Kweli Mungu ni muweza wa yote?

Kweli Mungu ni muweza wa yote?

Soma hapo juu nilivyokujibu na nitarudia tena kukujibu.

Sheria ina-dictate whether "kitendo" fulani ni kibaya au la.

Kabla ya uwepo wa sheria, haimaanisha "kitendo" husika hakikuwepo.

Incest ilikuwepo kabla ya sheria. Kitendo cha watu kufanya mapenzi na ndugu wa damu kilikuwepo. Si sawa kusema sheria ndiyo inaanzisha incest. Kitendo cha incest ni independent na sheria.

Umeelewa?



Kasome ujue nini maana ya vitu hivyo.

Kuuliza nini inatofautisha kijani, nyekundu na manjano ni kuonyesha jinsi gani hujui.



Religious zealots are closed minded. You happen to be one. Hutaki kujifunza, unapiga kelele tu.



Sasa kama una majibu mbona unalalamika tunapouliza maswali?
Kiranga mpaka sasa hujamjibu swali lake, leave alone maswali mengine mnayoyakimbia.

Mfano nimekuuliza, Je kabla ya amri kumi za mungu kushushwa, kuua, kudharau wazazi, kuabudu miungu wengine ilikuwa ni sawa? Hujajibu. Hapa unasema umejibu kila kitu.

Si mnafundishwa kuwa wakweli nyie? Sasa uongo wa nini.

Kama sheria ndiyo indiketa ya kitendo kibaya , kabla ya sheria ulitumia nini kuona ubaya wa kitendo hicho ? Kitendo kinakuwepo lakini hakina alama ya kukitambulisha ubaya wake.
Kuwepo kwa kitendo na Sifa za kuwa kibaya ni vitu viwili tofauti.

Kitendo cha kuhusiana ndugu wa damu hakikuwa Incest kabla ya sharia iliyotambua kuwa kitendo hicho ni incest kuwepo. Wana wa kike na wana wa kiume wa Adamu hawakuwa wanatemda dhambi kuzaa watoto. Yule aliyeweka mechanism ya wao kuweza kuzaa hakuwa ameweka mipaka ya ndugu wa damu kwanza.
Kitendo cha kuhusiana wana wa Adam wa kike na wakiume hakijawahi kuitwa au kuwa incest. Toa ushahidi.

Hakukuwa hata na hekima ya kutambuana Kama kaka na dada ni ujinga wa hali ya juu kuimgiza incest zama ambazo hata kaka na dada hazikuwa terms za kuwarifaa watoto wa kike na wa kiume. Kiranga ametafuta uvungu kajichomeka na viroja vyake vya kipu.uzi huyo achana naye labda akajadili na walevi wa gongo ambao hawajielewi. Mwenyewe ameathiriwa na kariri.

Kabla ya sheria kuhusu kuua ni kwa namna gani kuuwa kunakuwa Kosa au dhambi ? Mbona hutaki kuelewa. Pasipo sheria urarumia nini kutambua kwamba kitu Fulani ni kosa ?
Niambie namna ninavyoweza kutambua kwamba kuua ni kosa pasipo sheria
Hayo ya kudharau wazazi, kuabudu miungu yote unatakiwa uniambie namna ambayo waweza kutambua kuwa kosa pasipo prescription.

Nani muongo na kaongopa nini ? Majibu haya haya nimekujibu post za nyuma tatzio.ni wewe tu.
 
Last edited by a moderator:
Una ushahidi wa kuthibitisha Mungu kamuumba Adam na Eva?

Na nani kamuumba mungu?



Hao watoto wa kiume na kike waliitwa nani na walikua wangapi?

Can you draw a family tree inayokufikia wewe? This is funny.

Hao watoto wa kiume walizaa na nani according to the bible not according to you.

Go read the bible, na uje hapa useme hao watoto wa kiume walizaa na nani. Utakuta something different if you look at the bible. I dare you to go find this one out.



Una ruhusa ya kuamini chochote. Hukatazwi.

