Mwanangu ndio katimiza miaka mitatu mwaka huu, kwa umri huo kweli anaweza kufanya kazi, labda kama ni wa kike lakini wa kwangu sijaona kama anamudu kufanya kazi zaidi ya kubadilisha channel za TV tu.
Jambo hili sio kwa mama wa kambo tu, hata mama wazazi huwatesa sana watoto zao utadhani hawakutoka mkatika matumbo, mie kule Kibaha nimeshuhudi mtoto alipoteza shilingi mia moja! lakini alichomwa mikono yote miwili kwa moto baada ya kufungwa na nailoni na kumwagiwa mafuta ya taa, yule mtoto alipoteza vidole vyake vyote, ilikuwa ni kwenye miaka ya mwanzoni mwa 90. jambo lile mpaka leo linaisumbua akili yangu.