Kwenu wazazi mnaosomesha Watoto, Msisitize watoto wasomee Udaktari, Sheria, Engineer ama Uhasibu. Soko la ajira ni gumu ila huku kuna Nafuu

Kwenu wazazi mnaosomesha Watoto, Msisitize watoto wasomee Udaktari, Sheria, Engineer ama Uhasibu. Soko la ajira ni gumu ila huku kuna Nafuu

Makumbusho na Kariakoo zimejaza wauza simu wengi wenye MD zao na ajira hawajapata sijui nani anapata audacity ya kumshawishi mtu asome kitu fulani sababu kuna ajira ya uhakika. Msimamo wangu kwa wanaosoma ni huu:

1. Soma kitu unachoweza. Usisome kitu kigumu kisa umaarufu au kuonekana gangwe, utatumia gharama nyingi, muda mwingi na uwe average tu kwenye industry. Utakuwa yule daktari anafanya kazi hospitali ya serikali tu hana vituo vya pembeni sababu ni very average kwenye competitive market.

2. Soma unachopenda na uwe na vision nacho. Ukipenda kitu unakifanya kwa ufanisi zaidi, unafaulu kirahisi na unajua potentials zake, future yake, vitu visivyoonekana kwa wengine. Passion ni muhimu kuliko kulazimisha. Usifuate ndoto za wazazi. Mzazi unakuta alitamani awe Engineer masomo yakampiga sasa analazimisha uwe Engineer wakati uwezo huna, mzazi anataka cheo cha kutamkika akatambe kwenye jumuiya wakati wewe ni matter of life. Unless huyo mzazi ni 'muelewa' wa situation ilivyo na atachangia kukua kwako, kama yuko sekta fulani akikushawishi basi anamaanisha.

3. Soma kitu ukijua kuna kuajiriwa au kutoajiriwa. Ukisoma kwa kutegemea kuajiriwa ndio yaleyale ya Petroleum Engineering mtu ana ufaulu wa juu sana ila ana njaa mfukoni kisa hakuna ajira. Mtu aliyesoma Accounting ana uwezo mkubwa sana kujiajiri kuliko aliyesoma Pharmacy. Nina jamaa yangu alisoma Accounting akaiva akaenda kwa ndugu yake nani uko kufundishwa Auditing na vitu vya hivyo, anapiga Audit ya mtaani na anaenda ofisi kwa ndugu yake yuko certified kuchukua mhuri na saini. Hela nyingi anapata (mfano una kampuni uchwara zile mnafungua kwa kiherehere haijauza nusu mwaka unataka kufile tax ile kitendo cha kuthibitisha hujauza kitu unamlipa sijui 50,000 sijui 30,000), yeye alikosa kazi akaamua aongeze skills chache kwenye fani yake. Sasa Pharmacist ukikosa kazi utauza dawa za kienyeji kama application ya ulichosoma?
Mtaji wa kufungua Pharmacy ni mkubwa, huyo jamaa alianzia ghetto kwake na meza, kiti na laptop na vitabu vyao.

4. Usisome kitu kimoja kama unatafuta ufalme wa mbinguni. Soma alafu kuwa na skill nyingine kama graphics, photography, drawing, beautician kama ni mtoto wa kike, n.k. Nina mate wangu alisoma diploma ya Engineering ila ni DJ na analipwa vizuri kwenye u-DJ kuliko kwenye kulishwa vumbi uko kwa mafundi mchundo, na anafanya kazi sehemu nyingi. Side hustle inakusaidia kupata hela wakati umekosa ajira mwanzoni na inakusaidia ukiwa kwenye ajira vilevile. Hata ukipata hela unajua business gani ufanye, kama ni binti anajua ususi akienda kwenye ajira akapata hela anajua mtaji kiasi gani ananunua nini na nini anaanzisha kiofisi anaweka mtu.

N.B: Wakati namaliza chuo Magufuli alishafariki. Ushauri wangu 'ni wa kisasa' unaendana na mazingira ya sasa.
Ushauri kuntu huu....ukisoma kitu una passion nacho masomo yanakua marahisi, hata uki graduate unakua na confidence ya ku practice ulichosomea...sio kuchagua course ngumu,kila siku una sup unagraduate kwa mbinde, hata confidence inashuka, na wale graduates wanaoajiriwa huko makazini halafu wako incompetent ukiangalia kwa makini sababu ni hii ya kulazimisha kusoma kitu hauna interest nacho....

