Kwaya ya Mt. Kizito Makuburi chukueni hatua za kisheria dhidi ya Diamond & Zuchu

Kwaya ya Mt. Kizito Makuburi chukueni hatua za kisheria dhidi ya Diamond & Zuchu

Sun Zu

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2022
Posts
636
Reaction score
1,819
Sina chuki na Huyu Bwana Diamond, huwa napenda sana nyimbo zake, ni burudani tosha.

Ni takribani mwezi sasa toka huyu Bwana na bint Zuchu watoe wimbo wao walioupa jina 'Mtasubiri sana'. Ni wimbo mzuri katika muktadha wa burudani.

Ukakasi unakuja katika video ya wimbo huu. Kile kinachoonekana katika sekunde za mwanzo za wimbo huu ni dharau na kejeli kwa ukristo, na zaidi kwa kwaya ya Mt. Kizito Makuburi.

Uongozi wa Kwaya ya Mt. Kizito, Mwenyekiti, chukueni hatua za kisheria dhidi ya hawa watu, hatuwezi kuruhusu wimbo wetu wa YESU NI MWEMA kutumika kuinajisi imani, na katika hili hakuna kumuachia MUNGU. Chukueni hatua, shitakini huyu mtu kwa kutumia maudhui ya wimbo bila ridhaa ya kwaya, shitakini huyu mtu kwa kukashifu imani ya wengine.

Dharau dhidi ya imani nyingine sio mara ya kwanza kufanywa na huyu Bwana. Miaka kadhaa nyuma alishawahi kutoa wimbo kwa jina 'Hallelujah' huku wimbo huo ukisifia mambo ya kiasherati.

Kwa kuwa hawa wawili, Diamond na Zuchu wote ni waislamu, na kwa kuwa misikiti ipo mingi tu, kiliwashinda nini kuigiza Zuchu yupo msikitini anaimba Qaswida na diamond yupo club anampigia Zuchu simu kisha huyu bint anaacha Qaswida na kumfata Diamond waanze kutongozana?

Hizi ni dharau na dhihaka kwa wakristo! Kwamba bint mcha Mungu anathamini zaidi uasherati, anaacha kuimba kwaya anakimbilia uhuni, stupid!

Kumnyamazia kimya sio sahihi, he needs to be taught a lesson, mbona nyimbo zake ni nzuri tu bila kuingiza vikorombwezo vya dharau na dhihaka dhidi ya imani nyingine?

Haya anayoyafanya kwa imani ya kikristo anaweza kuthubutu kuifanyia imani yake islam?


#AchaDharau
 
Mimi ni mkiristo kabisa sioni shida yoyote kwenye ule wimbo. “ IFIKE MAHALI WAKRISTO TUACHE MIHEMUKO ! ... kama ameshakubali kuwa Yesu ni Mwema sana kwanini roho zetu zimekuwa na ufitina sasa !! .... Msanii ameakisi kile kilichopo kwenye jamii hivi sasa !! Miaka 29 ya ukristo “Mungu awasaidie kuelewa tangulizeni hekima mbele”
 
Mimi ni mkiristo kabisa sioni shida yoyote kwenye ule wimbo. “ IFIKE MAHALI WAKRISTO TUACHE MIHEMUKO ! ... kama ameshakubali kuwa Yesu ni Mwema sana kwanini roho zetu zimekuwa na ufitina sasa !! .... Msanii ameakisi kile kilichopo kwenye jamii hivi sasa !! Miaka 29 ya ukristo “Mungu awasaidie kuelewa tangulizeni hekima mbele”
Uko sahih Sana mkuu wkt mwinginee tuache miemko kasha kiri yesu Ni mwema mnataka nn nyie wakristo
 
Mimi ni mkiristo kabisa sioni shida yoyote kwenye ule wimbo. “ IFIKE MAHALI WAKRISTO TUACHE MIHEMUKO ! ... kama ameshakubali kuwa Yesu ni Mwema sana kwanini roho zetu zimekuwa na ufitina sasa !! .... Msanii ameakisi kile kilichopo kwenye jamii hivi sasa !! Miaka 29 ya ukristo “Mungu awasaidie kuelewa tangulizeni hekima mbele”
Usilamu sasa, angeuweza Moto wa masheikh? Achutame tu, aombe radhi na kuahidi kurekebosha sio kila akikosolewa anaona anaonewa tu
 
