Kwenye safari ya mafanikio ukishajua nyota yako inaandamwa jitahidi sana kudhibiti mhemko (emotion)

Kwenye safari ya mafanikio ukishajua nyota yako inaandamwa jitahidi sana kudhibiti mhemko (emotion)

Lanlady

JF-Expert Member
Joined
Feb 27, 2019
Posts
1,836
Reaction score
6,303
Huu ndio hasa ushauri wangu kwa kaka yangu mkuu wa mkoa wa Arusha. Inaonesha wazi nyota yake ya mafanikio ni kali sana na inaandamwa na kila mwenye nia njema na nia mbaya.

Kwa wasomaji wa biblia wataungana nami kwa kurejea matukio mbalimbali ya kuandamwa kwa watu wenye nyota za mafanikio. Wengine walitakiwa kuuawa ili kuzima mafanikio yao. Mfano Yusufu, Daudi nk. Hawa ni mfano tu wa waliobeba maono.

Hivyo basi ikiwa kuna mtu yeyote anadhani kwamba amebeba maono, na pengine nyota yake imekuwa iking'aa na kuandamwa; basi mtu huyo anapaswa kulinda sana hisia zake na kujiepusha na mihemko. Kwani adui zake huweza kutumia udhaifu huo wa kushindwa kuhimili mihemkonna hatmaye kumtengenezea zengwe.

Huo ni ushauri wangu kwa wote wenye nyota za mafanikio. Najua wakati mwingine si rahisi sana kudhibiti hisia, muhimu ni kujitahidi kwa kila hali kwani kufikia kilele cha mafanikio ni kama kuwa vitani.
 
NYOTA YAKO HAIWEZI ZIBITIWA UKIWA NA YESU KRISTO NDANI YAKO

HERODE ALITAKA KUZUIA NYOTA YESU ISIONEKANE LAKINI CHA AJABU MAMAJUSI KUTOKA NCHI YA MBALI WALIIONA NYOTA INAN'GARA SANA MASHARIKI WAKAJUA KING JESUS ANAZALIWA BASI WAKAMFUATA NA KUMLETEA ZAWADI NZITO NZITO DHAHABU,UVUMBA ,NA MANEMANE NA WAKAMSUJUDIA.
Walokole bhana.
 
Huu ndio hasa ushauri wangu kwa kaka yangu mkuu wa mkoa wa Arusha. Inaonesha wazi nyota yake ya mafanikio ni kali sana na inaandamwa na kila mwenye nia njema na nia mbaya...
Jambo la maana na la tahahadhari zaidi kwa watu makini, ni katika kujidhibiti kutoa siri na nguvu za ufalme kwa maadui :spandauB:
 
Huu ndio hasa ushauri wangu kwa kaka yangu mkuu wa mkoa wa Arusha. Inaonesha wazi nyota yake ya mafanikio ni kali sana na inaandamwa na kila mwenye nia njema na nia mbaya...
Mbona hakuna anayemwandama, isipokuwa hulka yake ya kuwadharau wengine kwa vile yeye ana madaraka ndiyo inayokosolewa? Ana bahati ya kuaminiwa, ila hana bahati ya kutunza hicho anachoaminiwa nacho. Ilitokea hivyo wakati wa JPM na huenda ikajurudia tena...!
 
Huu ndio hasa ushauri wangu kwa kaka yangu mkuu wa mkoa wa Arusha. Inaonesha wazi nyota yake ya mafanikio ni kali sana na inaandamwa na kila mwenye nia njema na nia mbaya.

Kwa wasomaji wa biblia wataungana nami kwa kurejea matukio mbalimbali ya kuandamwa kwa watu wenye nyota za mafanikio. Wengine walitakiwa kuuawa ili kuzima mafanikio yao. Mfano Yusufu, Yakobo nk. Hawa ni mfano tu wa waliobeba maono.

Hivyo basi ikiwa kuna mtu yeyote anadhani kwamba amebeba maono, na pengine nyota yake imekuwa iking'aa na kuandamwa; basi mtu huyo anapaswa kulinda sana hisia zake na kujiepusha na mihemko. Kwani adui zake huweza kutumia udhaifu huo wa kushindwa kuhimili mihemkonna hatmaye kumtengenezea zengwe.

