Kwenye chaka la vyama vingi kumejaa nguchiro wengi, kuwa makini

Kwenye chaka la vyama vingi kumejaa nguchiro wengi, kuwa makini

kavulata

JF-Expert Member
Joined
Aug 2, 2012
Posts
13,778
Reaction score
14,214
Hata tufanyeje lazima tufanane na wazungu kwenye siasa za vyama vingi. Aina hii ya siasa ililetwa kwetu na wazungu kwakuwa wana kazi nayo, lakini vyama na wanasiasa waliopigania uhuru waliikubali aina hii ya siasa kwa shingo upande kwa kulazimishwa.

Wakati wazungu wanaileta kwetu aina hii ya demokrasia walijuwa kuwa watawala wetu hawataikubali aina hii ya siasa, hivyo kwa vyovyote vile mabeberu watapata kundi la kuunga mkono ili wakati wakigombana wenyewe kwa wenyewe wao wnapata namna ya kutia mkono kwenye bakuli la rasilimali zetu.

Ndiyo maana nchi zote za Kiafrika zenye utajiri mwingi wa mafuta, madini, mbao hazifaidi mali zao hizo badala yake wanaofaidi ni wazungu kwa kupitia kundi linalokandamizwa na watawala. Na hakuna mtawala wala serikali inayoweza kuzuia hili lisitokee. Mfano, Uganda kuko shwari sasa hivi lakini subirini waanze kuyachimba mafuta yao muone timbwilitimbwili lao.

Dawa pekee ya kuzuia hili ni kuukumbatia utanzania wetu, utu wetu na tunu zetu ili zitusaidie wote kumuona, kumchukia na kupambana na adui wa nje tu na vibaraka wao. Na njia pekee ni kutengezena katiba na tume ya uchaguzi imara inayokubalika na wengi, kuendesha uchaguzi wa haki na wazi, kujali maisha na uhai ya kila mtanzania na kuunda taasisi imara za kuilinda katiba yetu. Hii itasaidia kupunguza mianya wanayotumia mabeberu kujipenyeza kwenye mataifa yenye rasilimali nyingi.

Hali ilivyo leo sio nzuri, mabeberu hawapati shida kupata watu wa kuwatumia kuingia Tanzania.

Mwafaka wa kitaifa ni kipaumbele kuliko ziara za mataifa jirani.
 
Nguchiro CCM, wako madarakani tangu Uhuru, rasilimali zetu zinawafaidisha wazungu na wahindi.

Mgodi wa Williamson Mwadui , Shinyanga ulikuwa haulipi Kodi kabisa.

Aga Khan Foundation na biashara zao zote kubwa walikuwa hawalipi Kodi kabisa, CHADEMA haihusiki na ubaradhuli huu.

Migodi ya uchimbaji dhahabu imeanza kulipa Kodi juzi.
 
Mtazamo wako ila kwa ulimwengu ulistaarabika hiyo ndio njia sahihi.
 
Mama wapambe nuksi, ulivyowaacha kwenye nafasi zao wamekuona dhaifu wameanza kukuharibia wachukue nafasi yako.

Suka upya Baraza la mawaziri na taasisi nyeti urudishe nidhamu kwa taasisi ya urais.

Haiwezekani umekataza watu kubambikiwa kesi halafu bado wanatekwa na kumbakiwa kesi.

Ulisema ukikuta bango sehemu unaondoka na mteule wako, bado tunateswa kwa kubeba mabango.

Kubali uchukiwe na wachache upendwe na wengi.
 
Nguchilo CCM, wako madarakani tangu Uhuru, rasilimali zetu zinawafaidisha wazungu na wahindi.

Mgodi wa Williamson Mwadui , Shinyanga ulikuwa haulipi Kodi kabisa.

Aga Khan Foundation na biashara zao zote kubwa walikuwa hawalipi Kodi kabisa, CHADEMA haihusiki na ubaradhuli huu.

