Le Mutuz: Historia ya kweli juu ya maisha yangu (My American experience)

Le Mutuz: Historia ya kweli juu ya maisha yangu (My American experience)

Huyo Peter Lwangisa nimesoma naye boarding enzi za primary. He used to be the most fearsome bully in school. I remember him as a vicious, violent, brutal individual who would beat you up for no reason. His was a reign of terror until the day he left the school. Kama mnaelewana naye huyo basi you guys must be cut from the same cloth.

- Mkuu ulianza na hasira zako na mimi sasa umemgeuzia huyu jamaa ambaye hata kubishana hajui, unawezaje kuwa bully shuleni ukawa kool mtumzima? Unaonekana una hasira sana pole sana ila mtafute adui yako maana humu hayupo ila angalia kwenye kioo utamuona wewe mwenyewe!

le Mutuz
 
- Unauliza majibu Samwel hayumo kwenye equation ya urithi na sio a threat kwa sababu hajasoma sana, tumia akili kidogo ndio maana majuzi nilimuambia my ex wale dada zangu hawana shida naye tena maana walichotaka ni Divorce wakiamini itanimaliza iliposhindwa basi hawana shida naye tena sasa wamewekeza kwa Mange, guys mbona ukisoma vizuri maelezo yapo very clear!,

- Imagine tukiwa kwenye ndoa my step sister alikataa kata kata watoto wangu wasilale kwake, lakini tulipokua in separation wakawa wanaenda kulala kwake niambie unaweza ku reason out na hizo akili?

le Mutuz
Le mutuz Le Mobimba BOMAYE wewe ni Great Thinker , upo smart.
 
Le Mobimba .....
. ktk kitu kitaliweka Jina lako sawa ni hii chapter unayotuandikia William Malecela ni Nani kwenye Taifa hili na umuhimu wake. XWife Pamoja na wale Maadui wako ndio sterling man walikuwa wanakupaka matusi makubwa makubwa bila soni!
Kwa history hii najua sasa umewashinda!
Nadhan sasa hawaelewani! kwa Mshindo huu mzito kabisa.
 
upload_2018-3-2_14-11-14.jpeg

PART 56:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Super Handsome hahaha Sekondari Form Two hii Wabebezz walikua wanajigonga ila sio wengi kama leo hahaha.. Nilikua najiuliza swali moja nimebakiza nini kuendelea kuishi USA? kazini nikaomba ruhusa ya likizo Wiki Mbili nikapanda ndege to Miami Beach kupumzika na kutafakari FACTS kwa makini , kwamba my ex alikua ameshaamua kunikomoa infact alichokua analilia sana ni angalau anilaze Rumande ili apate Ushujaa mbele ya Jamii lakini. Thanks to God kwa mara nyingine tena Jina la Baba yangu likaniokoa tatizo ni kwamba nilikua Too Strong kumuonyesha binadam yoyote kua ninaumia au hata kutingishika kidogo hii ilikua inawaudhi Wanawake kwa Wanaume wanyonge kwenye ile jamii ya Wabongo na ndio kwanza nilikua na gari jipya Nissan Pathfinder ..

Nilikua ninamfuatilia my ex na kundi lake kwa karibu sana bila wao kujua so nilijua kua wanapanga kunipeleka mahakamani kusudi wauchukue mshahara wangu ambao hata wao hawakujua kua ulikua sio kama zamani tena. Kwenye hilo kwa Sheria za USA sikua na ujanja na ndio ungekua mwisho wa furaha ya maisha yangu kule maana sasa ningekua mtumwa wa yule Mwanamke for the rest of my life in USA. Mifano ilikuepo wala sio mambo ya kuhadithiwa. Kuna Mbongo Engineer yalimkuta alihangaika mpaka akalazimika tu kumrudia mkewe akiwa senti moja hana mpaka leo ni mtumwa wa yule Dada ...

