Kwenye Sheria ya ndoa Ni vyema kuwe na mabadiliko

Kwenye Sheria ya ndoa Ni vyema kuwe na mabadiliko

Lotus 123

JF-Expert Member
Joined
Nov 5, 2021
Posts
3,151
Reaction score
5,513
Nafikiri Ni wakati muafaka wa kufanya amendment za Sheria ya ndoa ili kuweka wazi baadhi ya Mambo, mfano wanandoa kukubaliana namna ambayo Mali zitagawanywa au kutogawanywa Kama wakiitengana, kuwepo na kipengele Cha idadi ya wenza.

Dini zinaleta shida nyingi zaidi kwenye Mambo ya ndoa, kuwepo na kipengele kuhusu adhabu mahusisi ya mtu anayezini na mke wa mwingine, swala la kugawana Mali si sawa wakati huu kwa kuwa wakati tunafunga ndoa hatukukubaliana mahali popote kuhusu hilo, tunafunga ndoa kidini lakini tukiachana tunaenda mahakamani.

Ndoa zilizofungwa msikitini au kanisani zilitakiwa utatuzi wake uishie huko huko Ni hili unatakiwa wanandoa wakubaliane kabla chombo kitakachokuja tumika kutagua migogoro yao ,I beg to submit.
 
Baadhi ya makanisa kwa mujibu wa imani zao hawavunji ndoa, wanasema alichokiunganisha mungu mwanadamu asikitengenishe. Wanandoa wanaachana lakini hakuna kuo au kuolewa mpaka mmoja afe. Nyuma ya pazia ndoa ikishindikana kuishi Wachungaji wanaivunja kwa mikono ya mahakama bila wao kuhusika
 
Back
Top Bottom