Migodi ya uchimbaji dhahabu imeanza kulipa Kodi juzi.
Nguchilo wa kisiasa ni wale wanaowazunguuka watawala, hawa wanaweza kuua mtanzania mwenzao bila hata watawala kuwa na habari. Mtu yuko tayari kufanya lolote ilimladi chama kiende ikulu na ikiwezekana milele kwakuwa maisha yake yatategemea kama chama kitakwenda ikulu
Mama wapambe nuksi, ulivyowaacha kwenye nafasi zao wamekuona dhaifu wameanza kukuharibia wachukue nafasi yako.

Suka upya Baraza la mawaziri na taasisi nyeti urudishe nidhamu kwa taasisi ya urais.

Haiwezekani umekataza watu kubambikiwa kesi halafu bado wanatekwa na kumbakiwa kesi.

Ulisema ukikuta bango sehemu unaondoka na mteule wako, bado tunateswa kwa kubeba mabango.

Kubali uchukiwe na wachache upendwe na wengi.
Ni heri ya kiongozi ambae anabaki kimya kuliko anayetoa maagizo yasiyotekelezwa.
 
Hata tufanyeje lazima tufanane na wazungu kwenye siasa za vyama vingi. Aina hii ya siasa ililetwa kwetu na wazungu kwakuwa wana kazi nayo, lakini vyama na wanasiasa waliopigania uhuru waliikubali aina hii ya siasa kwa shingo upande kwa kulazimishwa.

Wakati wazungu wanaileta kwetu aina hii ya demokrasia walijuwa kuwa watawala wetu hawataikubali aina hii ya siasa, hivyo kwa vyovyote vile mabeberu watapata kundi la kuunga mkono ili wakati wakigombana wenyewe kwa wenyewe wao wnapata namna ya kutia mkono kwenye bakuli la rasilimali zetu.

Ndiyo maana nchi zote za Kiafrika zenye utajiri mwingi wa mafuta, madini, mbao hazifaidi mali zao hizo badala yake wanaofaidi ni wazungu kwa kupitia kundi linalokandamizwa na watawala. Na hakuna mtawala wala serikali inayoweza kuzuia hili lisitokee. Mfano, Uganda kuko shwari sasa hivi lakini subirini waanze kuyachimba mafuta yao muone timbwilitimbwili lao.

Dawa pekee ya kuzuia hili ni kuukumbatia utanzania wetu, utu wetu na tunu zetu ili zitusaidie wote kumuona, kumchukia na kupambana na adui wa nje tu na vibaraka wao. Na njia pekee ni kutengezena katiba na tume ya uchaguzi imara inayokubalika na wengi, kuendesha uchaguzi wa haki na wazi, kujali maisha na uhai ya kila mtanzania na kuunda taasisi imara za kuilinda katiba yetu. Hii itasaidia kupunguza mianya wanayotumia mabeberu kujipenyeza kwenye mataifa yenye rasilimali nyingi.

Hali ilivyo leo sio nzuri, mabeberu hawapati shida kupata watu wa kuwatumia kuingia Tanzania.

Mwafaka wa kitaifa ni kipaumbele kuliko ziara za mataifa jirani.
Huo ndio ukweli ndugu yangu
 
Mama wapambe nuksi, ulivyowaacha kwenye nafasi zao wamekuona dhaifu wameanza kukuharibia wachukue nafasi yako.

Suka upya Baraza la mawaziri na taasisi nyeti urudishe nidhamu kwa taasisi ya urais.

Haiwezekani umekataza watu kubambikiwa kesi halafu bado wanatekwa na kumbakiwa kesi.

Ulisema ukikuta bango sehemu unaondoka na mteule wako, bado tunateswa kwa kubeba mabango.

