Lawama zote za umeme ziwaendee Kitila Mkumbo na Nehemiah Mchechu

Lawama zote za umeme ziwaendee Kitila Mkumbo na Nehemiah Mchechu

Kenya waligawa shirka la umeme na sasa wanataka kuliunganisha tena.

Kwa Tanzania kwa sasa kugawa shirika sio akili wala maamuzi ya busara.

Fikiria hivi.
1. Generation wakizalisha umeme, watauzia transmission.

2. Transmission watauliza distribution kwa profit margin.

3. Distribution watauzia wateja wadogo wadogo kwa profit margin.

Mwisho mteja ndie atabeba mzigo wote wa hizo department.

Ndio maana nchi kama Kenya gharama za umeme ziko juu sana kwa sababu kama hizo.

Je watanzania wataweza kubeba gharama halisi za umeme?

Kumbuka Tanesco wameshasema mara nyingi kwamba bei yao ya umeme haiko halisi, ni bei ya chini kuliko uhalisia.

Hilo jambo limewashimda Kenya.
Ukiipata business model tu imekula kwako
 
Ile software walionunua na January ya billions 70 kutoka kuwa wahindi ingeisaidiaje TANESCO ili hali shirika halikuwa na matatizo kwenye distribution?
Mama Abdul kwa kuwakingia kifua hawa vijana majambazi unaipeleka nchi kubaya . Hawa wezi wanatakiwa wawe jela hivi sasa kwani hawawezi kuthibitisha kuwa nyumba walizonunua huko Dubai hazikutokana na ufisadi wao hapo TANESCO
Haaaa! ule ni mfumo mzima wa database ya shirika, si ya wale Mahindra lakini wali fail mapema sana ndiyo tunarudi pale pale hakuna usimamizi mzuri wa shamba la bibi Kwa maana kila mmoja akiona kuna upenyo anachota chake mapema.
TANESCO sehemu iko na wajinga wengi na ndiyo yenye staffs wengi ni distribution note me, Maharage aliwapa hela nyingi zaidi ya 3billion Kwa mikoa class A na 2 b Kwa mikoa mingine wafanye matengenezo yenye tija ahaaaa mtu mweusi akaonesha rangi yake Kwa kurudisha pesa mwisho wa mwaka wa bajeti tena karibu nusu, jamaa hapo ndipo alipoona kumbe humu Tanesco wajinga ni wengi sasa mwaka uliofuatia wa fedha akahamisha magori yote ofisini kwake ili ajipigie vizuri. Ukimpata Engineer wa Tanesco muulize yupo kitengo gani na yapi majukumu yake utakuja nipatia majibu hapa , kile ni kijiwe hakuna mgawanyo wA kazi hapo utategemea kupata matokeo chanya sahau. Ujawagusa hao mameneja wengi wao ni mzigo kama MD wao.
 
Bila kutafuna maneno, TANESCO ni shirika la umma lililoshindwa kabisa kufanya kazi zake ipasavyo.

Reforms za mashirika yote ya umma kwa sasa zipo chini ya Kitila Mkumbo na Nehemiah Mchechu.

Hao mabwana wakubwa wawili wameshindwa kuyaona yaliopo Tanesco> Wameshindwa kuelewa kuwa Tanesco hakuna "reforms" zitakazofanyika na kuwaokowa Watanzania na janga la umeme?

Sababu kila namna zitatolewa, lawama zitapelekwa kila mahala, sababu za kujitetea zinazoingia akilini hatzitokosa kuwepo, lakini ukweli ni kuwa Tanesco limekuwa ni shirika kubwa sana lisilo na faida (Huge White Elephant".

Ushauri na nyinyi kifanyike hatraa sana? Hakuna zaidi ya kulikata kata shirika na kulipunguza ukubwa wake.

Tanesco ianze kubomolewa kimikoa. Kila mkowa uwe na shirika lake la Umeme la kujitegemea, tuuziane umeme kimkoa. Simple and straight foreward solution.

Tuanza na mkoa mmoja mmoja hataka sana. Kila mkoa uwe na shirika lake la umeme.

