Kwetu mimi pekee sijaelimika ila useremala unanibeba, kaka na mdogo wangu walioelimika wanasota, nashauri VETA kabla ya chuo

Kwetu mimi pekee sijaelimika ila useremala unanibeba, kaka na mdogo wangu walioelimika wanasota, nashauri VETA kabla ya chuo

Kuelimika maana yake nini? Au mpaka ufike chuo kikuu.. Africa bado tuna safari ndefu sana.. (Useremala ilikuwa fani moja wapo ya Yesu ujue)
 
Waliofeli wanafeli Kwa kutumia kufeli Kwa watu wengine kama kipimo cha wao kufaulu. Haoni sabab y kuangalia waliofanikiwa zaidi Kwa sabab Kuna watu wamefeli zaidi yake. We unadhan huyu mtu yuko barab-bara?. Ndo hawa wanaoroga ndug wasifanikiwe ili wawasaidie walahi
Hana muda wa kuangalia waliofanikiwa zaidi yake, wakat ana benchmarking ya familia inamtosha kupiga kelele..
 
Bila shaka waliocomment wengi ni wenye degree na wapo kwa mashemeji zao,nashangaa wanamuwakia mtoa post,wakati mtoa post alikuwa anatoa ushauri.

Hili nimeshajiandaa niandae mazingira ambayo mtoto akiwa likizo aweze kupata muda wa kujifunza utaalamu mwingine nje ya masomo yake ili hata akimaliza chuo aweze kufanya mambo mengine nje ya alichokisomea
 
Bila shaka waliocomment wengi ni wenye degree na wapo kwa mashemeji zao,nashangaa wanamuwakia mtoa post,wakati mtoa post alikuwa anatoa ushauri.

Hili nimeshajiandaa niandae mazingira ambayo mtoto akiwa likizo aweze kupata muda wa kujifunza utaalamu mwingine nje ya masomo yake ili hata akimaliza chuo aweze kufanya mambo mengine nje ya alichokisomea
Hizo gharama za chuo bora nitamshauri aende VETA akimaliza nimpige na kama M2 hivi ya mtaji...Ila kama akilalamika sana unamuacha tu aende chuo
 
Upeo wako wa mambo ni mdogo,ukitaka kujua uhodari wa samaki shindsna nae akiwa kwenye maji,samaki hawezi kuwa mwamba akiwa nchi kavu!!
Hao ndugu zako wangapata fulsa ya kile walichosomea,wangekuwa mbali kwa maendeleo.Kufundisha,ukalimani wa lugha,matumuzi ya IT ofisini,wewe na VETA ysko unaziweza hizi kazi?!!
Kibaya kuhusu Elimu ya juu ni kukosa Skills,waalimu wa VETA ni kutoka kwenye kada ya Elimu ya juu,kama ulikuwa hujuhi,usiwacheke ndugu zako,instegemea wamesomea nini!kama wamesoma Civil engineering,harafu hawawezi kazi ya uselemara,hapo Sawa,maana useremala ni kipengere kwenye kozi yao,lakini kama mtu kasoma,"degree ya heritage preservation,political science,au udakitari,hizi taaluma lazima upewe fulsa ya kuajiliwa kwanza,bila hivyo ni ngumu,hata wao wakienda veta kusoma skills,kwenye ujuzi mbalimbali,watatoboa vzr
Wewe ndo uwezo wako mdogo sana tena sana.Huyo jamaa kaongelea changamoto ambazo familia nyingi zinapitia na yeye katumia familia yake kama mfano mzuri.

Na wala hajasema anajisifia...Na pia kama kweli kafanikiwa hivyo nampa pongezi.Na suala sio hizo ajira tu..ni malipo au mishahara baada ya kuajiriwa na uhalisia wa gharama za maisha.

Lazima tuweze kutumia elimu zetu tuweze kusurvive na kuishi..na ndo maana tunafundishwa vitu vingi sana ukiachilia professional tunazotumia.

