KikulachoChako
JF-Expert Member
- Jul 21, 2013
- 19,185
- 37,239
Leo nimekumbuka kiss hiki cha miaka kadhaa nyuma.....
Nilikuwa na rafiki yangu mpendwa alikuwa na mchumba ambaye ni shemeji yangu ambapo walikuwa mbioni kufunga ndoa.....na maandalizi na harakati za hapa na pale yalishaanza.....
Ni Shem ambaye tulizoeana kwa kuwa mara kadhaa nilikuwa nikifika kwa rafiki yangu nawakuta ingawa walikuwa hawaishi pamoja........
Siku moja na pita pita mitaa ya kariakoo nakutana na rafiki yangu wa siku nyingi tulisoma naye shule ya msingi miaka mingi iliyo pita.....katika harakati za kuchangamkiana tukajikuta tunapanga siku ya kuonana ili tuongee mengi zaidi maana aliniambia anaishi maeneo ya kigamboni.......
Basi weekend moja nikamtaarifu kuwa naenda kumtembelea na yeye alifurahi sana akaniambia kuwa itakuwa vizuri pia umjue Shemeji yako maana na yeye amekuja leo......nikamwambia Sawa.....
Masaa kadhaa nikawa nimefika aliponielekeza nishukie akamtuma kijana kuja kunichukua kuelekea nyumbani kwake.....si haba ilikuwa nyumba ya kisasa......
Wakati tukiendelea na maoengezi ya hapa na pale akamuita Shem aje nimsalimie.....laahaulah!! Ni yule mchumba wa rafiki yangu kule mtaani.....cha ajabu yule mwanamke hakuonesha mshtuko wowote nami nikauchuna kimya.....
Mida ilipotimu nikaaga nikaondoka zangu......Ile picha pale iliniachia maswali mengi sana lakini nikaamua kukaa kimya na kuendelea na maisha yangu......
Mpaka nahama pale mtaani Yule rafiki yangu alikuwa hajafunga ndoa bado na Yule bibie na kule kwa jamaa yangu kigamboni sikuulizia lolote kuhusu yeye na Yule bibie........
DAH!
KWELI KUISHI KWINGI NI KUONA MENGI........
Nilikuwa na rafiki yangu mpendwa alikuwa na mchumba ambaye ni shemeji yangu ambapo walikuwa mbioni kufunga ndoa.....na maandalizi na harakati za hapa na pale yalishaanza.....
Ni Shem ambaye tulizoeana kwa kuwa mara kadhaa nilikuwa nikifika kwa rafiki yangu nawakuta ingawa walikuwa hawaishi pamoja........
Siku moja na pita pita mitaa ya kariakoo nakutana na rafiki yangu wa siku nyingi tulisoma naye shule ya msingi miaka mingi iliyo pita.....katika harakati za kuchangamkiana tukajikuta tunapanga siku ya kuonana ili tuongee mengi zaidi maana aliniambia anaishi maeneo ya kigamboni.......
Basi weekend moja nikamtaarifu kuwa naenda kumtembelea na yeye alifurahi sana akaniambia kuwa itakuwa vizuri pia umjue Shemeji yako maana na yeye amekuja leo......nikamwambia Sawa.....
Masaa kadhaa nikawa nimefika aliponielekeza nishukie akamtuma kijana kuja kunichukua kuelekea nyumbani kwake.....si haba ilikuwa nyumba ya kisasa......
Wakati tukiendelea na maoengezi ya hapa na pale akamuita Shem aje nimsalimie.....laahaulah!! Ni yule mchumba wa rafiki yangu kule mtaani.....cha ajabu yule mwanamke hakuonesha mshtuko wowote nami nikauchuna kimya.....
Mida ilipotimu nikaaga nikaondoka zangu......Ile picha pale iliniachia maswali mengi sana lakini nikaamua kukaa kimya na kuendelea na maisha yangu......
Mpaka nahama pale mtaani Yule rafiki yangu alikuwa hajafunga ndoa bado na Yule bibie na kule kwa jamaa yangu kigamboni sikuulizia lolote kuhusu yeye na Yule bibie........
DAH!
KWELI KUISHI KWINGI NI KUONA MENGI........