Mara nyingi tulioolewa ndio wasababishaji kuwepo kwa nyumba ndogo. Hii inatokana na kujisahau wajibu wetu kwa mume.
Elimu na nafasi makazini zimechangia sana kujisahau. Unashindwa kunyenyekea maana una kipato sawa au wakati mwingine unamzidi mumeo. Hii inakujengea fikra potofu kua "hata mimi ninazo"
Kazi zako zote kwa mume anafanya dada. Uko busy pia. Baba akikosa attention yako obvious atatoka nje kufuata attention. Nyumba ndogo ikigundua hilo ni full kujitoa!
Wanaume ni kama watoto, kitu kidogo sana chaweza kumkimbiza au kumrudisha kwake, walioolewa tuwe waangalifu kwenye hili.
Degree yako na cheo chako acha getini kwako, ukiingia ndani vaa joho la mke wa kaizer. Utaweza. Hata kaizer akienda, hataweka makazi.
Ni hulka zao, kua lazima waonje onje kila kipitacho, haimaanishi hakupendi. Ila ukizembea, atapenda kule zaidi