Kubali uchukiwe na wachache upendwe na wengi.
Mama ni wale wale tu
 
Mama ni wale wale tu
Dhambi ya kutesa, kunyanyasa, kusumbua na kuua watu wako mwenyewe haitakuacha wewe, uzao na wanaokuzunguuka salama, it is just a matter of time. Kama mioyoni mwetu tutaifanya Ikulu yetu iwe ni ya watu wa aina fulani tu, Wallah furaha zetu na mipango yetu vitakuwa ni kubahatisha tu. Hakuna watu serious wenye mitaji serious wanaopenda kufanya biashara serious kwenye taifa ambalo haliko serious na amani. Tunawekeza sana kwenye utulivu balada ya AMANI.

Kama nchi ina Katiba madhubuti na taasisi madhubuti za kuilinda Katiba kuna uharamu gani matakwa ya wananchi kwenye chaguzi zetu yakapewa kipaumbele? Hakuna ujanja ujanja wa milele, hata wasomi wetu ambao ni waoga kuliko raia wa kawaida wanalifahamu hili. Binadamu ana tabia ya kukinai kitu hata kama kiwe kizuri vipi, na anapokinai haimaanishi hakitaki tena. Watu wanakinai biriani, nyama ya kuku wa kienyeji, ugali, ndizi za kila siku asubuhi, mchana, jioni sembuse chama kikutawale kwa miaka 60 mfululizo?.

Kwa roho moja tuache vyama vipishane Ikulu kwa amani na uwazi kama wananchi ndivyo wanavyotaka. Hii itapunguza nguvu za wakoloni wetu wa zamani na hila zao. Kosa la Gadafi lilikuwa kutouzingatia ukweli huu wa wananchi kuchoka hata kizuri pamoja na mazuri yake kwa wananchi wako. Binadamu anataka mabadiliko ingawa kasi na namna ya kuyaendea mabadiliko inatofatiana kati ya mtu na mtu na jamii na jamii, hata hivyo hakuna mzuiaji wa mabadiliko, usipoyaratibu wewe yatatokea yenyewe. Variety is the spice of life.
 
Kundi la watanzania ambao wanaiangusha nchi hii ni kundi la wasomi. Kaka wasomi wetu ni watazamaji (on lookers) tu wa mambo, wanalinda wasichokuwanacho, wameingiza vichwa vyao kwenye makwapa yao kunusa harufu za makwapa yao, eti wanalinda vimishahara vyao na kuiacha kazi ya kuilingania demokrasia mikononi mwa akina Zitto, Mbatia, Mbowe na vijana wengine wa kawaida ambao ni rahisi kufinyangwafinyangwa hata kwa kutumia manati tu ya kawaida. Mshahara wa prof wa Kenya ni mara 6 ya mshahara wa prof wetu kwakuwa prof wa kenya anaweza kusema wewe unaiba mali ya umma basi na mimi niongeze mshahara kama sivyo namimi sifanyi kazi zako au nitakupeleka mahakamani. Hii ni kwasababu elimu yetu haitoshi, hata prof hawezi kujiajili mwenyewe.

Wa
 
Dhambi ya kutesa, kunyanyasa, kusumbua na kuua watu wako mwenyewe haitakuacha wewe, uzao na wanaokuzunguuka salama, it is just a matter of time. Kama mioyoni mwetu tutaifanya Ikulu yetu iwe ni ya watu wa aina fulani tu, Wallah furaha zetu na mipango yetu vitakuwa ni kubahatisha tu. Hakuna watu serious wenye mitaji serious wanaopenda kufanya biashara serious kwenye taifa ambalo haliko serious na amani. Tunawekeza sana kwenye utulivu balada ya AMANI.

Kama nchi ina Katiba madhubuti na taasisi madhubuti za kuilinda Katiba kuna uharamu gani matakwa ya wananchi kwenye chaguzi zetu yakapewa kipaumbele? Hakuna ujanja ujanja wa milele, hata wasomi wetu ambao ni waoga kuliko raia wa kawaida wanalifahamu hili. Binadamu ana tabia ya kukinai kitu hata kama kiwe kizuri vipi, na anapokinai haimaanishi hakitaki tena. Watu wanakinai biriani, nyama ya kuku wa kienyeji, ugali, ndizi za kila siku asubuhi, mchana, jioni sembuse chama kikutawale kwa miaka 60 mfululizo?.

