Kwaresma na Pasaka Special Thread

Kwaresma na Pasaka Special Thread

Jifunze Kwaresma
 

Attachments

  • Screenshot_20250303_084322_Instagram.jpg
    Screenshot_20250303_084322_Instagram.jpg
    245.1 KB · Views: 3
Ij
Kufunga kwaresma tunaanza kesho ndugu yangu

Kanuni ni kama ifuatavyo

Tunafunga kuanzia asubuh mpaka jion saa kumi na mbili

Lakin kabla hujafungua unasali kwanza

Jitaid kunuia jambo mbele ya MUNGU MWENYEZI iwe changamoto au shukrani

Usifunge bila kusali itakuwa ni sawa sawa na kushinda NJAA tu

Lakin pia siyo unafunga tena usiku unaamka kula hapana hiyo siyo funga

Kama una swali lingine uliza mtumish
Kuna mtu kaniambia hapa kuwa unakunywa maji na unakula kidogo ila usishibe hii ni kweli?
 
Asanten sana jamani

Nimeona vijana wengi wa kiluther kkkt wamepaka majivu
 
IMG-20250302-WA0061.jpg


IFANYE KWARESMA 2025 KUWA YA TOFAUTI KIROHO

🟪🟪 Kwaresma ni kipindi maalum sana kiroho, ni safari ya kwenda nyikani na Bwana Yesu kwa muda siku 40.

🟪🟪 Kipokee kipindi hiki kama fursa ya Kiroho kwani ni kipindi cha kufunga, Kusali, Kutubu, na Kufanya matendo ya Huruma kwa wahitaji.

🟪🟪 Jiandae kiroho kwa kufanya toba halisi.

🟪🟪 Usiingie kwenye mfungo huu maalum ukiwa moyo wako una makwazo ama manung'uniko yeyote achilia kila jambo lililo gumu na ubaki huru.

🟪🟪 Weka nia maalum ya mfungo kwa kutenga na kumwambia Mungu akupe msaada hasa changamoto nzito na ngumu ambazo kwa upande wako unaziona huziwezi.

🟪🟪 Kama huna changamoto yeyote ya kiafya mfano kama si mjamzito ama husumbuliwi na ugonjwa wowote tafadhari jinyime kwa kutokula chakula.

🟪🟪 Usifunge kwa kujionyesha kwa watu kwamba na wewe umefunga, funga kwa kusudi ama nia uliyoikusudia ili Mungu akupe msaada wake.

🟪🟪 Kumbuka kipindi hiki hutokea mara moja tuu kwa mwaka hivyo ifanye kama fursa ya kiroho ambayo mara tuu baada ya kumaliza mfungo utavuna na kujiwekea akiba kubwa ya kiroho.

🟪🟪 Uwapo kwenye mfungo waombee na watu wengine kwani ukifanya hivyo Mungu atapokea maombi yako haraka na kwa urahisi.

🟪🟪 Saidia wahitaji hasa kwenye kipindi hiki cha Kwaresma, watu wote Mungu amewaumba kwa mfano wake hivyo unavyowasaidia tambua kwamba unagusa mboni yake.

🟪🟪 Omba kwa imani na Mungu ataisikia sauti yako

🟪🟪 Omba kwa kumaanisha na Mungu ataenda kukutendea sawa sawa na mapenzi yake

🟪🟪 Safari hii ya siku 40 itakuwa ni historia kwenye maisha yako kwani ukifunga na kuomba kwa imani Mungu ataenda kuruhusu mambo makuu mnoo yatendeke maishani mwako.

🟪🟪 Nakutakia Mfungo mwema wa Kwaresma na Mungu akubariki sana 🙏🏿🙏🏿🙏🏿
 
Back
Top Bottom