Sikuwahi kucheat wala kumpiga my ex lakini hasira aliyokua nayo hasa baada ya kushindwa kuniweka Rumande kama alivyopanga haikua na mfan. Llikizo yangu Miami Beach ikaisha nikarudi New York na uamuzi mzito na mgumu sana kama kawaida ya maisha yangu sijawahi kua na tatizo na kufanya maamuzi magumu na kwa wakati muafaka kama nilivyoamua kwenda Majuu ulikua ni uamuzi mzito sana na sikumshirikisha Mtu now again nikaamua maamuzi magumu sana ambayo yalikuja kuwashangaza na kuwaumiza my ex na kundi lake lote.

Mpaka leo bado wana Chuki isiyoisha ni uamuzi ulioiacha Jumuiya nzima ya Wabongo New York na hata Wabongo wote USA nzima mpaka leo bado wanao huo mshangao kwani ni uamuzi ambao haukuwa na historia nyuma yake ni almost nilikua wa kwanza kuufanya so kwanza nilienda kazini kwa bosi Mr. Jack nikamfahamisha uamuzi wangu mzungu akaanza kulia!
...ITAENDELEA
 
ilianza kama vichekesho na story ya majigambo ikaja kuwa ya kutafuta sympathy kwetu kwa kale kavideo,sasa imeturn na kuwa habari ya kututoa au kukaribia kututoa machozi.Mkuu heshima kwako na pole kwa uliyopitia

- Tatizo kwenye maisha yangu sijawahi kutafuta sympathy na yoyote ningekua nisingefika nilipo, soma habari yangu hakuna mahali utakuta nilitafuta ushauri NEVER! Kale kavideo was nothing to me kwa sababu Sheria niliyojipangia in my life ni as long as nimeamka salama I am ok,

- Nitakupa mfano mdogo wa mimi sio mtu wa sympathy, nikiwa mdogo ndugu yangu wa kiume Marehemu Senyagwa alifariki Serikali ikatoa ndege ya Jeshi kuwapeleka waombolezaji walio karibu na marehemu, kwenye kutaja majina ya watakakwenda nayo sikuwemo, hahahahahaha na walioandika walikua wanajua kua nipo, niambie ningekua mtu wa kulia lia ningefanyaje? lakini nilipanda gari la washikaji niakenda nikamzika ndugu yangu nikarudi maisha yanaenda mpaka leo,

- So please naomba ufute kauli za Sympathy na kavideo cause sio mambo yangu, kama ni Video nilikua na uwezo wa kuikana na hakuna ambaye angethibitisha kua ni mimi, cause mimi ndiye niliyemshauri kukataa zile picha zake na akakataa mpaka mwisho, so guy nielewe mimi sio mtu wa kulia lia na kama sio my ex kunichafua sana na mitandao nisingeandika this way ila amenilazimisha mwenyewe.

le Mutuz
 
upload_2018-3-2_14-14-37.jpeg

PART 57:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"
Picha hii nilikua kati kati ya maumivu ya ajabu ..In the end uamuzi wangu wa mwisho ulikua USA kwa ujumla nimepata AKILI KUBWAZ basi pesa zote nimelipia Elimu na Kutunza Familia Miaka 5 ya kuishi na mke na watoto 2 bila kazi. Kwa mlioishi Majuu mnajua one income watu 4 majuu ni impossible na kipindi chote cha maumivu pesa hazikua na thamani tena ila nikaja kugundua bank nimebaki na Dola 2000 tu lakini sikujali. Kwa mara ya kwanza nikajifunza umuhimu wa kua na AMANI MAISHANI kumbe Amani haina price cause uamuzi wangu mgumu ulikua ni KUTAFUTA AMANI kwanza ili kuacha kuishi kwa wasi wasi ugenini ..