Imani hiyo haimaanishi kitu hicho ni kweli.



Huo muongozo uliekwa lini? Simple question. No answer.



Sielewi ni lini mungu alieka muongozo wa kusema sasa binadamu humu ndani washatosha sasa kaka na dada wasifanye mapenzi ndiyo maana nakuuliza, huo muongozo uliekwa lini?

Pia sielewi ni jinsi gani dhambi inakuwa relative na kusema kwamba this is work of an intelligent designer.



Am out.

Ushahidi ni Mimi na wewe kuitwa binadam

Nani kakwambia Mungu aliumbwa hadi uulize nani kamuumba ?

Biblia iko wazi hata kwako kusoma utajua wana wa kiume na wa kike wa Adam na Eva waliotajwa na wasiotajwa majina.

Funniest part ni hoja ya memba ya JF kutaka apewe family tree toka Adam wakati yeye hata ya kizazi chake cha 4 ni kmtwisha gunia la misumari

Walizaa na watoto wa kike.

Nimeisoma hata concern yako nimeisoma. Alizaa watoto wa like ma wakiume wengi na aliisha mania ya miaka kwa hiyo watoto walisambaa mbali mbali.

Una ruhusa ya kuamini kwamba huamni chochote hukatazwi

Imani ya kutoamini chochote haimanishi hicho usichokiamini hakipo.

Huo mwongozo uliwekwa lini ni childish question kwa kuwa biblia iko wazi kusomwa hata na wasioamini chochote.

Wewe umejua lini kuwa incest ni dhambi na ulipata wapi hiyo prescription iliyo prescribe incest kuwa dhambi.
Nenda angalia prescription husika kupata unachohotaji. Inawezekana Una tatizo na ni mzito wa kuelewa jibidishe kusoma utaelewa hata Kama ni baada ya miaka 50.

Hakuna pahala nimeandika dhambi ni relative.
Tumezungumzia sheria kuanza lini. Sheria ikiwa effective imediatelly kosa huanza kutambulika kwa aliyekiuka sheria. Hili ni jambo dogo mno halihitaji hata cheti cha sheria kuelewa. Kitendo cha wewe kuwa binadam kamili kinatosha kuelewa hili.

Mmezoea miteremko na viroja vyenu. Bye
 
Kwanza ningependa nijue jinsi mnavyoweza kum-Quote mtu hoja kwa hoja ili nikujibu vizuri ila kwavile sijui nitajaribu kuyatenganisha majibu kwa aya.

Mungu alituumba kwa nia njema tuishi maisha yenye amani na yasiyo na kufa, shetani akaja akasema njia ya Mungu siyo sahihi njia yake yeye (shetani) ndiyo sahihi. Kumbuka wakati hayo yanatokea Malaika wengine walikuwa wakitazama. Mungu angeweza kumuangamiza shetani wakati uleule lakini wale Malaika wengine waliokuwa bado wako upande wa Mungu kama Mungu angetumia nguvu wangehisi njia ya Mungu kweli ina makosa ndo maana kamuangamiza shetani ili ukweli usijulikane.

Kwahiyo alichokifanya Mungu ni kumruhusu shetani aonyeshe njia yake yeye ili tujionee (wanadamu na malaika) ni nani aliyekuwa sahihi, Mungu au shetani. Na hadi Dunia ilipofikia leo hii ni wazi kabisa njia ya Mungu ndo ilikuwa sahihi. Wewe mwenyewe unalalamika Dunia ilivyo leo simply because njia ya shetani siyo sahihi, ile njia ya Mungu ndo ilikuwa sahihi. Kwahiyo baada ya kudhihirika njia sahihi wakati utafika Mungu atauondoa kabisa utawala wa shetani na tutaanza maisha mapya ya Dunia mpya.

Sikumfananisha Mungu na U.S.A. I was just trying to elaborate. Wote hapa tunafahamu U.S.A. ndiye police wa Dunia yetu kwasababu ya sababu zake inazozijua yenyewe. U.S.A. ingeweza kuamua isiwe police wa Dunia kama wangekuwa na sababu zao. Hali kadhalika kwa Mungu, aliamua kumuacha shetani atawale Dunia hii kwasababu alikuwa na sababu zake ambazo nimeshakuelezea.