Nje ya hapo, hata mabwawa yote, pamoja na bwawa jopya la Steigler, yazalishe umeme kwa 100% pamoja na vinu vyote vya Kinyerezi na IPtL na majenereta ya kizamani yazalishe, bado tatizo litakuwepo na pengone litazidi.

Kila mkoa ujipatie shirika lake la umeme na watendaji wake, ndiyo njia pekee iyayowezesha "monitoring and evaluation" ya ufanisi. Nje ya hapo tutapigana porojo kila siku.

Kitila na mchehu na ujanja wenu wote wa maneno, mmeshindwaa kuliona hilo? Au mmefungwa mikono? Mnalo la kujibu kwa Watanzania. Au mtueleze wazi kuwa TANESCO haipo chini yenu?

Kuilaumu serikali yote na kuilaumu tanesco yenyewe, ambayo haijuwi la kufanya utabaki kuwa ni ujinga tu. Wenye dhamana ya mashirika ya umma kwa sas ni hao watu wawili. Waje watueleze wamefanya, wanafanya nini kuhusu tatizo la daima la TANESCO?

Kuendelea kulilea shirika la TANESCO, unakuwa ni uongozi wa zima moto, utazimwa moto unapowaka lakini baada ya muda unaanza tena. Ukweli ni kuwa Reforms zimeshindikana Tanesco, tuingie kwenye Rebuilding ya Tanesco. Uta Rebuild bila kubomowa? Mawee.
Mawazoduni ya mtu asiyeenda hatashule
 
Nimeshangaa siku hizi Mpaka watu wazima na wazee umeme ukirudishwa wanashangilia Kama yanga au simba amefunga goli !
 
Bila kutafuna maneno, TANESCO ni shirika la umma lililoshindwa kabisa kufanya kazi zake ipasavyo.

Reforms za mashirika yote ya umma kwa sasa zipo chini ya Kitila Mkumbo na Nehemiah Mchechu.

Hao mabwana wakubwa wawili wameshindwa kuyaona yaliopo Tanesco> Wameshindwa kuelewa kuwa Tanesco hakuna "reforms" zitakazofanyika na kuwaokowa Watanzania na janga la umeme?

Sababu kila namna zitatolewa, lawama zitapelekwa kila mahala, sababu za kujitetea zinazoingia akilini hatzitokosa kuwepo, lakini ukweli ni kuwa Tanesco limekuwa ni shirika kubwa sana lisilo na faida (Huge White Elephant".

Ushauri na nyinyi kifanyike hatraa sana? Hakuna zaidi ya kulikata kata shirika na kulipunguza ukubwa wake.

Tanesco ianze kubomolewa kimikoa. Kila mkowa uwe na shirika lake la Umeme la kujitegemea, tuuziane umeme kimkoa. Simple and straight foreward solution.

Tuanza na mkoa mmoja mmoja hataka sana. Kila mkoa uwe na shirika lake la umeme.

Nje ya hapo, hata mabwawa yote, pamoja na bwawa jopya la Steigler, yazalishe umeme kwa 100% pamoja na vinu vyote vya Kinyerezi na IPtL na majenereta ya kizamani yazalishe, bado tatizo litakuwepo na pengone litazidi.

Kila mkoa ujipatie shirika lake la umeme na watendaji wake, ndiyo njia pekee iyayowezesha "monitoring and evaluation" ya ufanisi. Nje ya hapo tutapigana porojo kila siku.

Kitila na mchehu na ujanja wenu wote wa maneno, mmeshindwaa kuliona hilo? Au mmefungwa mikono? Mnalo la kujibu kwa Watanzania. Au mtueleze wazi kuwa TANESCO haipo chini yenu?

Kuilaumu serikali yote na kuilaumu tanesco yenyewe, ambayo haijuwi la kufanya utabaki kuwa ni ujinga tu. Wenye dhamana ya mashirika ya umma kwa sas ni hao watu wawili. Waje watueleze wamefanya, wanafanya nini kuhusu tatizo la daima la TANESCO?

