazingira na huwa natamani kuona lililo na nia njema linafanikiwa haswa kama ni kwa manufaa ya mazingira.

Kwa ujinga ambao Binaadamu tumekwishaufanya kwa Mazingira mpaka sasa naamini hata Mungu angetamani sisi Binaadamu wote tuangamie Wabaki Wanyama, Wadudu, Miti ,Milima, Mabonde n.k. isiyolipiza ubaya na ukatili wa sisi Viumbe Mwenzao Binaadamu.
 
Wamasai wanaua sana Simba na wanyama uko, wanakula sana wanyama pori na mara nyingine huwapa ramani poachers tembo walipo na huwapa hifadhi pia, wanyama kama simba na chui na tembo ukiangalia wanakaa mbali sana na walipo wamasai na kila siku wanaongezeka, njia ni moja tu,

Waamishwe wapelekwe kwingine, tatizo ni wanaona kitega uchumi chao kinaondoka, na nyerere hakuona mbele akawaacha humo, enzi hizo walikuwa makumi elfu sasa hivi ni zaidi ya laki5, baada ya miaka 20 watakuwa milion10.

Je wanyama wataishi wapi

Binadam tuna tanzania nzima ya kuishi na wanyama japo ni wengi tumewaachia kasehem kadogo
Sasa kwann tuwaaache wamasai wajazane na kuwapora wanyama eneo lao.

Mama we watoe humo baada ya miaka 10 wote watakuwa washasahau na kuzoea
 
Wamasai wanaua sana Simba na wanyama uko, wanakula sana wanyama pori na mara nyingine huwapa ramani poachers tembo walipo na huwapa hifadhi pia, wanyama kama simba na chui na tembo ukiangalia wanakaa mbali sana na walipo wamasai na kila siku wanaongezeka, njia ni moja tu, waamishwe wapelekwe kwingine, tatizo ni wanaona kitega uchumi chao kinaondoka, na nyerere hakuona mbele akawaacha humo, enzi hizo walikuwa makumi elf sahv ni zaidi ya laki5, baada ya miaka 20 watakuwa milion10
Je wanyama wataishi wapii
Binadam tuna tanzania nzima ya kuishi na wanyama japo ni wengi tumewaachia kasehem kadogo
Sasa kwann tuwaaache wamasai wajazane na kuwapora wanyama eneo lao
Mama we watoe humo baada ya miaka 10 wote watakuwa washasahau na kuzoea
Muongo
Huna uthibitisho wowote zaidi ya kutunga vijinamba.
Kwanza ni kosa la jinai kutunga takwimu.
 
Wanaharakati uchwara sikuwasikia kipindi nyumba za wakazi wa kimara na Mbezi zikibomolewa tena bila fidia ila Leo kwasababu mkate wao umeguswa wamekuja juu hao wanaojiita wanaharakati Wana NGOs zao huko kwenye jamii ya wamasai wanapiga pesa sana
 
Tukikuuluza we ni mtu wa wapi, utasema Mm naitwa "may day Mwanyiro mdigo mwenyeji Tanga wilaya ya mkinga kijiji Mwakijembe" Halafu hutak wamasai wawe na Asili?Ile ni ardhi yao kama waizraili walivyopewa kanaani na sayuni, kama Muarabu alivyopewa Makka ma Madina,Kama red Indians walivyopewa America,.Division hii kijiografia kaifanya Mungu muweza. Kila mtu ana Asili yake. #stopmasaieviction#
 
Nimekuwa napata ukakasi kuhusu matumizi ya haya maneno kwani ni dhahiri kuwa Matatizo pia yaweza kuanzia hapa.

Kwanza sitaki kuamini ya kwamba hilo eneo ni la/au ni kwa ajili ya Jamii yoyote na si ya Kimasai pekee, na pia siamini kama waishio huko ni Wamasai pekee.

