Kwenye vijiwe vya kahawa, kashata kachori na pweza hivi sasa stori kubwa ni Rais Samia

Kwenye vijiwe vya kahawa, kashata kachori na pweza hivi sasa stori kubwa ni Rais Samia

Kusema ukweli kwa kazi mama anapiga siwezi sema anastahili hongera kwasababu naona tayari anayo ila tu mfikishieni salamu nampenda sana kifupi anapendwa kila kona ya nchi hata ukija huku mkoani kwakweli mama Samia anatrend sana, Mungu ampe wepesi kwenye kazi zake.




MAGUFULI4LIFE.
 
nikiwa kiraia zaidi, nimejumuika na wananzengo vijiwe vya kahawa, kashata, kachori na pweza. Stori na hadithi nyingi zimetekwa na jina la Rais, Dr Samia Suluhu Hassan.

Kwamba huyu mama ni hodari, anajali sana, ana bidii mno ya kazi, anaskiza sana maoni ya wananchi, ni mahiri na makini sana kwenye kuchukua maamuzi magumu na hatua za kuwaletea wananchi uhuru, haki na maendeleo.

Wanadai mama amefungua nchi, fursa zipo na zinaonekana saivi na pesa inapatikana kwa wenye kuchapa kazi kwa bidii na inaonekana.

Ubora wa maisha na urahisi wake, unapanda na kuongezeka siku hadi siku. Wangwana na watafutaji hawa wasiochoka wala kukata tamaa, kwakweli wanafurahia na kunufaika kwa jitihada na hatua mbalimbali za kiuchumi anazochukua Raisi.

Wadau wanafunguka zaidi kwamba nchi ni tulivu mno, haijawahi kutokea. Ulinzi na usalama wa mipaka, mali na raia ni wa uhakika sana nchini. Amani imetawala pote Tanzania.

Hii ni sehemu ndogo tu ya makundi mengi sana wanaofurahia na kunufaika na mipango ya serikali ya Dr Samia mthalani bodabodas, mabajaji, madaladala nk.

Wanadai 2025 kama huyu muMama atagombea, basi uhakika wa kura zao ni asilimia 100%. Wanashauri watoa taarifa na wengineneo bora wakafanye mambo mengine lakini sio uongozi wa nchi hii wakati huu.

Kiufupi huyu muMama anapendwa sana na anakubalika mno vijiweni.

Kupambana na huyu mama ni kupoteza muda.....

Wacha tusubiri,
Time Will tell.....
Tumfanye awe Rais wa maisha na hata akifa aendelee tu kutawala maana hana mpinzani na kupambana nae ni kupoteza muda fu.
 
Bara la Afrika ukiwa na Akili timamu fanya kila njia utimkie nje,ukibaki kwenye hili Bara lililojaa watu wajinga na wendawazimu nakuhakikishia UTAIPANDEKA!
Ni kweli usemayo. Wapumbavu ndiyo wanaongoza nchi kwa sapoti ya mapumbavu walio wengi.
 
Atakayechukua Fomu Kushindana na Rais Samia atavuna aibu na kulaaniwa na watanzania. mtu yeyote Asithubutu kuchukua Fomu Kushindana na Rais samia maana aibu atakayoipata kwa hakika atazimia na kupoteza fahamu.

Rais Samia ni mpango wa Mungu Mwenyewe na aliyepewa kibali cha kuongoza Taifa letu.
Unapenda sana kuandika lakini udhaifu wako mkubwa ni kutojua kupangilia point zako zikaeleweka vizuri.Una tatizo pia la kutokujua matumizi sahihi ya alama na wapi uanze na herufi kubwa.Fanyia kazi hili kwakuwa unaonekana umewekeza sana kwenye kutuletea Threads ndefu kila mara.
 
ndoto zako za usingizi wa kwenye daladala 🤣
Tindo alishachanganyikiwa na kuchanganywa na uchapa kazi wa Rais samia na kasi ya mh Rais katika kuwaletea maendeleo wananchi.ndio maana alishabakia anapuyanga tu na vimaneno vyake vya kwenye keyboard akiwa kajificha chumbani kwake. Ukimwambia andamana unaona anakwenda kujificha vichakani na mvuta Bangi mwenzake mdude😄😄
 
nikiwa kiraia zaidi, nimejumuika na wananzengo vijiwe vya kahawa, kashata, kachori na pweza. Stori na hadithi nyingi zimetekwa na jina la Rais, Dr Samia Suluhu Hassan.

Kwamba huyu mama ni hodari, anajali sana, ana bidii mno ya kazi, anaskiza sana maoni ya wananchi, ni mahiri na makini sana kwenye kuchukua maamuzi magumu na hatua za kuwaletea wananchi uhuru, haki na maendeleo.

Wanadai mama amefungua nchi, fursa zipo na zinaonekana saivi na pesa inapatikana kwa wenye kuchapa kazi kwa bidii na inaonekana.

Ubora wa maisha na urahisi wake, unapanda na kuongezeka siku hadi siku. Wangwana na watafutaji hawa wasiochoka wala kukata tamaa, kwakweli wanafurahia na kunufaika kwa jitihada na hatua mbalimbali za kiuchumi anazochukua Raisi.

Wadau wanafunguka zaidi kwamba nchi ni tulivu mno, haijawahi kutokea. Ulinzi na usalama wa mipaka, mali na raia ni wa uhakika sana nchini. Amani imetawala pote Tanzania.

Hii ni sehemu ndogo tu ya makundi mengi sana wanaofurahia na kunufaika na mipango ya serikali ya Dr Samia mthalani bodabodas, mabajaji, madaladala nk.

Wanadai 2025 kama huyu muMama atagombea, basi uhakika wa kura zao ni asilimia 100%. Wanashauri watoa taarifa na wengineneo bora wakafanye mambo mengine lakini sio uongozi wa nchi hii wakati huu.

Kiufupi huyu muMama anapendwa sana na anakubalika mno vijiweni.

Kupambana na huyu mama ni kupoteza muda.....

Wacha tusubiri,
Time Will tell.....
Uchawa umerasimishwa huko CCM
 
Atakayechukua Fomu Kushindana na Rais Samia atavuna aibu na kulaaniwa na watanzania. mtu yeyote Asithubutu kuchukua Fomu Kushindana na Rais samia maana aibu atakayoipata kwa hakika atazimia na kupoteza fahamu.

Rais Samia ni mpango wa Mungu Mwenyewe na aliyepewa kibali cha kuongoza Taifa letu.
Hivi shida ni Nini mwe!!!?
 
Back
Top Bottom