Kuendelea kulilea shirika la TANESCO, unakuwa ni uongozi wa zima moto, utazimwa moto unapowaka lakini baada ya muda unaanza tena. Ukweli ni kuwa Reforms zimeshindikana Tanesco, tuingie kwenye Rebuilding ya Tanesco. Uta Rebuild bila kubomowa? Mawee.
Naona wahuni mnatafuta sababu ya kuiuza Tanesco kwa waarabu. Kwendeni zenu.
 
You are making one wrong assumption kuwa GENERATION, DISTRIBUTION NA TRANSMISSION zitakuwa owned by different entities!! Hiyo model yako ni hiyo madalali walioko planning commission wanaipigia chepuo ili wauze na kupata commission yao!!
The model being advocated here is where the entities while separate but are still Mali ya UMMA; so hilo suala la profit spread will easily be mitigated!
Sio lazima kama Kenya wameshindwa na Tanzania nayo ishindwe! Tusiwe wavivu wa kufikiri.
Mkuu, kua mali za umma haiondoi uhalisia wa gharama za umeme.
 
Acheni lawama, mama alishasema mwisho wa umeme kukatika ni mwezi wa tatu...waacheni TANESCO watekeleze majukumu yao halali
Hata wapewe miaka 20 hawatakuja na Suluhu yoyote..

Kwani haya matatizo ya umeme yameanza juzi wakati wa Samia Suluhu Hassan?

Yameanza seriously wakati wa Jakaya Kikwete pale ambapo watumiaji umeme walipoongezeka sana huku vyanzo vya umeme vikiwa vilevile..

Watu wakatumia fursa ya matatizo haya kufanya ufisadi badala ya tatizo hilo liwafanye watumie akili zao kwa kasi na ubora zaidi ili kuleta suluhu ya kudumu..

Since then (almost 30 yrs now) sababu zinazotolewa ni zilezile na ahadi ni zilezile lakini tatizo liko palepale..

Mzee baba, Hayati John P. Magufuli alijitajidi kidogo lakini amekufa na kufa na reforms zake. Waliokuja wanaendeleza tatizo tu na story zilezile za wakati wa Mkapa na Jakaya Kikwete zimerudi tena..

In my opinion, FaizaFoxy (mwana CCM huyu) ana hoja ya akili sana na inachohitaji ni kuongezewa nyama tu ktk kuiboresha. Na ofcoz hiyo ndiyo itakuwa suluhu ya kudumu Kwa ishu hii na zingine zote inazohusi maendeleo ya kijamii..

Kwa mfano, si tu Shirika hili livunjwe vunjwe na mamlaka ya usimamizi wa sekta ya nishati iwekwe kwenye mikoa na wilaya...

Hili la kuvunjwa vunjwa ni sawa kabisa.

Lakini kama mfumo wa utawala wa kuteua viongozi DSM au Dodoma na kuletwa na mtu mmoja aitwaye Rais kuja kutawala/kuongoza wananchi wa mikoa husika utaendelea, pendekezo la FaizaFoxy linaweza lisilete tija inayotarajiwa..

Tunataka watawala wa mikoa na wilaya wachaguliwe na wananchi wa mikoa na wilaya husika na wawajibike kwao katika mambo yote ya usimamizi wa utawala na maendeleo ya jamii ya mikoa husika..

Sambamba na hilo☝️☝️, lazima pia mifumo ya mamlaka ya usimamizi wa kifedha kuanzia vyanzo vya mapato (kodi), bajeti na ajira za wafanyakazi wote ziwe mikononi mwa mamlaka ya mikoa na wilaya husika na sio kama ilivyo sasa kwamba, kodi zote, ajira zote ni mpaka DSM au Dodoma iamue ndo baadae Rais (kwa sasa Samia) ndo aamue mikoani na wilayani tupeleke ngapi na amlete nani na kwa wakati gani ili awatawale wenyeji..

Kwa mfumo huu uliopo sasa ni ngumu sana kutoboa kimaendeleo kwa haraka kwa sabb una - encourage impunity na kutowajibika kwa viongozi..!

