Kwaresma na Pasaka Special Thread

Kwaresma na Pasaka Special Thread

Usela usela nipunguze usela, maana ujana na usela ni kutia chumvi kwenye pera
Dunia hii mtumish haina Raha ya kudumu

Unaweza kura Raha miaka 10 ikatokea siku moja tu ukawekwa jera na ile Raha yako uliyo kula miaka inapotea hapo hapo, unaanza mateso

Kwahiyo jipatanishe na KRISTO YESU
 
Amani iwe kwenu watumishi wa MUNGU katika kristo YESU

Tumsifu YESU KRISTO. AMINA

Tumshukuru MWENYEZI MUNGU kwa kila jambo hasa kwa kumtuma mwanae aje atukomboe . AMINA

PASAKA ni nini pasaka ni kuteseka/mateso/ kifo/kufa/na kufufuka kwa YESU KRISTO

PASAKA ilianzia misiri lakini badae wana wa Israel MWENYEZI MUNGU aliwaagiza waadhimishe pasaka kama kumbukumbu la kwamba wao walikuwa watumwa wa mateso huko misiri

Hivyo wakristo kwa sasa huadhimisha pasaka kama kumbukumbu la kwamba TULIKUWA WATUMWA/ WAFUNGWA WA MINYORORO YA SHETANI mpaka pale BWANA wetu YESU KRISTO alipokuja kutukomboa kwa mateso yake makali pale msalani

Je kwaresma ni nini, kwaresma ni ibada ni ibada ambayo husindikizwa na mfungo wa siku 46 kutoa Dominika 6 hivyo siku hubaki 40

Kufunga kwaresma ni kufanya nini, kufunga ni kuyakalibisha mateso ya YESU KRISTO ambaye ni mfufua wa ulimwengu wote

Hivyo wewe uliyefunga unapaswa kuwapikia wengine ambao hawajafunga na kutoa pesa yako iliyopaswa kula ili uwalishe ndugu na watu Baki

Lakin ndugu zangu kufunga bila sala huko ni kushinda NJAA kabisa
Kufunga bila kunuia jambo flani huko nako ni kushinda NJAA kabisa

Lakin pia kwaresma huanza na jumatano ya MAJIVU

MAJIVU ni nini, MAJIVU hutukumbusha kwamba sisi wanadamu ni mavumbi na mavumbini hakika tutarudi

Masomo husika yoel 2:12-18
Injili husika mathayo 6:1-6,16-18

Moderate tafdhari nawaomba uzi huu msiuunganishe maana uzi utakuwa wa milele kwa update za kila siku juu ya neno la MUNGU la kipindi cha kwaresma

Basi nawakaribisha tufunge na tumuombe MUNGU wetu aliye mwema sana

SAYUNI BOY
Pamoja na maelezo, uchambuzi na ufafanuzi mzuri katika hoja ya msingi,

nina maswali madogo mawili ya nyongeza kwa pamoja,

Je,
kwa mwaka huu, kwaresma itaanza lini na Pasaka itakua lini?🐒
 
Alhamisi this week, right?
kwa Neema na Baraka za Mungu nikipata wasaa mzuri nitashiriki ibada hiyo muhimu Jimbo kuu la Dar es salaam katika Parokia Ya Roho Mtakatifu segerea ikiwa patakua na ibada ya jioni 🐒
Ni jumatano siyo alhamisi

Lazima iwepo jion

Jumatano ya majivu ndo ibada pekee inayo kusanya watu wengi zaid katika kanisa
 
Back
Top Bottom