Naaaamu Turejee sasa
Jamii forum na Hati chafu, za mapenzi ni kweli zinaharibu nyuzi???? Mkaguzi mkuu wa nyuzi JF
fdizzle na msaidizi wake
TODAYS wata jibu Embu tuone
Inaendea
kile chombo chao au meli walyokuja nayo ilikua na mushkeri kidogo sasa kufika kwao pale ni kwajili ya marekebisho alafu ile meli kumbe waliiteka na watu waliopo mule sikujua waliwaacha wapi nahisi yawezekana waliwatosa majini lakini pia mule mlikua na vitu walivyoteka Mchele, unga, sukari, samaki na vingne vingi kwaiyo kwa ishu ya misosi aikua tabu tena kwangu apo ni mtelezo tu.
Kwaiyo apo sasa yule Sofia ndio alikua mpishi na Mimi mda mwingi ndio nilikua nae kumsaidia kutengeneza samaki na mboga mboga kisha msosi fresh.
Wale jamaa walendelea kuwepo pale mpaka maji yalipo pungua kwwnye kile kisiwa kunakua na siku maalumu ya kutoka yale maji sasa ile meli ndio ilikua na tatizo chini kwaiyo maji Yale yalipo pungua ndipo ikawa nafasi ya wao kuweza kurekebisha ile meli.
Walifanya mawasiliano na wenzao wakaja pale wakfanya marekebisho ile meli ikapata afazali sasa hapo ndio wakaniambia twende mbele yani niondoke nao kuelekea uko kwenye uharamia wa kuteka meli baharini humo .
Walitoa begi moja la silaa kisha wakaniambia nichague ipi itakayo nifaa nikachagua silaa moja inaitwa Raifo sina hakika kama nimeandika sahihi wakaniuliza kwann umechagua hii niliipenda tu zile ni Silaa ambazo zilitumiwa na ma sniper kwa juu ilikua na lenzi binafsi nieleze nilishawai kufundshwa kutumia silaa na babu yangu alikua muwindaji wa wanyama pori alikua anatumia izi silaa lakini sio kama ile.
Hii iliboreshwa zaidi na baba yangu nae alikua mtaalamu wa kutumia silaa.
Basi nilichukua ile silaa ili kuwaonesha kwamba na Mimi naweza itumia nikafanya jambo moja wale wabaya wangu nyani ndio nikaona ngoja niende uko Leo nika wanyooshe nikamchukua Sofia tuka elekea kule msituni uzuri nikakutana nao tukiwa na Sofia nikamtandika nyani mmoja na tukarudi kule na Sofia na yule nyani.
Yule nyani pale wale wajamaa walimtafuna vizuri mi ndio nilimtengeneza sasa hapa nikajua jamaa hawa magumashi akuna cha dini wala nini hawa ni maaalamia tu dini wanayao lakini awa izingatii wnabaki tu na kivuli cha dini awana lolote tulikula nyani yule vizuri .
Sasa tukaingia kwenye utekaji katika ishu hii ya utekaji tulishateka teka sana Ila kuna tukio moja lilikua kubwa ambalo tulikutan nalo uko baharin, tulikutana na meli ya wafanya biashara ambayo ilikua na mizigo tuliwateka wale jamaa na tukachukua mzigo wao,
wao tukawaacha na hata meli atukuizamisha sasa kumbe wale jamaa wakafanya mawasiliano na askari wa patrol kutokana na ule uaharamia tuliofanya sisi atuna habari ghafla wakaja wale patrol na boti zao walitumia spika vipaza sauti vile kwamba tunatakiwa tujisalimishe alafu ile meli yetu pale palipotengenezwa palileta itilafu tena kwaiyo ikawa aina spidi sasa mi ndio nilikua na ile silaa ya kulenga mbali nilikua juuu
kwaiyo pale ikabidi nianze akuna kungoja walikua na boti zao mbili nilipiga moja kwenye tenki za mafuta nikapasua wale jamaa fasta wakahamia nyingne nzima ile niliyopiga ikalipuka hapa nafikiri wali elewa kua kuna mdunguaji.
