Kwaresma na Pasaka Special Thread

Kwaresma na Pasaka Special Thread

Tumebakiwa na siku masaa machache sana kesho jumatano tarehe 5 tutaanza kipindi cha kwaresma kwa mfungo tukianza kwa jumatano ya majivu
 
Ratiba ya ibada ya MAJIVU kanisa kuu la st Joseph
 

Attachments

  • IMG_20250304_102842_805.jpg
    IMG_20250304_102842_805.jpg
    586.7 KB · Views: 2
Ratiba ya kufunga kula inakuaje mkuu?
Ratiba inakuwa kama ifuatavyo

Tunafunga chakula yaan tunafunga kula siyo kula kidogo

Unapoamua kufunga wewe funga siyo ule kidogo hapana

Na mwisho wa kula ni mda wa usiku siyo unaamka tena usiku saa 11 unaanza kula daku hapana, huko kutakuwa ni kubadilisha ratiba ya kula tu wala siyo kufunga

Na kufungua tunafungua saa 12 lakin jitaid kabla hujafungua kwa chakula unapiga hata Sala kidogo

Usipende kufungua chakula kabla hujasali

Asante mtumish
 
Mnajishindisha njaa tuu hamna kufunga wala nini!! Nyie Kuleni kitimoto na pombe ndo Vitu vyenu nyie na kufunga Wapi na wapi bhnaaa
 
Amani iwe kwenu watumishi wa MUNGU katika kristo YESU

Tumsifu YESU KRISTO. AMINA

Tumshukuru MWENYEZI MUNGU kwa kila jambo hasa kwa kumtuma mwanae aje atukomboe . AMINA

PASAKA ni nini pasaka ni kuteseka/mateso/ kifo/kufa/na kufufuka kwa YESU KRISTO

PASAKA ilianzia misiri lakini badae wana wa Israel MWENYEZI MUNGU aliwaagiza waadhimishe pasaka kama kumbukumbu la kwamba wao walikuwa watumwa wa mateso huko misiri

Hivyo wakristo kwa sasa huadhimisha pasaka kama kumbukumbu la kwamba TULIKUWA WATUMWA/ WAFUNGWA WA MINYORORO YA SHETANI mpaka pale BWANA wetu YESU KRISTO alipokuja kutukomboa kwa mateso yake makali pale msalani

Je kwaresma ni nini, kwaresma ni ibada ni ibada ambayo husindikizwa na mfungo wa siku 46 kutoa Dominika 6 hivyo siku hubaki 40

Kufunga kwaresma ni kufanya nini, kufunga ni kuyakalibisha mateso ya YESU KRISTO ambaye ni mfufua wa ulimwengu wote

Hivyo wewe uliyefunga unapaswa kuwapikia wengine ambao hawajafunga na kutoa pesa yako iliyopaswa kula ili uwalishe ndugu na watu Baki

Lakin ndugu zangu kufunga bila sala huko ni kushinda NJAA kabisa
Kufunga bila kunuia jambo flani huko nako ni kushinda NJAA kabisa

Lakin pia kwaresma huanza na jumatano ya MAJIVU

MAJIVU ni nini, MAJIVU hutukumbusha kwamba sisi wanadamu ni mavumbi na mavumbini hakika tutarudi

Masomo husika yoel 2:12-18
Injili husika mathayo 6:1-6,16-18

Moderate tafdhari nawaomba uzi huu msiuunganishe maana uzi utakuwa wa milele kwa update za kila siku juu ya neno la MUNGU la kipindi cha kwaresma

Basi nawakaribisha tufunge na tumuombe MUNGU wetu aliye mwema sana

SAYUNI BOY
Kwaresma, Majivu, Ijumaa kuu vyote ni church politics, haviko kwenye Biblia kuwahusu wakristo wa leo.
Yesu alishateswa, kusurubiwa, kufa, kufufuka na kupaa zake mbinguni zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Kilichobakia kwa sasa Injili ipigwe kwa kwenda mbele na Yesu ainuliwe milele.
 
Sisi tunafunga ndugu yangu karbu tuungane kwa mfungo
Tunafunga ili iweje? yesu amesha tukomboa Hatuna dhambi,... alafu tayari yesu amesha jua nani ataenda motoni na nani ataenda kwa roho mtakatifu kama umesha wekwa kwenye kundi la motoni hata ufunge kizazi hautoboi
 
Kwaresma, Majivu, Ijumaa kuu vyote ni church politics, haviko kwenye Biblia kuwahusu wakristo wa leo.
Yesu alishateswa, kusurubiwa, kufa, kufufuka na kupaa zake mbinguni zaidi ya miaka 2000 iliyopita. Kilichobakia kwa sasa Injili ipigwe kwa kwenda mbele na Yesu ainuliwe milele.
Kwahiyo ijumaa kuu yaan mateso ya YESU ni kinyume na injili yaan siyo injili?

Kwahiyo na kufunga nako si injili mtumish?

Unaielewaje injili wewe binafis
 
Back
Top Bottom