Mkuu Kiranga, Mungu alishauumba huo ulimwengu usiyo na mabaya wala shetani. Shetani alikuja baadaye (maana ya neno shetani ni mpinzani) kwasababu Mungu alitupa uwezo wa kuchagua mazuri na mabaya. Shetani alikuwa ni malaika mwema hapo mwanzoni kabla hajaamua kuasi. Mungu hakutuumba kama robots/machines. Mungu siyo dictator.

Ahsante.

Hapana mkuu unakosea unaposema maana ya shetani ni upinzani.....iko hivi ushetani ni matendo i mean kiumbe chochote kikifanya matendo maovu ya kutisha tunasema ni ushetani ht binadamu anaweza kuwa shetani endapo atafanya hayo niliyokueleza.Na hakuna kiumbe mungu alichokiumba akakiita shetani huyo unahisi ni shetani anajina lake rejea kwenye vitabu vya dini utapata alikuwa akiitwa lucifer lakini baada ya kutenda uovu akaitw shetani amini ni mtenda maovu hapo utagundua ushetani ni matendo wala si kiumbe pia si mpinzani kama ulivyodai hapo awali.
 
Last edited by a moderator:
Wanaosema mungu yupo hawajathibitisha kwamba mungu yupo.

Na hawajajibubimekuwaje mungu mwenyebuwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaanua kuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.
 
Wanaosema mungu yupo hawajathibitisha kwamba mungu yupo.

Na hawajajibubimekuwaje mungu mwenyebuwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaanua kuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.

Edit kidogo mkuu, ...wakati aliweza...
Uandike ...alikuwa na uwezo au angeweza.
Ili Kariri yako isomeke na kueleweka.
 
Hujapata tafsiri ya maovu au unaiwekea makengeza tu hutaki kuisoma?

Sijakwambia kwamba katika ulimwengu ulioumbwa na mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote, kiumbe yoyote kupatwa na chochote asichokitaka na kukosa chochote anachokitaka ni uovu?

Sinakwambia kwa jibu lisilo mjadala wala milinganyo kwamba binadamu kuua wanyama katika ulimwengu huu ni uovu?

Unataka jibu gani zaidi?

Kwahiyo sie binadamu kuchinja wanyama na kuwafanya vitoweo nao pia ni uovu?
 
Uovu ni relative term kutegemea na mila, desturi na imani za jamii husika.

Unapouliza kama kuua wanyama ni uovu au si uovu, swali lako linakuwa vague.

As I have mentioned kwamba uovu ni relative, namaanisha kwamba kitendo cha kuua mnyama na kumla ni uovu au si uovu kutegemeana na jamii moja na nyingine.

Kwa mfano kwa mmasai hiyo si uovu. Ni mfumo wa maisha yao kula nyama.

Lakini kwa a Jainist monk, huo ni uovu kwani ni kinyume na imani yao.

Ndiyo maana nasema swali liko vague. Unapouliza kama ni uovu, you have to be specific. Je ni uovu with respect to what?

Kuna post mtu alisema kwamba incest ilikuwa si dhambi lakini leo ni dhambi. Hapo anaonyesha dhambi ya incest ni relative with time na mazingira and not absolute. This is a point that shows God is not intelligent in the first place.

Hii inaonyesha suala la "uovu" ni social construct. Jamii husika inaeka mila na desturi zake in place zinazosema jambo fulani ni uovu au si uovu. Si mungu.

Hivyo kitu kinapokuwa relative to that point, then in the real sense, it does not exist.

Mpaka sasa hatupewa jibu juu ya Problem of evil with respect to Nepal's earthquake.

Mnaruka na kukimbia maswali. Pope Francis alikua mkweli alipoulizwa hili swali akasema hajui. Hapa ni kurukaruka bila kutoa majibu.