Awakuchukua mda waliondoka pale sie tukaendelea na safari yetu taratibu alafu katika kupora vitu kuna jamaa nilimpora begi ndogo ivi ye nahisi alikua mtu wa kanisa nilivyo fungua nilikuta kuna vitu vya kanisa na pia kulikua na msaba wa dhahabu niliuchukua nikauficha ikitokea uko mbeleni unisaidie kama nikiuza.
kumbe walivyo ondoka wale patrol walienda kujipanga,
sisi atuna habari
Ghafla walifika wale jamaa na boti tatu tena sasa walipofika awakuchelewa wakaanza kurusha risasi kwetu yule masuz na mwingne ally pamoja na mwingne tena kasimu wao wakaanxa kujibu mashambulizi mi nilkua kwa juu kabisa wao wapo chini katika kurushiana zile silaha yule masuz dada ake na Sofia akapigwa risasi kifuani kwenye moyo nyingne begani akazima pale pale.
Sasa kule juu Mimi nikaendelea kulusha zile risasi ila walikua wanatuzunguka awatulii sehem moja baadae Mimi niliipigwa risasi ya kiuno lakini ilinipalaza au kunikwangua aikuingia moja kwa moja nilikua navunjika kiuno hapa lakini sikupata athari kubwa basi nilidondoka toka kule juu mpaka chini kwenye meli nikapoteza fahamu pale pale.
Nilipokuja kuzinduka tuilikua kisiwani yule Sofia alikua akinisaidia kunitibu lile jeraha la kuchunwa na risasi alitumia kisu cha moto kuchoma lile jeraha kuondoa kama kuna unga ule wa silaha ili kuua sumu maana zikibaki huwa zinaleta mazara ata kansa pia akachukua majani flani ivi porini akaniwekea ya dawa.
Jamaa yule kaka ake na Sofia masuz tayari alishafariki ivyo tulifanya namna pale tuakamsitiri jamaa, Dada ake alikua na majonzi sana siku ile ndio ishatokea sasa,
Tulikaa pale kwa siku kazaa baadae tukaondoka pale kisiwani tuka elekea kwao walikotokea wao uko somalia namimi kama jamaa yao tulishaungana pale basi tulienda waote mpaka somalia.
Tulipofika kule baada ya kuwasili Mogadishu niliambatana na Sofia mpaka kwenye makazi yake nilikutana na ndugu zake akanitambulisha fresh na pia akafanya mpango kwenye shughuli za uvuvi kuniunganisha na jamaa flani ivi ambao wao walikua wana vua papa kwa kutumia ndoana flani ivi za shaba ndio zilikua imara kwa kuwanasa wale papa.
Niljiunga na jamaa kufanya ile kazi ila Mimi nilikua upande wa kuchochea makaa ya mawe tulikua kwenye zile meli zinazotumia makaa ya mawe sio mafuta ndio nilikua na chochea ila baadae nilisogea mbele nikaacha kuchochea makaa nikawa kwenye upande wa kuvua.
Kule sasa kwenye kuvua ndio nikajua jamaa wanavua papa kwa kutumia chambo za mahiti ya watoto wachanga wa binadamu jinsi wanavyopata vichanga ni vile labda kama mtu mimba yake imeharibika au mtoto kafia tumboni zile mimba kubwa au kazaliwa kafa au wale wanao toa ujauzito mimba kubwa sasa katika kutupa ndio watu wanatumia iyo fursa ule uchafu unachukuliwa na inawekwa oda kabisa kwenye ma hospital tena ina pesa nzuri tu ambayo ma dokta huwa wanapata kupitia hii ishu mpaka leo.
Lakini ni kwa usiri inafanyika hii biashara sio waz wazi so kupitia chambo hiki papa huwa wanakamatika kilahisi na hata ukimpasua ishu ya kukuta labda sikio la binadamu au kidole nywele viungo vya binadamu kwa ujumla ni kawaida sana
Ni ishu ya kikatili ki binadamu lakini ndio watu na kazi zao ..................... Latino is on
Sio kweli
slip way