Nashengena
JF-Expert Member
- Apr 20, 2013
- 2,913
- 5,318
Muache tu aandike atakavyo, lakini sheria ya mirathi itaamua mgawanyo wa mali. Na iwapo mume amekufa, atapata 1/3 ya malz zake na iliyobaki inaenda kwa watoto , hii ni kama mtatumia sheria ya kiserikali. Yeye akifariki mume atarithi pamoja na watoto. Kama ni muislam safi inaweza kugawanywa kwa kutumia sheria za kiislam, au kama mnafuata mila sana zitagawanywa kutokana na mila husika. Hayo makaratasi ya kazini wala usihangaike nayo sana.Simple. Mwambie kwa lugha nzuri tu na wewe waenda kuhuisha tena taarifa hixo na kumuondoa yeye kama mrithi na kumweka baba yako na watoto.
Hapa tunahitaji tume ya uchunguziNiliishuhudia hii kazini kila mtu kaandika mrithi ni mtoto, nilikua mmoja wa wachache sana kumuandika mme kwakweli mme atembee kifua mbere
Nilikuwa nimemwambia Maxecence Melo usipo-comment kwenye hii post anifute JF permanentlyDaaah hii comment tuiwekee lamination. Ndaga fijo shemeji; uzidi kuenjoy ndoa yenu na dada etu[emoji120][emoji120][emoji120]
Wazazi wa mke huwa wana uchungu sana na watoto wa binti yao kuliko wazazi wa mme kwa watoto wa kijana wao. Ndo maana ni vyema mme amuandike mkewe na watoto.Sasa bahati mbaya umefariki una uwakiwa watoto wako watanufaika na mali zako? Kuna jambo nimejifunza kuna rafiki yangu kaka yake alfarikia kaacha mke na watoto wa3 na Nyumba na viwanja kwenye urithi aliandika baba yake, sasa cha kushangaza huyo baba yake ana chukua pesa za kodi ya nyumba ana wagaiya watoto wake t, huyo rafiki yangu akipewa mgao hana kataa, na huyo Baba hawapi mgao mke wa marehemu na wajukuu zake, viwanja vyote mzee ana uza pesa ana wagaiya watoto wake wa kuwa zaa tu.
Nlikumiss big broHapa tunahitaji tume ya uchunguzi
Asilimia kubwa wanawake hawaandiki wanaume kama warithi wao! Nilifanikiwa kufanya hii kazi ya kupeleka taarifa za next of kin pale ofisini kwangu nikaliona hilo! Ila haina shida hata asipokuandika kama mrithi wake pale kunapotokea kifo mume au MKE ndo anapewa kipaumbele kama mna ndoa halali!Sasa cha ajabu nini?? Ni wapi uliona mwanamke anamweka mume kama mrithi my friend. Mimi ni mtumishi sijawahi kuona.. Hata uwaaulize au kuwashauri huwezi kubadirisha hiyo mitazamo yao..
So why ukae uumize kichwa kwa vitu none sense. Unajua wazi kwa nini huwa wanafanya hivyo. Kwa hiyo usiumize kichwa. Au una uhakika atatangulia kufa yeye? If not why bother?
Wote ndio Hali hiyo hiyo na maisha ya naendelea tena kwa furaha na Amani.
Kwani akitangulia wewe utashindwa kutunza watoto mpaka uwe concern na nini aliandika?
Baada ya kifo wanaotesekaga ni wajane (Wanawake) na sio wagane.
Mwanamke anaamini yeye akifa utaoa mke mwingine ambaye ndiye atakayekuja kula vyote alivyochuma au mlivyochuma pamoja na atawanyanyasa watoto wake aliowaacha.... Na wanaona mifano hai kila siku na ni kweli.
Sasa utatumia mbinu ipi kumwaminisha kuwa kwako haitakuwa hivyo?
Kumbuka mwanaume ndio mwenye maamuzi ya kuoa au kuto oa.. Tofauti na mwanamke akifiwa kuolewa ni ngumu sana Maana Hana maamuzi juu ya mwanaume. Labda achukue viserengeti. Ingawa wapo wachache wanao olewa tena.
So relax chapa kazi, lea familia achana na hivyo vitu vidogo kama you're machured enough kwenye ndoa.
Jenga future bora ya familia yako hata usipo kuwepo una uhakika hakuna kikaragosi kutoka kwenye ndugu zako atakae ingilia future na rasilimali ulizoacha vinginevyo usipoteze muda na akili.
Wanaume ndio tunaopaswa kujenga Mifumo ya kuaminika na wenzi wetu vinginevyo mtaishia kuharibu ndoa.
Njia ya kwanza ni kudhihirisha kwa vitendo kuwa huna na huhitaji chochote chake(isipokuwa responsibilities za kawaida kwenye family, mahitaji, maendeleo, Ada etc.) lakini Mali no no.. Jinsi ambayo utakuwa huonyeshi interest kwenye maeneo hayo ndivyo atakavyo kuamini na kukabidhi mwenyewe Mali na mirathi.
Kadiri unavyoonesha interest kwenye vitu hivyo ikiwemo mirathi uliyo Sema ndivyo atazidi kuikimbiza mbali nawe Maana ni Ishara ya kutoaminika.
Be Gentle man my friend utaishi kwa raha, Amani na furaha na mkeo.