Mimi ningependa kuona mwanafunzi kuanzia mwaka wa kwanza anapata sehemu ya kujishikiza hata kwa masaa mawili kwenye shirika ambalo linatoa ujuzi unaoendana na fani anayosomea, hii inasaidia kumfanya mwanafunzi ajue what to expect mtaani, opportunities,akazanie nini kwenye course yake ambacho kinaendana na demand mtaani, inakua kama feedback system, experience kazini ina consolidate anachosomea mwanafunzi, na akitoka darasani analeta new ideas kazini...akitoka hapo ana Experience + Knowledge + Confidence...graduate anakua ameiva...
 
unapotosha watu mkuu, vitu kama hivi kama huhusiki na kada ni bora unyamaze
Yupo sahihi Computer Engineering ni ina-deal na Electronics zaidi unacheza sana na ma-hardware kufumuafumua mavifaa ya Computer na kufanya marekebisho, HESABU za kufa mtu km hupendi HESABU achana nayo soma tu CS utengeneze ChatGPT ya kwako basi
 
Mimi ningependa kuona mwanafunzi kuanzia mwaka wa kwanza anapata sehemu ya kujishikiza hata kwa masaa mawili kwenye shirika ambalo linatoa ujuzi unaoendana na fani anayosomea, hii inasaidia kumfanya mwanafunzi ajue what to expect mtaani, opportunities,akazanie nini kwenye course yake ambacho kinaendana na demand mtaani, inakua kama feedback system, experience kazini ina consolidate anachosomea mwanafunzi, na akitoka darasani analeta new ideas kazini...akitoka hapo ana Experience + Knowledge + Confidence...graduate anakua ameiva...
Hii wapo wanaofanya Ila ni wale wenye CONNECTION TU
 
Hao computer science hawawezi kuwa hata fundi TV ama simu mtaani ndio uwalinganishe na computer engineering ? upo serious wewe ?
Una point Ila uwasilishaji wako tu ndio una tatizo

Computer Engineering na Computer Science vinategemeana Ila Computer Engineering ni zaidi ya Computer Science kwenye masuala ya Electronics & Hardware's tu Ila vingine vyote ni sawa ingawa soko la ajira linawahitaji sana wale waliosomea Computer Science
 
Computer science ndio yenye ajira nyingi na ndio nzuri zaidi
Zote zina Ajira Computer Science & Computer Engineering utofauti ni mmoja ata-deal na hardware's (CE) na mwingine ata-deal na softwares (CS),

Ingawa aliesoma Computer Engineering anaweza kufanya kazi za mtu aliesomea Computer science Ila aliesoma Computer Science hawezi kufanya baadhi ya kazi za mtu aliesoma Computer Engineering

Kwa hio ukiangalia hapo mwenyewe utaona mwenye wigo mpana ni yule aliesomea Computer Engineering
 
Doctor, engineer au Lawyer ikishindikana angalau somea uhasibu.

Niseme tu ya kwamba wapo wanaosomea hata degree ya kifaransa wanapata ajira hapahapa Tanzania lakini Probability (makadirio ya uwezekano) ya kupata hizo kazi ni ndogo.

Lakini hizi kozi tajwa angalau zina Probability (makadirio ya uwezekano) nzuri ya kuajiriwa sambamba na malipo mazuri, vijana wengi tu wapo makazini kwenye hizi kazi na hali zao kiuchumi si haba. Haimaanishi kwamba wooooote wanaajiriwa ama kujiajiri, LA HASHA!! wengine wanasugua benchi mtaani lakini kozi hizi angalau zina nafuu kwenye Probability (makadirio ya uwezekano) ya kuajiriwa ama kujiajiri, Mambo hayana formula lakini ni vema kufanya kitu walau kina Probability (makadirio ya uwezekano) nzuri, hata kwenye muziki yupo Diamond platnumz lakini probability ya mtu aliemaliza form 4 aanze kuimba ategemee muziki pekee kuendesha maisha ni ndogo sana, ni heri adungue mgahawa wake angalau kuna Probability nzuri ya uhakika wa kuendesha maisha yake.

Madaktari wana bodi yao Medical Council of Tanganyika, jina la daktari linaanza kwa Md flani. Afya ndio mtaji jamani, Uhitaji wao ni mkubwa, mishahara yao si haba, na mtu akiweza kujiajiri afungue hata sehemu yake kama zahahanati ni jambo la neema kwa jamii maana huduma za afya bado zipo chache.