KURUDI NYUMBANI BONGO ndio uliokua uamuzi wangu mgumu na sababu moja ya msingi ni nilikua ninakataa kua mtumwa wa my ex kwa kulazimishwa na Sheria lakini nikajiuliza swali Watoto itakuaje? na Nikirudi Bongo nitashambuliwa sana kua nimekimbia kuogopa kuchukuliwa pesa but nikajiuliza ipi bora kuchekwa nikiwa na Amani au kusifiwa nikiwa sina amani? nilijua my ex na kundi lake hawakulifkiria kabisa la mimi kurudi nyumbani wao furaha yao ilikua wameshanipata now it is only a matter of time kabla hawajanikomoa .

Nilimfahamisha mzungu kua ninaacha kazi siku ile ile ninarudi Tanzania FOR GOOD. Machozi yakaanza kumtoka mzungu akanipeleka kwa Bosi mkubwa Mr. Reney mzungu mkubwa akabadilika rangi akawa mwekundu ila wakaishia kunikubalia. Mzungu akanipa mshahara wa Wiki 4 akawapigia Union ilikua Jumatatu nikatumia siku 3 kuweka sawa mambo ya my penshion na pesa za kukatwa kulipia watoto nikaweka sawa nikakata one way tiketi ya Swiss Air now ilikua Jumatano sikumwambia Mbongo yoyote. Nikalipia madeni ya Shule nikafanya shopping ya mwisho nyumba nzuri gari zuri havikua na faida yoyote mbele ya kukosa Amani Alhamis

Kwa mara ya kwanza nikamfahamisha Dada mmoja bosi wa my ex kazini kwake na ndiye niliyekua ninamtumia ku cummunicate na my ex kwa sababu kwenye makubaliano ya Divorce niliomba Sharti la kutokuongea tena na my ex ikibidi nitamtumia huyu Dada bosi wake na tulikubaliana vizuri tu na kweli mpaka leo Mwaka wa 7 sijawahi kumsemesha ingawa amejaribu mara nyingi lakini nimekataa Ijumaa nikapanga mabegi yangu 2 tayari kwa safari ilipofika Ijumaa

...ITAENDELEA
 
Le Mobimba .....
. ktk kitu kitaliweka Jina lako sawa ni hii chapter unayotuandikia William Malecela ni Nani kwenye Taifa hili na umuhimu wake. XWife Pamoja na wale Maadui wako ndio sterling man walikuwa wanakupaka matusi makubwa makubwa bila soni!
Kwa history hii najua sasa umewashinda!
Nadhan sasa hawaelewani! kwa Mshindo huu mzito kabisa.

- Well, cha msingi ilikua ni kuweka sawa ukweli kwanza, mimi sio anybody wala anything isipokua ni raia mwema ninayeishi maisha niliyoyachagua na ninayoyaweza, ila nina a lot to teach vijana wadogo wanaoanza maisha that is all,

- Kwa mfano ni jinsi nilivyorudi na Dola 1,000 na leo nimezigeuza kua a serious business sasa hivi by Jumatatu ninafungua Online Radio acha kua na kampuni kabisa ya Social MEdia, nafikiri someone needs to know that

le Mutuz
 
upload_2018-3-2_14-26-57.jpeg

PART 58:- "MY AMERICAN EXEPRIENCE"

Picha ya Coupon niliyonunulia tiketi na Hotel at Zurich ...Kwa kawaida kabla ya kufanya maamuzi yangu magumu hua ni muhimu sana natafuta JUSTIFICATIONS ambazo ni FACTS ninaziweza kuzisimamia hata mbele ya Watu wenye akili kua ilikua ni lazima nifanye nilichokifanya Uamuzi wa kurudi Bongo ulikua na tatizo moja kubwa sana Watoto! ...but nikaanza ku reason out kua hata nikibaki Watoto hawatakua wangu tena yatakua maisha ya kugombea watoto mahakamani kila siku, nitapangiwa muda wa kuwa nao na Mwaka Mmoja na Nusu wa Separation watoto wangu walikua wameshabadilika ukiwaona tu unajua wana tatizo.