Huo ni ushauri wangu kwa wote wenye nyota za mafanikio. Najua wakati mwingine si rahisi sana kudhibiti hisia, muhimu ni kujitahidi kwa kila hali kwani kufikia kilele cha mafanikio ni kama kuwa vitani.
Huyu hana nyota njema

Labda tukukumbushe umesahau

Alimpiga Mzee warioba akavuruga mkutano wa katiba

Anahusishwa na shambulia la lissu

Anahusishwa na uporaji wa magari ya matajiri

Anahusishwa na upoteaji utekaji na mauaji wakati wa mwendazake

Anahusishwa na uteka wa tajiri na mfanyabiashara Mo

Anahusishwa na kupoteza kwa Ben saa 8

Anahusishwa na kutekwa kwa mwanamuziki Roma mkatoliki

Ana RB anatafutwa na polisi kwa kutishia kumuua mfanyabiasha wa GSM

Huyu ni mhalifu anayelindwa na mfumo
 
Huyu hana nyota njema

Labda tukukumbushe umesahau

Alimpiga Mzee warioba akavuruga mkutano wa katiba

Anahusishwa na shambulia la lissu

Anahusishwa na uporaji wa magari ya matajiri

Anahusishwa na upoteaji utekaji na mauaji wakati wa mwendazake

Anahusishwa na uteka wa tajiri na mfanyabiashara Mo

Anahusishwa na kupoteza kwa Ben saa 8

Anahusishwa na kutekwa kwa mwanamuziki Roma mkatoliki

Ana RB anatafutwa na polisi kwa kutishia kumuua mfanyabiasha wa GSM

Huyu ni mhalifu anayelindwa na mfumo
Waambie ukweli Hawa mapimbi!
 
Huu ndio hasa ushauri wangu kwa kaka yangu mkuu wa mkoa wa Arusha. Inaonesha wazi nyota yake ya mafanikio ni kali sana na inaandamwa na kila mwenye nia njema na nia mbaya.

Kwa wasomaji wa biblia wataungana nami kwa kurejea matukio mbalimbali ya kuandamwa kwa watu wenye nyota za mafanikio. Wengine walitakiwa kuuawa ili kuzima mafanikio yao. Mfano Yusufu, Yakobo nk. Hawa ni mfano tu wa waliobeba maono.

Hivyo basi ikiwa kuna mtu yeyote anadhani kwamba amebeba maono, na pengine nyota yake imekuwa iking'aa na kuandamwa; basi mtu huyo anapaswa kulinda sana hisia zake na kujiepusha na mihemko. Kwani adui zake huweza kutumia udhaifu huo wa kushindwa kuhimili mihemkonna hatmaye kumtengenezea zengwe.

Huo ni ushauri wangu kwa wote wenye nyota za mafanikio. Najua wakati mwingine si rahisi sana kudhibiti hisia, muhimu ni kujitahidi kwa kila hali kwani kufikia kilele cha mafanikio ni kama kuwa vitani.
Ni wakati Gani unaweza kutofautisha kati ya Mhemko na Ukweli?

Tatizo linakuja pale ambapo Watanzania hamtaki kuchukuliwa hatua Kwa uovu mliotenda!! Just call a spade a spade and not a big spoon. Tukishajitambua kuhusu kitu Ukweli ndo hapo nchi itasonga mbele
 
Ni wakati Gani unaweza kutofautisha kati ya Mhemko na Ukweli?

Tatizo linakuja pale ambapo Watanzania hamtaki kuchukuliwa hatua Kwa uovu mliotenda!! Just call a spade a spade and not a big spoon. Tukishajitambua kuhusu kitu Ukweli ndo hapo nchi itasonga mbele
Mhemko ni pale unapofanya jambo au kutoa maamuzi kutokana na hisia zako binafsi.
Kwa mfano kwenye lile tukio, ni kweli kabisa yule dada alikuwa anamjibu kama vile anaongea na 'mshkaji' wake. Sasa, mkuu alipaswa kumsoma na kisha kuendana naye pasipo kumtakia yale maneno.

Tujitahidi sana kudhibiti mhemko. Hata humu jf, kuna watu nia yao ni kukukera. Usipokuwa makini,utawajibu hovyo
 
Back
Top Bottom