Pia kwa kutumia na kusisitiza kunasibisha eneo hili na Wamasai pekee ni kama ndio kunawapa kiburi cha kuamini hayo ni maeneo yao, kana kwamba Mungu aliwakabidhi wao tu...tofauti na ninavyofahamu mimi kwamba ardhi hii ni mali ya kila Mtanzania, na Raisi ndio Msimamizi kwa niaba ya Watanzania wote.

Ndio maana hata Viwanja tukimilikishwa tunapewa muda maalumu wa kumiliki, kwamba mkataba ukiisha Mamlaka kwa niaba ya Wananchi wote wanaweza kukwambia hatukuongezei tena muda wa kukaa eneo hili hivyo tafuta sehemu nyingine.

Hali inapaswa kuwa hivyo hivyo kwa kila Mwananchi bila upendeleo wala umaalumu wa Jamii moja kutoka nyingine.

Kama Mndengereko wa Mtwara atatakiwa ahame Kijiji tupitishe bomba la Gesi kwa manufaa ya Wananchi wote wakiwepo wale waishio Kigoma, basi hili laweza kumkuta pia Muha wa Kigoma, Mhehe wa Iringa, Mmasai wa Oldonyosambu n.k.

Na mbona Wamasai hao hao kama tu Jamii nyingine wamekuwa wakihama kutoka eneo moja hadi lingine tangu kale?.. Wangoni walitokea Kusini mwa Afrika, Wa iraq wametokea Kaskazini wa Africa...vipi leo waone ugumu wakiambiwa tunataka muhamie kati kati ya Nchi?.

Sitounga mkono iwapo hili litafanywa kwa manufaa ya Wachache lakini nitaunga mkono kama litafanywa kwa manufaa ya wengi, na kwa bahati mbaya au nzuri mpaka sasa sijaona sababu za kuniridhisha kuwa kinachofanywa ni uonevu na si kwa manufaa ya Uma wote wa Tanzania.

Mimi ni muumini wa mazingira na huwa natamani kuona lililo na nia njema linafanikiwa haswa kama ni kwa manufaa ya mazingira.

Kwa ujinga ambao Binaadamu tumekwishaufanya kwa Mazingira mpaka sasa naamini hata Mungu angetamani sisi Binaadamu wote tuangamie Wabaki Wanyama, Wadudu, Miti ,Milima, Mabonde n.k. isiyolipiza ubaya na ukatili wa sisi Viumbe Mwenzao Binaadamu.
Kama wewe ni mwanamazingira kweli ungeanza na hao wanyama. Kwamba ikiwa nafasi haitoshi ku-coexist wao na binadamu nani ahame?

Kwamfano vyura wa project ya hydropower Kihansi (kama rare and endegered species) si baadhi yao walihamishiwa USA ili wasitoweke?

Kwahiyo punguzeni wanyama Ngorongoro (kama nao ni rare and endegered species) kutokana na idadi ya binadamu (Wamaasai) kuongezeka; basi hao wanyama waende Mikumi Ruaha au Chato nk.

Vinginevyo kuna jamii ya Watanzania ambayo hawaongezeki? Wanyakyusa Wandamba, Waluguru, nk wakiongezeka mtawahamishia wapi?

"Overriding interest" ya Serikali katika suala la ecosystem ya Ngorongoro lazima iwe uhai na ustawi wa binadamu! Sio wanyama au watalii au mapato ya nchi kama kodi, tozo, nk.
 
Vyombo vya habari vya Mapaka😁😁😁
image26.jpg
 
Wanaharakati uchwara sikuwasikia kipindi nyumba za wakazi wa kimara na Mbezi zikibomolewa tena bila fidia ila Leo kwasababu mkate wao umeguswa wamekuja juu hao wanaojiita wanaharakati Wana NGOs zao huko kwenye jamii ya wamasai wanapiga pesa sana
Nadhani kipindi hicho ulikuwa bado hujapata ufahamu.... Walipiga kelele sana ila ndo kelele za samaki majini.... Sasa masai ni mkate wa nani
 
Back
Top Bottom