Mama yao alikua anahangaika kuwa train ili wa fit anachotaka yaani kuonyesha Wanampenda yeye kuliko mimi a nonsense theory cause ninajua from Criminology Studies kua Watoto ni watu wenye akili sana za their Security kuliko hata sisi watuwazima ikitokea a choice ya kuchagua baina ya Baba na Mama yupi wa kuishi naye watoto automatically 99.1% watachagua Mama tu cause ndiye anayewalisha na kuwa nao wakati wote Mwanaume akiwa kazini lakini watoto wakikua wanaamua tofauti sio kwamba hawajui kua mama yako anawavuruga ...

Safari ilikua imeiva Ijumaa tu kesho Jumamosi safari kwa bahati ikatokea Concert la Mzee Yusuph Ijumaa usiku nikaenda na kama kawa my ex akaingia na kundi lake wakiwa na jeuri nzito sana usoni mwao nilikaa pembeni nawachora tu nawacheka kimoyo moyo kua kesho mtapata mshituko wa ajabu hahaha nilikua na mshikaji wangu Peter kama kawaida hata yeye sijamuambia kua kesho ni balaaa ...uchunguzi wangu wa siri ni kwamba my ex na wenzake walishaenda mahakamani na Wanasheria walishapata makaratasi ya kunifikisha mahakani kudai mshahara wangu nikasikia furaha waliokua nayo makaratasi ninatakiwa kupewa Jumatatu.

Nasikia my ex alishaanza kutafuta nyumba kubwa ya kuishi kwa kutumia mshahara wangu hahahaha nilicheka sana mwenyewe kimoyo moyo ingawa bado nilikua napigana na nafsi yangu kuhusu watoto kwenye makaratasi ya Divorce my ex alidai lazima abaki na watoto na Sheria inamruhusu then likanijia wazo la nitawafanyia nini watoto kama mimi mwenyewe sipo sawa! baada ya kulipia lipia kila kitu muhimu nikabaki na Dola 1500 tu!

..ITAENDELEA
 
View attachment 703634
PART 58:- "MY AMERICAN EXEPRIENCE"

Picha ya Coupon niliyonunulia tiketi na Hotel at Zurich ...Kwa kawaida kabla ya kufanya maamuzi yangu magumu hua ni muhimu sana natafuta JUSTIFICATIONS ambazo ni FACTS ninaziweza kuzisimamia hata mbele ya Watu wenye akili kua ilikua ni lazima nifanye nilichokifanya Uamuzi wa kurudi Bongo ulikua na tatizo moja kubwa sana Watoto! ...but nikaanza ku reason out kua hata nikibaki Watoto hawatakua wangu tena yatakua maisha ya kugombea watoto mahakamani kila siku, nitapangiwa muda wa kuwa nao na Mwaka Mmoja na Nusu wa Separation watoto wangu walikua wameshabadilika ukiwaona tu unajua wana tatizo.

Mama yao alikua anahangaika kuwa train ili wa fit anachotaka yaani kuonyesha Wanampenda yeye kuliko mimi a nonsense theory cause ninajua from Criminology Studies kua Watoto ni watu wenye akili sana za their Security kuliko hata sisi watuwazima ikitokea a choice ya kuchagua baina ya Baba na Mama yupi wa kuishi naye watoto automatically 99.1% watachagua Mama tu cause ndiye anayewalisha na kuwa nao wakati wote Mwanaume akiwa kazini lakini watoto wakikua wanaamua tofauti sio kwamba hawajui kua mama yako anawavuruga ...

Safari ilikua imeiva Ijumaa tu kesho Jumamosi safari kwa bahati ikatokea Concert la Mzee Yusuph Ijumaa usiku nikaenda na kama kawa my ex akaingia na kundi lake wakiwa na jeuri nzito sana usoni mwao nilikaa pembeni nawachora tu nawacheka kimoyo moyo kua kesho mtapata mshituko wa ajabu hahaha nilikua na mshikaji wangu Peter kama kawaida hata yeye sijamuambia kua kesho ni balaaa ...uchunguzi wangu wa siri ni kwamba my ex na wenzake walishaenda mahakamani na Wanasheria walishapata makaratasi ya kunifikisha mahakani kudai mshahara wangu nikasikia furaha waliokua nayo makaratasi ninatakiwa kupewa Jumatatu.

