Kukubali kitu kuwa bila ya kuwa na uthibitisho kwamba kipo.
imani ni ushahidi wa vitu visivyoonekana.
Mfano kuna mechi ya simba na yanga halafu mia nikasema hivi:
"Naamini kuwa Yanga atamfunga simba"
Je, unauelezea vp mfano wangu huo kuendana na tafsiri yako ya neno imani.
Hiyo si fact. Ni kitu ulichojikubalisha tu kwamba Yanga atamfunga Simba.
Lakini inaweza kukosea kabisa na Simba akamfunga Yanga.
Huwezi kufanya imani iwe fact.
Sijasema kwamba hiyo ni fact. Hebu soma vizuri swali langu.
Je, unauelezea vp mfano wangu huo kuendana na tafsiri yako ya neno imani.
Kumbuka kuwa sijasema habari za fact ninazungumzia imani. Ukiona inakupa shida sema mie niuelezee mfano wangu huo kuendana na tafsiri ya neno imani nijuavyo.
You can say whatever you want to say, but without evidence to support your malarkey, is dumbicious. Science is based on evidence that is verifiable, repeatable, and testable.Ni sawa na nikikwambia binadamu ana macho matatu, halafu ukibisha nitake tena wewe ndio unithibitishie hana hilo jicho la tatu ambalo wewe hulioni
I told you the thing doesn't exist at all
Kama roho ipo, unaweza kuthibitisha?
Kama huwezi, unajuaje kwamba ipo?
Hebu nipe mifano japo mitatu kuhusu hilo neno imani yenye kuendana na tafsiri yako.
Mtoa mada hajauliza kama unaamini kuwa roho ipo, ameuliza kama roho ipo.
Unajibu swali ambalo hujaulizwa (kwamba unaaamini au huamini roho ipo) na lile ambalo umeulizwa (kama roho ipo) hujalijibu.
Nilijua tu yatakushinda sababu siku zote njia ya muongo ni fupi,sasa hivi ndiyo unajua alichokiuliza mtoa mada, ila wakati tunajadili kuhusu imani hukujua mtoa mada anauliza nini hadi ulipoona umekwama ndiyo unakumbuka mada inasema nini.
Tatizo bado liko palepale, ni kwamba wewe kushindwa kuelewa au kutaka kupotosha neno imani nililotumia kuelezea roho. Kwahiyo huwezi kuniambia sijajibu nilichoulizwa kama itakuwa neno imani halijaeleweka.
Nikikwambia unitajie rangi ya sauti yako halafu wewe ukasema kuwa sauti haina rangi. Je,itakuwa ndiyo hujajibu swali langu? kwa sababu mie nimeuliza rangi ya sauti we unaniambia sauti haina rangi.
Binadamu ambae anafikiri vizuri hawezi kusema kitu fulani hakipo kwasababu tu hajawahi kukiona au hakina ushahidi bali husema hajui kama kipo au hakipo
Huyu anatafakari vizuri sana kwasababu hana ishahidi either way
Lakini wewe unaesema hakuna hiyo inakuwa inamaana kwamba tayari unaushahidi wa kilichokufanya useme hakuna na hiki ndio kinachohitajika hapa
Unasemaje hakuna bila kutupa ushahidi wa hakuna yako?
Sijui kama umeona matatizo ya mtazamo wako!
1. imani yako imekuponya- tuchukulie unaumwa ukienda kwa mchungaji wako ukiamini atakuponya ni kweli utapona lakini aliyekuponya si mchungaji ni wewe mwenyewe umejiponya!
2. ukiamini kufanikiwa utafanikiwa na ukiamini kushindwa utashindwa pia!
3. ukiamini kitu kibaya kitokee kitatokea kweli na ukiamini kitu kizuri kitokee kitatokea pia!
this is the LAW OF ATTRACTION like attracts like and the contrary is the fact.
Maisha ya binadamu ni kama sumaku.
You can say whatever you want to say, but without evidence to support your malarkey, is dumbicious. Science is based on evidence that is verifiable, repeatable, and testable.
That is why all non theists are mindless and dumb.
Hujabadili ukweli kwamba ulichoulizwa si "unaami i kwamba roho ipo?" Ila ni "roho ipo?".
Ukiinguza habari za imani kila mtu ana imani yake, na unaruhusiwa kuamini chochote, kwa hiyo kuanza kujadili imani ni upuuzi.
Ndiyo maana mtoa mada hakuuliza kuhusu imani yako, kauliza from a factual context.
Mbona unatapatapa mkuu? Wapi nilipoeleza imani yangu?
Mie nimesema swala roho ni swala la imani halafu ndiyo nikaeleza roho ni nini.
I did it already. You must be dumb for not seen my cross exam.Then prove me wrong
Ukishasema suala la roho ni suala la imani ushatoka nje ya swali.
Kwa sababu imani kila mtu anaruhusiwa kiwa nayo na hakuna jinsi ya kuanza kupima imani, kwa sababu imani ni kukunali kitu kabla ya uchinguzi.
Mleta mada ameuliza swali kwenye context ya fact.
You got it wrong from the get go.
Ni hali ya kutimia kwa vigezo!
Anaita sasa!
Sasa mkuu kuna watu ambao walikuwa wanaumwa tukaamini watapona ila hawakupona wakafa.
Kuna wengine waliamini mwaka 2010 Dr.Slaa angeshinda urais ila haikuwa hivyo. Mara ngapi shuleni huwa tunaamini baadhi ya watu watafaulu mitihani ila matokeo yakitoka inakuwa tofauti na tulivyoamini.
Je,unazungumzia vp hapo?