Embu jiulize ingekuwa Wakristu wawili, wanaigiza wanapigiana simu mmoja yupo msikitini, anatoka anaanza kutongozwa hali ingekuwaje? Embu tuendelee kuheshimu imani za watu wengine hata kama kwa imani zetu tunaafikiri wanatenda makosa, tuwaache na makosa yao kwa kuwa hayaingilii uhuru wetu.Lakini tusifanye jambo lolote la kuonyesha kuwa imani ya mwenzako ni dhaifu

Walikuwa na uwezo kabisa kipande hicho, wakafanyia msikitini kwa kuwa wote ni waislam, na Tanzania miskiti ipo kila mtaa na huyo binti angeitwa akiwa anaimba qaswida, isingeleta shombo yoyote
 
Embu jiulize ingekuwa Wakristu wawili, wanaigiza wanapigiana simu mmoja yupo msikitini, anatoka anaanza kutongozwa hali ingekuwaje? Embu tuendelee kuheshimu imani za watu wengine hata kama kwa imani zetu tunaafikiri wanatenda makosa, tuwaache na makosa yao kwa kuwa hayaingilii uhuru wetu.Lakini tusifanye jambo lolote la kuonyesha kuwa imani ya mwenzako ni dhaifu

Walikuwa na uwezo kabisa kipande hicho, wakafanyia msikitini kwa kuwa wote ni waislam, na Tanzania miskiti ipo kila mtaa na huyo binti angeitwa akiwa anaimba qaswida, isingeleta shombo yoyote
CC sonofobia , asubuhi sana
 
Ebu tuelezee tuelewe kwamba kainajisi vip dini na huo wimbo wa mt makuburi.

Me niliona simu inaita akaiangalia na kutuonyesha watazamaji, akatoka nje kuipokea na kutokomea mazima

Ili tusiwe wafata mkumbo kama wengine, kwani tatizo linanzia wapi ? Muslim kuimba kwaya, kuingia kanisani, au mihemko
 
Ebu tuelezee tuelewe kwamba kainajisi vip dini na huo wimbo wa mt makuburi.

Me niliona simu inaita akaiangalia na kutuonyesha watazamaji, akatoka nje kuipokea na kutokomea mazima

Ili tusiwe wafata mkumbo kama wengine, kwani tatizo linanzia wapi ? Muslim kuimba kwaya, kuingia kanisani, au mihemko
Bint, mkristo, katika mazoezi ya kwaya ya kumsifu Mungu anaona simu ya mhuni, anatoka kuipokea anapigwa vocal, anaona kwaya upuuzi analala mbele kwa muhuni wake.

Kwamba masifu kwa Mungu hayana uzito kwa ukristo ila uhuni na uasherati unatuzidi, hii ni tafsiri kwamba imani ya kikristo ni dhaifu na ndio maana wameamua kuichezea chezea
 
Kwenye ule wimbo wa Banana wa Zoba mbona wanaonesha wanaimba kwaya na wanatoka nje wanatongozana, Kimyaaaaaa

Kuna wimbo wa Rosa Ree I'm not Sorry anaingia Kanisani kavaa nusu uchi, kashika chupa ya pombe huku anavuta bangi akaenda hadi kwa Padri kuungama, kimyaaaaa

Kuna ile Movie ya Kibongo ya Sister Maria Uwoya alifanya kufuru mule ndani, Kimyaaaaaaa

Sio shabiki wa Mondi ila hapo naona ni chuki zimetumika, tuwaonee huruma hao vijana wanatafuta rizki kwa shida sana.
 
Bint, mkristo, katika mazoezi ya kwaya ya kumsifu Mungu anaona simu ya mhuni, anatoka kuipokea anapigwa vocal, anaona kwaya upuuzi analala mbele kwa muhuni wake.

Kwamba masifu kwa Mungu hayana uzito kwa ukristo ila uhuni na uasherati unatuzidi, hii ni tafsiri kwamba imani ya kikristo ni dhaifu na ndio maana wameamua kuichezea chezea
Punguza Jazba

 
Ebu tuelezee tuelewe kwamba kainajisi vip dini na huo wimbo wa mt makuburi.

Me niliona simu inaita akaiangalia na kutuonyesha watazamaji, akatoka nje kuipokea na kutokomea mazima

Ili tusiwe wafata mkumbo kama wengine, kwani tatizo linanzia wapi ? Muslim kuimba kwaya, kuingia kanisani, au mihemko
Acha kushupaza libichwa we guruguja
 
Back
Top Bottom