Sasa ikiwa binadamu tunatofautiana kwenye kutambua ni lipi ovu na lipi si ovu,sasa mnaposema Mungu kaumba ulimwengu ambao unaruhusu maovu je,huwa mnatumia tafsiri ya maovu kwa Mila,desturi au imani ipi kuyatambua hayo maovu?
 
Mpaka sasa.

Hakuna aliyethibitisha kwamba mungu yupo.

Hakuna aliyefafanua imekuwaje mungu mwenyebuwezo wote, ujuzi wote na upendo wote akaumba ulimwengu ambao unaruhusu uovu.

Je, aliweza kuumba ulimwengu ambao haunanuovu ila hakutaka tu?

Kama aliweza kuumba ilimwengu huo na hakutaka tu, basi hana upendo wote.

Au alitaka kuumba ulimwengu huo ila hakuweza tu?

Kama alitaka ila hakuweza tu, basi huyo si muweza yote.

Mungu muweza yote, mjuzi wa yote ambaye hapo hapo kaishia kuumba ulimwengu huu wenye mabaya na maovu ni contradiction ambayo haijapatiwa ufumbuzi mpaka sasa.

Umejaribu kuonesha kuwa pengine mungu aweza akawa hana upendo au uwezo wote,lakini hayo yote yanategemea na huu ulimwengu ambao mungu anasema kauumba. Kwa maana kwamba ikiwa mungu hajaumba kweli huu ulimwengu suala la kuwa ana upendo au hana litakuwa halina maana,hivyo ikiwa kweli mungu kaumba huu ulimwengu basi hapo ndiyo italeta maana kujua kuwa mungu anao upendo na uwezo wote au hana.
 
Wanaosema mungu yupo hawajathibitisha kwamba mungu yupo.

Na hawajajibubimekuwaje mungu mwenyebuwezo wote, ujuzi wote na upendo wote kaanua kuumba ulimwengu ambao mabaya yanawezekana wakati aliweza kuumba ulimwengu ambao mabaya hayawezekani.

Ushahidi wenye kuthibitisha kuwa kweli hakuna Mungu hadi sasa hakuna,mmebaki tu mara mungu hana upendo mara hana uwezo wote sijui kwanini kaumba ulimwengu una maovu? Lakini hamtoi ushahidi wa kutokuwepo kwa Mungu.

Yapi yaliyokuwa yanakufanya useme mungu yupo kabla haujawa atheist?
 
Sasa ikiwa binadamu tunatofautiana kwenye kutambua ni lipi ovu na lipi si ovu,sasa mnaposema Mungu kaumba ulimwengu ambao unaruhusu maovu je,huwa mnatumia tafsiri ya maovu kwa Mila,desturi au imani ipi kuyatambua hayo maovu?

Earthquake inayouwa watoto na watu wengine ni jambo ovu. Cancer inayoua watu ni jambo ovu. What have these people done to deserve cancer or earthquake?

Kwa mfano uovu juu ya genocide in Rwanda ambavo watoto wanauliwa, famine Somalia watoto na wanawake wanakufa njaa, watoto kuzaliwa na cancer etc etc

Huo ni uovu in the context that, kama mungu alikua na uwezo wa kuzuia mtoto asizaliwe na cancer, au famine, au genocide, na ana mapenzi tele kwa nini hakuzuia?

Pia, uelewe unapokubaliana na mimi kwamba uovu ni relative basi unaondoa dhana nzima ya uwepo wa uovu na hii inapingana na dini. In other words, tunasema uovu unatokana tu na jamii na si vitabu vya dini.

Hapo ndiyo utagundua vitabu hivi viliandikwa kwa manufaa ya jamii fulani na si ulimwengu wote. Ni masimulizi tu ya jamii fulani. Mfano, mungu huyo anapomsaidia mfalme Daudi katika vita, unabaki kujiuliza kama mungu ni wa wote na kaumba vitu vyote kwa nini achukue upande kwenye vita?
 
