Laiti kama Ruto angeyafanya haya kabla ya maandamano ya gen Z angeimbwa kama shujaa wa Afrika. Afrika tunakwama wapi!?

The Phylosopher

JF-Expert Member
Joined
Mar 11, 2015
Posts
1,968
Reaction score
2,957
Mtu mmoja aliwahi kuniambia usemi unaosema tujifunze kwa makosa hauko sahihi kwani kuna makosa hayatakupa muda wa kurekebisha chochote.

Ni kwa sababu ya hiyo dhana namuona Ruto alikuwa na nafasi nzuri sana ya kuimbwa na historia kama Rais aliyejali wanyonge kwa kupunguza matumizi ya wakubwa.

Bahati mbaya amechelewa maana kwa vyovyote atakavyofanya sasa itaonekana ni kwa sababu ya presha ya wananchi.

Hayo mambo aliyoyaamua yapo sana hata hapa kwetu yaani bunge kujadili mafao ya wake za viongozi wakati tuna waalimu ambao wanalipwa laki tatu na nusu na watu duni wengi tu.

Naomba Serikali zetu zitumie hili saga la Kenya kujifunza kuachana na matumizi ya kijinga yasiyoendana na uhalisia wa maisha ya watu wanaowaongoza.

Zaidi ya hayo naomba watawala wetu waachane na machawa na wasifiaji wavae uhalisia wa maisha ya watu wao na shida zinazotesa watu na wasiwachukie wakosoaji maana mkusanyiko wa wakosoaji wengi ndio huzaa uasi.
 
Tungejifunza wapi,
ujasiri, uthubutu na umakini wa hatua anazochukua kutuliza na kuzima mihemko ya maandamano ya amani yaliyokosa uelekeo na kupoteza malengo na kugeuga ghasia?πŸ’

Huyu ni shujaa, mwenye utashi na haiba ya tofauti na ya kipekee kabisa na viongozi karibu wote wa kisiasa Africa....

kongole nyingi sana kwa maamuzi magumu anayoendelea kuyachukua na kurejesha Amani katika Taifa la Kenya πŸ’
 
Alipaswa asisubiri watu waingie barabarani na kuandamana alitakiwa kufikiri sana na haya maamuzi aliyoyatangaza sasa alitakiwa kuyafanya mapema kabisa akianza utawala wake.
Sasa kusubiri Hadi hasira za wananchi ndio uanze kufuta mashirika kufuta malipo kwa wake zako kusitisha ununuzi wa magari angeweza kufanya hayo mapema sana
 
95% ya viongozi wa Africa ni wajinga sn ni miungu watu wanamini wapo ajili ya kutumikiwa na wananchi na siyo kuwatumikia wananchi, maendeleo na kuishi kwa wananchi inakuwa ni hisani yao na siyo takwa la kikatiba wala kisheria, vijana wakiamka mbona Africa ni tajiri sn na ufisadi ukipungua tu hata kwa 25% mbona Ulaya wataanza kuja kuomba misaada Africa, Africa inateswa na viongozi mafisa na wenye viburi.
 
Viongozi wengi wa Africa ni wajinga sn wana viburi
 
Mie nadhani Mungu alitaka tujifunze jambo la maana sana kupitia huyu Rais William Samoe Arap Kipchirchiri Ruto, kwa mtu alieko katika uongozi wa kisiasa katika serikali za wanadamu, anastahili kufanya panapotokea ugumu. Mpaka sasa hapo wanasiasa tumechota maarifa πŸ’

jinsi ya kudhibiti hasira za waandamanaji ni Jambo lingine pia
 
muerevu unaongea kwa uchungu sana πŸ’
 
Hustler ameamsha hasira za common wananchi.Ma bad@πŸ˜ŽπŸ™
 
Ebu kanza mtuambie nasisi tujue amwfanya maamuzi gani huyo hastla, maana huku back benches sauti haifiki...🀨
 
Kwa ujinga tulionao sidhani kama kuna la kujifunza
Kila wakati neno hili nalisikia ooh kuna la kujifunza
Hii shule mtamaliza lini?
Naona mnataka kukusanya dhahabu zihifadhiwe Bank
Mnachimba ila hamuhifadhi
Kuna nchi hawana ila wananunua na kuweka

Kila leo kuna la kujifunza
Huyu Ruto awashukuru wakuu wa vikosi wasomali maana wakikuyu na wangemtoa madarakani
 
Ebu kanza mtuambie nasisi tujue amwfanya maamuzi gani huyo hastla, maana huku back benches sauti haifiki...🀨
Nyuzi za hotuba yake zimo humu ndani amefanya mageuzi makubwa sana kwenye matumizi ya serikali kiasi cha kunusuru ksh billion 177
 
Tanzania.

Viongozi hakuna kitu watajifunza wana viburi vya madaraka, madaraka yanawapofusha, madaraka yanawalevya.. Lakini wanajua kuwa sisi watanzania ni waoga, sisi ni kama WAFU hivyo hakuna kitu kitakaa kitokee.
 
Sidhani kama tatizo la tunao wapa dhamana ni chawa liko Kwao wenyewe Kwa kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama kutumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi na uoga kwa viongozi wao, a.k.a kujizima data
 
Huwezi kuwa na mipango huku unawaza kuiba na kuwaja uchaguzi ujao lazima kuwe dira ya taifa na siyo maono ya Rais
kama kiongozi mwenye dhamira njema na maono ya mbali sana katika kuwaletea maendeleo na kuinua hali za maisha ya wanainchi sina mawazo kama hayo, labda wengine πŸ’

hata hivyo,
Kama Taifa tunayo dira ya maendeleo ya Taifa sambamba na global , seventeen sustainable development goals πŸ’
 
Umeona zinafuatwa au tunafuata maono ya Rais aliyepo madarakani? kila Rais huja na mawazo yake huoni Marekeni kila Rais lazima afuate dira ya taifa, kesho Rais akisema tuanze kilimo cha matikiti kuna mtu atabisha? Royal tour iko wapi? annuani za makazi zipo wapi? ni utapeli tapeli tu hakuna la maana hajui hata tunataka kufanya nini
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…