Engineers wana bodi yao, Engineers Registration Board, jina la daktari linaanza kwa Eng, flani. hawa ndio mafundi mitambo, wahandisi wa barabara, wanaojenga majengo, wahandisi wa computer, n.k. huku waliojaa wengi ni wanaume tofauti na kwengine, kwa wanawake nadhani huwa wanapata upendeleo maalum kwenya ajira.

wanasheria wana bodi yao, Tanganyika law society, jina la daktari linaanza kwa wakili flani. hapa wapo wale mapilato wanaotembelea gari zimeandikwa J, wapo washauri wa sheria wa kulipwa, wapo mawakili, wapo wenye law firms zao, n.k. asikwambie mtu yani watu wapo tayari kutoa chochote kukwepa maisha nyuma ya nondo, kudai haki zao, kujitetea, n.k. wanasheria ndio wanufaika hapa.

wahasibu wana bodi yao, National Business Aviation Association, jina la daktari linaanza kwa Cpa flani. ndio wanaohusika na usimamizi wa fedha kuanzia mapato, matumizi, faida , n.k. wapo kwa wingi karibu kila shirika maana pesa bila usimamizi ni hatari, kwa cpa kima cha chini cha mshahara inasemekana ni milioni 1.3, kwenye kujiajiri kuna accounting firms hawa ndio wanahusika na kusimamia hesabu za makampuni, kusaidia watu kupeleka tax returns TRA, n.k. pesa ipo.

Ni kipimo cha kuonyesha uzito wa haya mambo, bodi hizi zipo tangu zamani na ili uwe mwanachama inabidi ufanye mitihani yao.

Pia ni inapendeza kuanza kusomea taaluma mapema vyuoni baada ya kuhitimu form 4, diploma miaka mitatu kisha unaingia degree pamoja na wale waliotokea sekondari form 6, kumbuka form 6 ni elimu ya sekondari wala sio elimu ya taaluma ndio maana mtu aliesoma form hawezi kuajiriwa bila degree lakini mwenye Diploma anaweza kupata ajira bila degree, Pia kazi za degree ni za wote waliotokea form 6 kwenda degree na wale form 4>diploma>degree lakini kazi za diploma ni maalum kwajili ya walioanza kusoma chuo baada ya form 4, nchi zilizoendelea kama Kenya walishafuta form 5 na 6 ni moja kwa moja kuanza kusomea taaluma chuoni.

Wanaijeria ndio jamii ya waafrika walioelimika zaidi wanasisistiza watoto wao wasomee Doctor, Lawyer ama Engineer, waisrael na wahindi ndio makundi yenye wasomi zaidi wanasisitiza watoto wao wasomee Doctor, engineer ama Lawyer, hio accountant.

Nliisha acha kuwashauri wath wasome nini
Baada ya kugundua mtaji ni watu sio taaluma

Soma chochote hakikisha una watu basi
 
Computer engineering ina soko kubwa zaidi, ndio kozi baba kwenye mambo ya computer ikifuatiwa na hizo zingine.

Compuuterengineer anaweza kuwa fundi mitambo pia kwenye hardware, ama hata fundi wa simu na laptops upande wa software na hardware.
Wewe unaongea kitu usichokijua
 
Doctor, engineer au Lawyer ikishindikana angalau somea uhasibu.

Niseme tu ya kwamba wapo wanaosomea hata degree ya kifaransa wanapata ajira hapahapa Tanzania lakini Probability (makadirio ya uwezekano) ya kupata hizo kazi ni ndogo.

Lakini hizi kozi tajwa angalau zina Probability (makadirio ya uwezekano) nzuri ya kuajiriwa sambamba na malipo mazuri, vijana wengi tu wapo makazini kwenye hizi kazi na hali zao kiuchumi si haba. Haimaanishi kwamba wooooote wanaajiriwa ama kujiajiri, LA HASHA!! wengine wanasugua benchi mtaani lakini kozi hizi angalau zina nafuu kwenye Probability (makadirio ya uwezekano) ya kuajiriwa ama kujiajiri, Mambo hayana formula lakini ni vema kufanya kitu walau kina Probability (makadirio ya uwezekano) nzuri, hata kwenye muziki yupo Diamond platnumz lakini probability ya mtu aliemaliza form 4 aanze kuimba ategemee muziki pekee kuendesha maisha ni ndogo sana, ni heri adungue mgahawa wake angalau kuna Probability nzuri ya uhakika wa kuendesha maisha yake.

Madaktari wana bodi yao Medical Council of Tanganyika, jina la daktari linaanza kwa Md flani. Afya ndio mtaji jamani, Uhitaji wao ni mkubwa, mishahara yao si haba, na mtu akiweza kujiajiri afungue hata sehemu yake kama zahahanati ni jambo la neema kwa jamii maana huduma za afya bado zipo chache.