Kwa roho moja tuache vyama vipishane Ikulu kwa amani na uwazi kama wananchi ndivyo wanavyotaka. Hii itapunguza nguvu za wakoloni wetu wa zamani na hila zao. Kosa la Gadafi lilikuwa kutouzingatia ukweli huu wa wananchi kuchoka hata kizuri pamoja na mazuri yake kwa wananchi wako. Binadamu anataka mabadiliko ingawa kasi na namna ya kuyaendea mabadiliko inatofatiana kati ya mtu na mtu na jamii na jamii, hata hivyo hakuna mzuiaji wa mabadiliko, usipoyaratibu wewe yatatokea yenyewe. Variety is the spice of life.
You are very correct. Dr Antony Diallo alimuuliza Kassimu Majaliwa" Mh Una Raha gani unatembea umezungukwa na bunduki zaidi ya 20"? Akaongeza kuwa hayo maisha ya wasi wasi mnayatengeneza wenyewe.
 
Kundi la watanzania ambao wanaiangusha nchi hii ni kundi la wasomi. Kaka wasomi wetu ni watazamaji (on lookers) tu wa mambo, wanalinda wasichokuwanacho, wameingiza vichwa vyao kwenye makwapa yao kunusa harufu za makwapa yao, eti wanalinda vimishahara vyao na kuiacha kazi ya kuilingania demokrasia mikononi mwa akina Zitto, Mbatia, Mbowe na vijana wengine wa kawaida ambao ni rahisi kufinyangwafinyangwa hata kwa kutumia manati tu ya kawaida. Mshahara wa prof wa Kenya ni mara 6 ya mshahara wa prof wetu kwakuwa prof wa kenya anaweza kusema wewe unaiba mali ya umma basi na mimi niongeze mshahara kama sivyo namimi sifanyi kazi zako au nitakupeleka mahakamani. Hii ni kwasababu elimu yetu haitoshi, hata prof hawezi kujiajili mwenyewe.

Wa
Wasomi wetu wana reflect ule tabia ya kiafrika ya ubinafsi. Yaani yeye akishakuwa analipwa huo mshahara ya 5M na malupulupu kibao. Basi habari zingine kuhusu watanzania wengine hana tena.
 
Ujinga wa mtanzania masikini ndiyo chanzo cha yote haya.
Maskini tutawasingizia tu hata wale wanaoibuka na kupata pesa na vyeo wanasahau tena hao maskini. Wasomi nao wameingia mtegoni. Akishapata hiyo masters basi hata kukosoa maovu anaachana nayo kisa asije akawaudhi wateuaji. Yaani ni njaa kwa kwenda mbele hujui maskini ni yupi na tajiri ni tupi
 
Wasomi wetu wana reflect ule tabia ya kiafrika ya ubinafsi. Yaani yeye akishakuwa analipwa huo mshahara ya 5M na malupulupu kibao. Basi habari zingine kuhusu watanzania wengine hana tena.
Wakishastaafu na kuacha kazi na kipato kupungua wanakumbana na upuuzi wao waliofanya wakati wana madaraka, Wana sauti, na wana nguvu za kurekebisha sera ili ziwafae wote badala ya kwenda kijijini na zawadi za sukari na mikate. Na wao wanapiga kelele kuhusu kikokotoo kama wengine ambao hawakuwa na sauti.

Wengine wanarudi kuomba kazi tena za kuendelea kuajiriwa.
 
Maskini tutawasingizia tu hata wale wanaoibuka na kupata pesa na vyeo wanasahau tena hao maskini. Wasomi nao wameingia mtegoni. Akishapata hiyo masters basi hata kukosoa maovu anaachana nayo kisa asije akawaudhi wateuaji. Yaani ni njaa kwa kwenda mbele hujui maskini ni yupi na tajiri ni tupi
Siku hizi hata waandishi wa habari na watangazaji wametiwa kigugumizi.
 
Back
Top Bottom