Waendelee kuwasupport kwa biashara ndogo ndogo hao ndugu zake...na pia wao wanaweza kutumia elimu zao na exposure zao kuangalia hiyo biashara ya useremala wanaweza msaidia vipi etc...Elimu zao zitumike nyumbani, na watafanikiwa.Na hata huko baadae wakipata ajira waendelee kuendeleza hizo biashara zao na zaidi wakimtumia huyo huyo ndugu yao ambaye tayari anaexperience ya ujasiriamali
 
Ni kweli kabisa, kwenye maamuzi inabidi tupime mzani sehemu yenye ujitaji zaidi.

Kwa sasa kuna tatizo kubwa sana la ajira, kwenda veta ni muhimu zaidi kumuandaa kijana awe na ujuzi wa kuanza kujitegemea akikosa ajira ama anavyoendelea kuomba ajira.

Akienda Jkt haitamsaidia akikosa ajira. Ukakamavu wa kujikomboa kiuchumi Veta na muhimu zaidi.

Mkuu, kwa hoja hizi, una elimu kubwa sana. Endelea kupambana, utaajiri wengi.
 
Naumia sana nikifikiria wazazi walivyojinyima kutulipia ada, kuna kipindi walikopa kabisa, naumia sana kuona mategemeo ya wazazi kwa ada walizolipa hayajafikiwa,,, Inauma sana !!

Ukiachana na maumivu ya wazazi na mimi napitia maumivu mazito, kaka na mdogo wangu walisoma kwa juhudi sana, sioni kama ipo fair kwa wanachopitia, walistahili zaidi sana sana sana. mtu alie kwenye unafuu wangu akijisifu ana ahueni basi ni wazi ni mjinga.


Binafsi niliishia form 4 mwaka 2012 shule ilinipita kushoto, mzee aliniambia nijiandae kurudi kijijini, ilibidi nikajiongeza nianze kujifunza chochote nikaingia kwenye useremala kwa msaada wa mjomba wa rafiki (mjini connection), nikawa saidia fundi kidogo nikaweza kuhama hata nyumbani na kumiliki pikipiki, nikajichanga changa na mimi nikawa na ofisi yangu inayonipa kipato si haba kwakweli hata kagari kapo, haikuwa rahisi hata kidogo hasa mwanzoni, kuna kipindi kidume chozi lilinitoka kwa ugeni wa kazi lakini nilikomaa.

Sasa hapo home kuna bro na mdogo wangu wa kike wamemaliza vyuo ngazi ya degree lakini mambo si mambo kiuchumi, bro alihangaika hizi kazi za kujitolea, akaingia kitaa akapata kazi kampuni binafsi kazi kibao malipo kiduchu, alisota miaka minne kampuni ikafungwa na kazi ikaisha,,, ikabidi home pale tujichange tumpe mtaji, ikabidi ajifunze kunyoa nae akafungua ofisi yake, kiuchumi pana nafuu lakini hadi kafika hapo kapitia misoto kwa ukosefu wa ajira za ofisini.

Kwa mdogo wangu nae tangu 2020 alipomaliza chuo hali bado sio poa, ilibidi tujichange change nae apige mwendo, biashara ya keki mara ya kwanza ilibuma kwake akawa yupo home, tukajikusanya kusanya kwa sasa angalau ana kamgahawa kidogo pana unafuu.

Nilichokuwa najiuliza ni kwamba, hizi elimu zinaandaa wengi wawe maofisini wanasukuma kalamu na kukaa kwenye viti wakisubiri mishahara lakini hizi ajira zimekuwa adimu, nimeona kwamba yafaa zaidi kungekuwa kuna veta kabla ya kwenda chuo.
Hamna lolote umejitungia uwongo ujifurahishe na ukashifu elimu ambayo ulishindwa kuipata. watu kama wewe tunawafahamu wako wengi ni kama wachawi wako kuwakatisha tamaa watu wengine wasisome. We umeshindwa kusoma wacha upambane na hali yako siyo kuja kusemea elimu vibaya humu. Elimu kuitafuta ni agizo la Mungu watu wataenedelea kusoma mlioshindwa pambaneni na mambo yenu mengine.
 