Ni kweli mkuu vijana wa sasa tunatakiwa tuache tamaduni za wazee wetu ya kuwategemea watoto, tunatakiwa sisi ndiyo tuwape watoto urithi wa Elimu na pesa ili wasije kujiingiza kwenye tamaa, tunavyo wategeme watoto ndiyo tunazidi kuwa fanya washindwe kutimiza marengo yao.Matola , kila siku nadefend JPM hapa JF maana nilimfahamu tangu anasoma Lake secondary school baada ya kufukuzwa katoke seminary. Tulimzidi umri. Hata Pascal Mayalla kabla ya kuumia mkono na lile lipikipiki likubwa! Oh nisije gundulika nikafuta hii ID. Please behave, nasisitiza mtoto wako akiolewa acha aende akajenge kwa mumewe. Wewe tafuta vyako si kutegemea Watoto. Acha Watoto wajenge maisha yao. Wewe jilie vyako tu.
Ni uchuro kutegemea Watoto wakutunze. Kwa heri na sitaandika tena kuhusu hili
Nipo nipo. Natumai hata kadi ya benki anayo shemejiNlikumiss big bro
Bro nimekabidhi hadi kitambulisho cha nida.... mtu anaekufanya ukunje sura kwa utamu sio wa kumchukulia poa, tatizo tunaangaliaga mabaya tu wakati mazuri ni mengi mnoNipo nipo. Natumai hata kadi ya benki anayo shemeji
Nimemuandika mume baada ya kujua zile form hazina impact kihivo, kwanza mtu ukifa huo muda wa kupekua mafile kutafuta form hawana unless unaishi mbali na ndugu zako.Bro nimekabidhi hadi kitambulisho cha nida.... mtu anaekufanya ukunje sura kwa utamu sio wa kumchukulia poa, tatizo tunaangaliaga mabaya tu wakati mazuri ni mengi mno
Wewe umeonyesha uhalisia wako na maono ya familia yako, na yeye ameonyesha mwelekeo wake. Endelea kuishi.Salaam kwenu,
Niko kwenye ndoa mwaka wa8 saivi na tumejaaliwa kuwa na watoto wawili. Mimi namwenzangu tumeajiriwa Kwenye taasisi moja ya umma japo kwenye vituo tofauti.
Mwezi huu kukatokea agizo lakuhuisha taarifa za wafanyakazi ili ziwe za kisasa na halisia kuliko mwanzo.
Zoezi hili lilihusisha urekebishaji wa baadhi ya taarifa zilizopo kwenye mikataba ya wafanyakazi ambayo waliijaza walipoajiriwa.
Kwa kuwa wakati tunaanza kazi hatukuwa na familia, sehemu ya warithi Kwenye mikataba tulikuwa tumeweka wazazi na ndugu zetu. Sasa kutokana nakuwa na familia tulichopanga mimi na mwenzangu nikwamba kwenye maboresho tujiandike sisi wenyewe Kama warithi wakwanza pamoja na watoto wetu.Mimi kwenye mkataba nikamweka mke na watoto wangu Kama tulivyokubaliana.
Nimekuja kushtuka baada ya kuona mkataba wa mke wangu ambapo yeye kamwandika baba yake mzazi pamoja na watoto. Mimi hakuniandika kabisa.
Mkataba wake nimefanikiwa kuuona baada ya kuongea namhusika aliyekuwa anaikusanya Kisha kuipeleka sehemu husika.Hadi saivi mke hajui kwamba nimegundua kitendo hicho.
Najiuliza,hili tukio mke kalifanya kwa makusudi au bahati mbaya.
Au kitaalam sio lazima mwanamke kumwandika mumewe Kama mrithi?
Je, niendelee kujifanya sijui au nimuulize nijue nia yake yakufanya hivyo?
Wasalaam!
Nenda uombe mkataba wako ufanye amendment kidogo na wewe badilisha weka hata mdogo wako tena wifi yake.
Ngoma iwe draw, wanaita Ngoma ngondoigwa
Hahaa na ana watoto lukuki wa huko njeUnaandika mme ana nyumba ndongo ishirini kidogo. Mimi nimeandika wanangu na baba na mama yangu.
Naanzaje kukosa?🤣🤣Nilikuwa nimemwambia Maxecence Melo usipo-comment kwenye hii post anifute JF permanently
Jamani, Kwenye hii mada naona woooote mmepuyanga kwamba Kazini/Waajiri wanaandika Majina ya Warithi, Hiki kitu Hakipo! Kazini wanaandikishwa NEXT OF KIN kwa maaana ya Mtu wako wa Karibu mwenye Umri wa Miaka 18+ anayeweza kutoa taarifa muhimu kuhusu wewe endapo kuna dharura.Asilimia kubwa wanawake hawaandiki wanaume kama warithi wao! Nilifanikiwa kufanya hii kazi ya kupeleka taarifa za next of kin pale ofisini kwangu nikaliona hilo! Ila haina shida hata asipokuandika kama mrithi wake pale kunapotokea kifo mume au MKE ndo anapewa kipaumbele kama mna ndoa halali!
Na cc tukiamdika watoto wetu wanalalamikaKiukweli nimegundua wanawake wengi hawaandiki waume zao sababu ya maisha ya sasa ww ukiandika andika acha kuwaza jambo ilo ingawa linaumiza