Lazaro Nyalandu, Mwanaccm pekee aliyepinga Udikteta wa awamu ya 5 kwa vitendo

Lazaro Nyalandu, Mwanaccm pekee aliyepinga Udikteta wa awamu ya 5 kwa vitendo

Nyalandu hakuwa na njaa yakutafuna kodi za wananchi! Ana kauzungu flani na roho yakufikiria wengine!! Kutana na kina mwi guru huyo akikosa uongozi atapiga mayowe,rusha maneno mabaya hata ngumi na atajipendekeza kwa mwenyevyeo mpaka arudi kwenyecheo!!
Kongole zake Nyalandu na tusisahau ananyandua pazuriiii....
 
Tungali tunaendelea na ule mwezi mtukufu wa Mungu , ambao ni mwezi huu wa 3 , fuatilia simulizi hii ya Nyalandu

View attachment 2933903

Pamoja na ukweli kwamba Nyalandu alirejea ccm baada ya Jiwe kuondoka , lakini bado Ukweli uko wazi kwamba ndiye Mwanaccm pekee aliyepinga Udikteta wa kishamba wa Jiwe hadharani , ilikuwa hatari sana kwake , maana angeweza hata kuuliwa kwa kitendo hicho .

Haijawahi kuwa utamaduni wa wanaccm kujivua vyeo kwa sababu ya Uchafu wa kiongozi mkuu , huyu rekodi yake haiwezi kufanana hata na Mrema ambaye alisubiri kwanza apokonywe Cheo ndio atoke , tena baada ya kuahidiwa vyeo vikubwa huko alikoenda .

Mamluki wa Jiwe akiwemo Hamis Kigwangwala alitangaza bungeni kwamba atamshitaki Nyalandu Mahakamani kama sehemu ya vitisho vya kumshughulikia , Lakini hadi Kigwangwala anazeeka hakuwahi kwenda hata kwa mjumbe wa nyumba 10 kumshitaki Nyalandu

Pamoja na kwamba Nyalandu amerejea CCM kwa sababu za kimaisha lakini atabakia kuwa miongoni mwa wanaccm waliomdhalilisha Jiwe hadharani , huyu alipinga ROHO MBAYA YA KINYAMA YA JIWE KUZUIA WANACCM KWENDA KUMUONA LISSU HOSPITALI BAADA YA KUJERUHIWA NA MAMLUKI WALIOTUMWA NA SERIKALI YA JIWE (HII NI KWA MUJIBU WA TUNDU LISSU MWENYEWE) , hata hivyo Mzee Mwinyi (RIP) alikataa unafiki huo na kuamua kwenda Nairobi kumuona Lissu bila kujali lolote (hii ilichagizwa na ucha Mungu wake) , Wanaccm wengine wote waliufyata kwa hofu ya kutekwa na kuuawa .

NITASEMA KWELI DAIMA FITNA KWANGU MWIKO
unaanza dalili za kurudi ccm wewe mama kama unaanza kusifia waliorudi ccm inamaana unajuwa kabisa ccm ndiyo kwenyewe huko chadema mnateseka tu karibu CCM
 
Aliyesema nyalandu ni fisadi anauza wanyama na kugawa vitalu maneno hayo yalitoka kwenye jukwaa la chadema na viongozi wake kwa style ile ile ya lowassa sisi wananchi huwa tunawaamini sana viongozi wa chadema wakituambia jambo vipi leo hii utubadilishie!

..mimi nilikuwa namjibu mchangiaji aliyedai Nyalandu alihusika na lile tukio maarufu la kupakia twiga na wanyama wengine ktk ndege na kuwapeleka Uarabuni. Nimesema Nyalandu hakuhusika kwasababu bado alikuwa hajateuliwa kuwa Waziri wa Maliasili.

..kama kuna kashfa nyingine alihusika nazo uwanja uko huru kuzitaja na mimi binafsi sina ushahidi wa kupinga madai yenu.
 
Nyalandu aliokolewa na Network yake USA , si kwamba hakutakiwa kumalizwa , uliza wakubwa wakueleze vizuri , na hiyo network ndio ilimpa ujasiri wa kuondoka ccm mchana wa jua kali , Nyalandu hakujiondoa ccm usiku
Huko Chadema alikuta nyumbu tuu akaona bora CCM na akaondoka Chadema mchana kweupeee.
 
Ni pale ambapo askari ana risasi chache sana..., adui yupo mbele yake anakenua; ila yeye anatumia risasi zake adimu kuendelea kumcharaza risasi marehemu...

Ingekuwa vema kama huyo marehemu angechalazwa risasi wakati askari huyu ameshashinda vita yupo anakunywa Gahawa na kuangalia what it has been na sio what might have been....
 
Back
Top Bottom