Suluhu ni kuwepo na mamlaka za serikali za mitaa zilizo huru na kamili kwelikweli na sio usanii huu uliopo sasa wa serikali za mitaa Kwa jina tu lakini maamuzi yote ya kiutawala na kifedha yanatoka DSM au Dodoma..
 
Mkuu, kua mali za umma haiondoi uhalisia wa gharama za umeme.
Motive ya shirika la umma na motive ya kampuni ya mtu binafsi [ private sector] ni tofauti. Shirika la umma linatakiwa lijiendeshe kiufanisi hivyo kutoa huduma kwa bei nafuu lakini bila hasara; unlike the private sector who are always driven by the maximization of profit!
 
Acheni lawama, mama alishasema mwisho wa umeme kukatika ni mwezi wa tatu...waacheni TANESCO watekeleze majukumu yao halali
Wametumwa hao ukweli wanajua kwanini wasisubili miezi 6 waliyopewa Tanesco ikaisha ndio waje na mapendekezo yao?
 
Sikubaliani na wewe.

Hilo unalotaka practically halitawezekana. Kuna mikoa haina vyanzo vya umeme. Yenyewe itaishia kununua kwenye mikoa yenye Ina vyanzo vya umeme. Gharama za umeme mikoa hiyo itakua juu kuliko ile yenye Ina vyanzo.

Hapo tayari ni udhaifu kwamba unagawa shirika lakini mmoja anapata na mwengine anakosa.
 
Ndio ninayosema kila siku kiwango cha upuuzi wa watanzania kinatutosha wenyewe ni watu wakujiandikia upuuzi tu kutoka vichwani kwetu.

Production wise umeme unavyanzo mahususi;; inabidi ueleze kila mkoa uwezo wake wa kuzalisha umeme kwa vyanzo vyake, shared network distribution zake, infrastructure za kuingia (kwa kifupi inataka mjinga mwenzako kuona una, hoja) otherwise the pathetism of what you wrote is beyond a reasonable mind to how things work.

Second Nehemia alishawahi kuwa NED ndani ya TANESCO, based on ‘Corporate Code of Governance’ as a neutral supervisor ulishawahi ona report ya TANESCO kuhusu concerns za; internal control issues, internal audit risk concerns, risk management matters. Hayo mambo yalikuwa sehemu ya majukumu yake kama NED with finance experience.

Tunayoandika yanataka abc kuelewa tunatokea wapi.

Mpaka kukasirika kwa kusoma ujinga; ni kwa sababu tumeshavumilia vya kutosha.

It’s just a shitty country, ambayo hayati Magufuli alikuwa anajaribu kuikombos.

Vinginevyo ukisoma mada ni ujinga mtupu kama huu; mtu anatoa upuuzi tu kutoka kichwani.

I don’t care natwanga tu, I am sick of reading nonsense.

Kutukana hovyo hovyo kunaashiria mapungufu makubwa. Ukiwa na mapungifu mengi, hasa mapungufu ya utulivu wa akili na reasoning, unaishia kutukana hovyo hovyo ukiamini una-compensate vitu ulivyovikosa. Jambo ambalo siyo kweli.

Tuliza akili, argue professionally, sensibly and reasonably. Wengine watakuwa kwenye nafasi ya kujua nani ana ufahamu wa kutosha na nani anafanya argument based on ignorance.

Mleta mada ana hoja, japo siyo lazima kila mkoa kuwa na kampuni yake. Hoja ya msingi ni kwamba, TANESCO, kama yalivyo mashirika mengine yanayosimamiwa na serikali, has miserably failed. Tunahitaji sekta binafsi ipewe hili jukumu, huku tukijua kuwa ni vigumu sana kampuni moja kufanya majukumu yote yatakayosababisha upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa eneo lote la nchi. Hivyo ni vyema kuwa na makampuni binafsi zaidi ya moja. Lakini kutegemea Serikali hii ambayo uteuzi wa wa wakuu wa taasisi za serikali unaangalia zaidi ukada wa CCM kuliko maarifa, ni kusubiria embe chini ya mchongoma.
 
Back
Top Bottom