Engineers wana bodi yao, Engineers Registration Board, jina la daktari linaanza kwa Eng, flani. hawa ndio mafundi mitambo, wahandisi wa barabara, wanaojenga majengo, wahandisi wa computer, n.k. huku waliojaa wengi ni wanaume tofauti na kwengine, kwa wanawake nadhani huwa wanapata upendeleo maalum kwenya ajira.

wanasheria wana bodi yao, Tanganyika law society, jina la daktari linaanza kwa wakili flani. hapa wapo wale mapilato wanaotembelea gari zimeandikwa J, wapo washauri wa sheria wa kulipwa, wapo mawakili, wapo wenye law firms zao, n.k. asikwambie mtu yani watu wapo tayari kutoa chochote kukwepa maisha nyuma ya nondo, kudai haki zao, kujitetea, n.k. wanasheria ndio wanufaika hapa.

wahasibu wana bodi yao, National Business Aviation Association, jina la daktari linaanza kwa Cpa flani. ndio wanaohusika na usimamizi wa fedha kuanzia mapato, matumizi, faida , n.k. wapo kwa wingi karibu kila shirika maana pesa bila usimamizi ni hatari, kwa cpa kima cha chini cha mshahara inasemekana ni milioni 1.3, kwenye kujiajiri kuna accounting firms hawa ndio wanahusika na kusimamia hesabu za makampuni, kusaidia watu kupeleka tax returns TRA, n.k. pesa ipo.

Ni kipimo cha kuonyesha uzito wa haya mambo, bodi hizi zipo tangu zamani na ili uwe mwanachama inabidi ufanye mitihani yao.

Pia ni inapendeza kuanza kusomea taaluma mapema vyuoni baada ya kuhitimu form 4, diploma miaka mitatu kisha unaingia degree pamoja na wale waliotokea sekondari form 6, kumbuka form 6 ni elimu ya sekondari wala sio elimu ya taaluma ndio maana mtu aliesoma form hawezi kuajiriwa bila degree lakini mwenye Diploma anaweza kupata ajira bila degree, Pia kazi za degree ni za wote waliotokea form 6 kwenda degree na wale form 4>diploma>degree lakini kazi za diploma ni maalum kwajili ya walioanza kusoma chuo baada ya form 4, nchi zilizoendelea kama Kenya walishafuta form 5 na 6 ni moja kwa moja kuanza kusomea taaluma chuoni.

Wanaijeria ndio jamii ya waafrika walioelimika zaidi wanasisistiza watoto wao wasomee Doctor, Lawyer ama Engineer, waisrael na wahindi ndio makundi yenye wasomi zaidi wanasisitiza watoto wao wasomee Doctor, engineer ama Lawyer, hio accountant.
Sheria hakuna kitu
 
Kwanini kuzamia kwenye statistics na computer science/IT?


Sent using Jamii Forums mobile app
Computer Science ni field pana ajabu!

Msingi wa mafanikio ya hii field ni Statistics maana the now and future is all about data. Data bila statistics haziendi.

Ukiniuliza kuhusu statistics, nitakwambia unapaswa kujua mean, mode and median. Mengine yote yanaanzia hapa (hasa kwenye mean).

Well, anayesoma Computer Science leo hii bila kufikiria habari za data modeling aka machine learning ambayo msingi wake ni statistics hana budi kutafakari upya mtazamo wake.

Hivyo basi, statistics adds an edge to computer Science candidate. Bila in-depth statistics - yaani candidate asome HTML,CSS na JavaScript - hela iko ila sio kihiivyo.

Chaguo ni lako mkuu!
 
Computer Science ni field pana ajabu!

Msingi wa mafanikio ya hii field ni Statistics maana the now and future is all about data. Data bila statistics haziendi.

Ukiniuliza kuhusu statistics, nitakwambia unapaswa kujua mean, mode and median. Mengine yote yanaanzia hapa (hasa kwenye mean).

Well, anayesoma Computer Science leo hii bila kufikiria habari za data modeling aka machine learning ambayo msingi wake ni statistics hana budi kutafakari upya mtazamo wake.

Hivyo basi, statistics adds an edge to computer Science candidate. Bila in-depth statistics - yaani candidate asome HTML,CSS na JavaScript - hela iko ila sio kihiivyo.

Chaguo ni lako mkuu!
In short computer science ni tawi la hesabu
 
Back
Top Bottom