Nakuunga mkono sana kwenye hili Mkuu, tena kama kwa sasa hali ya kiuchumi hairuhusu basi badala ya JKT ni afadhali iwe kwenda VETA.

Hata kama sio wote watapata nafasi, hao hao wachache kwa utaratibu utakaoonekana unafaa waende wakajifunze ufundi.

Kuna watu watatetea JKT lakini kiuhalisia ni kupotezeana muda na kutesana bila sababu.
Nakuunga mkono.
Kwa sababu lengo la kupeleka vijana JKT ilikuwa kuwafanya wawe wazalendo,kuwaondoa uwoga na kuwa shupavu/shujaa.
Lakini nikiwacheki bado ni waoga na panya road wanasumbua mitaani.
 
Naumia sana nikifikiria wazazi walivyojinyima kutulipia ada, kuna kipindi walikopa kabisa, naumia sana kuona mategemeo ya wazazi kwa ada walizolipa hayajafikiwa,,, Inauma sana !!

Ukiachana na maumivu ya wazazi na mimi napitia maumivu mazito, kaka na mdogo wangu walisoma kwa juhudi sana, sioni kama ipo fair kwa wanachopitia, walistahili zaidi sana sana sana. mtu alie kwenye unafuu wangu akijisifu ana ahueni basi ni wazi ni mjinga.


Binafsi niliishia form 4 mwaka 2012 shule ilinipita kushoto, mzee aliniambia nijiandae kurudi kijijini, ilibidi nikajiongeza nianze kujifunza chochote nikaingia kwenye useremala kwa msaada wa mjomba wa rafiki (mjini connection), nikawa saidia fundi kidogo nikaweza kuhama hata nyumbani na kumiliki pikipiki, nikajichanga changa na mimi nikawa na ofisi yangu inayonipa kipato si haba kwakweli hata kagari kapo, haikuwa rahisi hata kidogo hasa mwanzoni, kuna kipindi kidume chozi lilinitoka kwa ugeni wa kazi lakini nilikomaa.

Sasa hapo home kuna bro na mdogo wangu wa kike wamemaliza vyuo ngazi ya degree lakini mambo si mambo kiuchumi, bro alihangaika hizi kazi za kujitolea, akaingia kitaa akapata kazi kampuni binafsi kazi kibao malipo kiduchu, alisota miaka minne kampuni ikafungwa na kazi ikaisha,,, ikabidi home pale tujichange tumpe mtaji, ikabidi ajifunze kunyoa nae akafungua ofisi yake, kiuchumi pana nafuu lakini hadi kafika hapo kapitia misoto kwa ukosefu wa ajira za ofisini.

Kwa mdogo wangu nae tangu 2020 alipomaliza chuo hali bado sio poa, ilibidi tujichange change nae apige mwendo, biashara ya keki mara ya kwanza ilibuma kwake akawa yupo home, tukajikusanya kusanya kwa sasa angalau ana kamgahawa kidogo pana unafuu.

Nilichokuwa najiuliza ni kwamba, hizi elimu zinaandaa wengi wawe maofisini wanasukuma kalamu na kukaa kwenye viti wakisubiri mishahara lakini hizi ajira zimekuwa adimu, nimeona kwamba yafaa zaidi kungekuwa kuna veta kabla ya kwenda chuo.
Na ndiyo maana wadau wa elimu tunaendelea kupiga kelele ili serikali ibadilishe hii mitaala yao ya sasa.

Kuna umuhimu mkubwa wa kuwekeza kwenye elimu ya kumjengea mhitimu maarifa na ujuzi zaidi, kuliko hii elimu ya sasa ambayo imejikita zaidi kuwandaa wahitimu kufaulu mitihani ya kukaririshwa, na baadaye kuajiwa.