Nasikia my ex alishaanza kutafuta nyumba kubwa ya kuishi kwa kutumia mshahara wangu hahahaha nilicheka sana mwenyewe kimoyo moyo ingawa bado nilikua napigana na nafsi yangu kuhusu watoto kwenye makaratasi ya Divorce my ex alidai lazima abaki na watoto na Sheria inamruhusu then likanijia wazo la nitawafanyia nini watoto kama mimi mwenyewe sipo sawa! baada ya kulipia lipia kila kitu muhimu nikabaki na Dola 1500 tu!

..ITAENDELEA
Story yako inasisimua sana aisee........hongera kwa maamuzi magumu!
 
upload_2018-3-2_14-51-12.jpeg

PART 59:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Picha hii ni Ijumaa ya mwisho in USA ...I was tired now kwa sababu nilijua my ex na genge lake wanayo summons ya mahakama nikifanya mchezo wakijua kua ninaondoka watanizuia Airport sitaruhusiwa na Uhamiaji kuondoka so nikaitumia Ijumaa nzima kuwa Confuse Wabongo nikatangaza kua natayarisha event ya Music nitakayoifanya in Two weeks to come nilikua najiwekea kinga incase akijua mtu kua naondoka kesho yake akasema watu watamshangaa mbona ninatayarisha Event ...hahahaha...

Now Jioni yake yaani Ijumaa Balozi Mahiga Waziri wa sasa wa Nje aliyekua Balozi kule UN akatuita mimi na my ex nyumbani kwake ili kujaribu kutupatanisha, hakujua tulishafikia uamuzi wa kuachana alianza na kumuuliza Swali moja tu my ex alimuambia "Neema matatizo mliyonayo najua yanaanzia kwenye biashara unayoifanya naomba uniambie hiyo Biashara ni yako wewe binafsi, ni yenu wote wawili au ni ya mumeo?" akaongeza kabla hujajibu "Mimi siwezi kua na Biashara ambayo haieleweki ni yangu au ya mke wangu ni lazima iwe yetu wote ikiwa tofauti ninamuacha mke wangu siku hiyo hiyo" "Sasa naomba niambie biashara ni ya nani?" kilikua ni kama kibao cha moto my ex alibakia mdomo wazi hana jibu cause for Sure nilimpa mtaji wa Dola 5,000 lakini hata mimi mwenyewe sikujua baadaye biashara ni ya nani! ...

Balozi hakutaka habari ndefu sana akatuambia ameshajua tatizo lilipo so haikua hata na sababu kuongea zaidi lakini my ex akaomba kuongea na kuanza kumtukana Baba yangu mzazi matusi mazito mazito kwamba hafai ndiye chanzo cha matatizo mengi baina yetu ...hahahaha that was the biggest joke of my life Baba yangu alilala macho kumtafutia kazi ya Ubalozi leo hafai Duh! .anyways I maintained my kool nilimuambia neno moja tu kua "Siku utakapopata mume imara kama mimi tena nifahamishe nitakuchangia mchango wa harusi" nikamuaga Balozi nikaondoka ndio tukakutana tena kwenye Taarabu na my ex na genge lake (leo my ex ni mke wa Pili wa mtu na amebadili Dini na kua Muisilam) hahaha

Lord have mercy...I mean miezi 3 baada ya kuoana niligundua mambo 2 kuhusu my ex ni Mvivu na Ana roho mbaya sana nilijua uvivu ni kwa sababu ya kuzaliwa kwenye utajiri ila la pili nikamuuliza straight....ITAENDELEA!
 
upload_2018-3-2_15-2-22.jpeg

PART 60:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"
Picha hii kabla sijaoa I was a Happy man ...My ex alinijibu kua roho mbaya ni ya Mama yake mzazi Baba yake hakua nayo I mean binadam wote tuna Good side and Bad ila kuna wengine Shetani anawazidia like my ex ..I am not standing here na kujifanya mkamilifu HAPANA ninayo mapungufu na kubwa lililokua linamkera sana my ex ni uwezo wangu wa kujua mambo mengi sana nina uwezo wa kuona dalili na kutoa tahadhari kwa litakalofuatia.