Ushahidi wenye kuthibitisha kuwa kweli hakuna Mungu hadi sasa hakuna,mmebaki tu mara mungu hana upendo mara hana uwezo wote sijui kwanini kaumba ulimwengu una maovu? Lakini hamtoi ushahidi wa kutokuwepo kwa Mungu.

Yapi yaliyokuwa yanakufanya useme mungu yupo kabla haujawa atheist?

Wewe unayesema mungu yupo ni wapi umethibitisha uwepo wake?

Unaposhindwa kuthibitisha kwamba mungu yupo then kuna chances kwamba huyo mungu hayupo.

Suala la upendo na problem of evil linaonyesha logical contradictions katika sifa za huyo mungu. Logical contradiction inamaanisha hicho kitu ni uwongo.

Either hamtaki kuelewa au mnajifanya hamuelewi. Thibitisheni kwamba huyo mungu yupo. Au mmeshindwa?
 
Mi naamini Mungu yupo na yeye ndio Alpha na Omega,hakuanza wala hatakwisha. Uwepo wake ni wa milele.
 
Mi naamini Mungu yupo na yeye ndio Alpha na Omega,hakuanza wala hatakwisha. Uwepo wake ni wa milele.
Hili ni possible kweli ??? mana everything has started point as well finished point how come God awe ivo mbona hio concept yako ni differ sana
 
Kwahiyo sie binadamu kuchinja wanyama na kuwafanya vitoweo nao pia ni uovu?

Hili swali utaliuiza mara ngapi na unataka nikujibu mara ngapi?

Nataka uniambie namba ya mara unazotaka nilijibu ili nilimalize hapahapa.

Halafu, baada ya kulijibu, nikuulize, linahusika vipi na kithibitisha mungu yupo.
 
Umejaribu kuonesha kuwa pengine mungu aweza akawa hana upendo au uwezo wote,lakini hayo yote yanategemea na huu ulimwengu ambao mungu anasema kauumba. Kwa maana kwamba ikiwa mungu hajaumba kweli huu ulimwengu suala la kuwa ana upendo au hana litakuwa halina maana,hivyo ikiwa kweli mungu kaumba huu ulimwengu basi hapo ndiyo italeta maana kujua kuwa mungu anao upendo na uwezo wote au hana.

Unachosema ni nini hapo?

Mungu yupo lakini hajaumba ulimwengu?

Umekubali kwamba mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hawezi kuwa ameumba ulimwengu huu?

Unaondoa argumnt ya order katika ulimwengu kama moja ya ushahidi wa kuwepo mungu?
 
Ushahidi wenye kuthibitisha kuwa kweli hakuna Mungu hadi sasa hakuna,mmebaki tu mara mungu hana upendo mara hana uwezo wote sijui kwanini kaumba ulimwengu una maovu? Lakini hamtoi ushahidi wa kutokuwepo kwa Mungu.

Yapi yaliyokuwa yanakufanya useme mungu yupo kabla haujawa atheist?

First thing first get the basics right.

Ushahidi hauthibitishi, ushahidi unatoa ushahidi. Kinachothibitisha ni uthibitisho.

Kama huwezi kujua hilo, kujadili uwepo wa mungu ni kitu kikichokupita kimo.

Pili, kwa sababu suala hili limekupita kimo, hata ukipewa contradiction ambayo inaonyesha mungu hayupo, hutaielewa.

Kukuelewesha wewe hili jambo ni sawa na kumuelewesaha mbwa ku solve quadratic equation kwa general formula.
 
Unachosema ni nini hapo?

Mungu yupo lakini hajaumba ulimwengu?

Umekubali kwamba mungu mwenye uwezo wote, ujuzi wote na upendo wote hawezi kuwa ameumba ulimwengu huu?

Unaondoa argumnt ya order katika ulimwengu kama moja ya ushahidi wa kuwepo mungu?

Mungu ndiye aliyeumba Mbingu na nchi na kila kilichomo
 
Wanaosema mungu yupo hawajathibitisha kwamba yupo.

Na hawajaondoa contradiction ya "the problem of evil".
 
Back
Top Bottom