Elimu ya ufundi, ubunifu, ujasiriamali, usimamizi katika biashara, michezo, muziki, tehama, nk ipewe kipaumbele kwenye mitaala mipya.
 
Kwenye ukoo wetu kuna wasomi kibao lkn yupo Mwamba mmoja wa darasa la 7 na biashara yake ya mkaa anakimbiza wote. Wanamuogopa
Ndiyo matokeo ya ujinga, angalia ulicho-comment. Watu hawasomi watajirike, elimu ni kwa ajili ya kutoa huduma ndugu. Utibiwe na daktari, nesi, upimwe na mtaalam wa maabara, uandikiwe dawa na mfamasia. Ujengewe na injinia, mifugo yako itibiwe na bwana mifugo. Uhudumiwe benki na mtalam wa mambo ya benki. Kesi yako isimamiwe na mwanasheria. Mkipataga matatizo ndio mnajua umuhimu wa wasomi sahivi umekula mihogo yako huna tatizo unaweza kuandika chochote. Hakuna mbadala wa elimu ukishindwa kaa pembeni. Ujinga ni mzigo mzito sana kuubeba. Nenda shule umri ni namba tu uone raha ya kusoma, ukitaka kujua utamu wa ngoma uingie ucheze.
 
Naumia sana nikifikiria wazazi walivyojinyima kutulipia ada, kuna kipindi walikopa kabisa, naumia sana kuona mategemeo ya wazazi kwa ada walizolipa hayajafikiwa,,, Inauma sana !!

Ukiachana na maumivu ya wazazi na mimi napitia maumivu mazito, kaka na mdogo wangu walisoma kwa juhudi sana, sioni kama ipo fair kwa wanachopitia, walistahili zaidi sana sana sana. mtu alie kwenye unafuu wangu akijisifu ana ahueni basi ni wazi ni mjinga.


Binafsi niliishia form 4 mwaka 2012 shule ilinipita kushoto, mzee aliniambia nijiandae kurudi kijijini, ilibidi nikajiongeza nianze kujifunza chochote nikaingia kwenye useremala kwa msaada wa mjomba wa rafiki (mjini connection), nikawa saidia fundi kidogo nikaweza kuhama hata nyumbani na kumiliki pikipiki, nikajichanga changa na mimi nikawa na ofisi yangu inayonipa kipato si haba kwakweli hata kagari kapo, haikuwa rahisi hata kidogo hasa mwanzoni, kuna kipindi kidume chozi lilinitoka kwa ugeni wa kazi lakini nilikomaa.

Sasa hapo home kuna bro na mdogo wangu wa kike wamemaliza vyuo ngazi ya degree lakini mambo si mambo kiuchumi, bro alihangaika hizi kazi za kujitolea, akaingia kitaa akapata kazi kampuni binafsi kazi kibao malipo kiduchu, alisota miaka minne kampuni ikafungwa na kazi ikaisha,,, ikabidi home pale tujichange tumpe mtaji, ikabidi ajifunze kunyoa nae akafungua ofisi yake, kiuchumi pana nafuu lakini hadi kafika hapo kapitia misoto kwa ukosefu wa ajira za ofisini.

Kwa mdogo wangu nae tangu 2020 alipomaliza chuo hali bado sio poa, ilibidi tujichange change nae apige mwendo, biashara ya keki mara ya kwanza ilibuma kwake akawa yupo home, tukajikusanya kusanya kwa sasa angalau ana kamgahawa kidogo pana unafuu.

Nilichokuwa najiuliza ni kwamba, hizi elimu zinaandaa wengi wawe maofisini wanasukuma kalamu na kukaa kwenye viti wakisubiri mishahara lakini hizi ajira zimekuwa adimu, nimeona kwamba yafaa zaidi kungekuwa kuna veta kabla ya kwenda chuo.
Mstari wa mwisho kuwe na Veta kabla ya chuo ndo umebeba dhima yenyewe
 
Back
Top Bottom