Kwa mfano kuna wakati tulikua na House Girl mbongo siku moja akaamua kutoroka hakurudi tena nikamuonya my ex usimuongelee negatively kwa yeyote cause habari zitamfikia tu kwa sababu hatukua tunamlipa kama Sheria ya USA inavyotaka anaweza kutingiza matatani ...my ex kama kawaida hakusikia maana mimi najifanya najua sana siku moja kuna Mama mmoja wa kizungu akapiga simu ya nyumbani kumuulizia kuwa mbona hamuoni tena na alikua anamsafishia nyumba my ex akaanza kumuongelea negatively kua katoroka anatafutwa na Uhamiaji na maneno mengi sana yasiyohusu ..

kumbe yule Mama ni Mwanasheria wa Haki za Binadam baada ya siku 3 yule House Girl alienda kumsafishia nyumba mama wa kizungu akamuambia yote yaliyosemwa na my ex ohhh my God msichana kwa panic akaanza kufunguka kila kitu hasa kuhusu malipo mzungu akampigia my ex na kumtaka afike ofisini kwake anataka kutufungulia kesi my ex akanificha lakini bahati nzuri msichana mmoja mbongo alikua anajua yule House Girl alipo walikua close yule msichana akanishitua kuhusu kilichojiri nikamuomba amuite yule House Girl nikutane naye akatoa sharti nisije na my ex nikakubali tukakutana nikamuomba sana radhi akaniambia kama isingekua wewe mke wako angeshika adabu.

Akaniambia nimetoroka kwa sababu ya mke wako mvivu mno.well nikaenda naye kwa mzungu akamuomba amsamehe mke wangu kwa niaba yangu Mama wa kizungu akanionya niongee na my ex tusirudie tena kuleta House Girl nikamshukuru sana Mungu ila sikumuambia kitu my ex ambaye alikuja kugundua yote na kuomba sana radhi kwangu kitu ambacho kilikua ni kawaida sana in our marriage tatizo kubwa ni we were too far apart at Uwezo wa kufikiri na kuona mbali au kukubali ukweli unapotokea ambalo ni tatizo langu namba moja KUKUBALI UKWELI

..ITAENDELEA
 
upload_2018-3-2_15-41-37.jpeg

PART 61:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"

Picha hii ni Wiki ya pili Bongo baada ya kurudi...I know for a Fact kua I am American in Sipirit wala sio siri mimi ni Mbishi na Super Stubborn simuamini anyone in my life NINAMUAMINI MUNGU na again sijawahi kua na tatizo la kukubali the UGLY TRUTH na anytime sijawahi kuamini maneno ya mtu bila kujaribu mwenyewe na kutafuta FACTS mwenyewe ....SIJAWAHI KUNYWA POMBE WALA KUVUTA SIGARA IN MY LIFE so my Brain is Sober and Clean as you can imagine kumjua kwangu sana Mungu kwa karibu kumenifanya nikose FEAR OF ANYTHING I am a number one believer of TIMMING.

Kwa mfano my ex amenitukana sana kwenye mitandao na kwa muda mrefu sana alianzia Jamiiforums alipoona hainisumbui akahamia kwa Mange wakati Marehemu Mama yangu amefariki ndipo walipoanza kushirikiana kunitukana na hasa kumtukana Marehemu Mama yangu now kumjibu kwa lugha yake nilikua siwezi Unanzaje kumvua nguo mama wa watoto wako? na kuna siku akampa Mange my copy of Passport I was shocked lakini sikuwahi kumuonyesha kua nimeshituka ila niliamua kunyamaza kusubiri my day hii story ambayo sijamtukana ninaamini imenisaidia kujibu matusi mengi aliyonitukana sana na kwa muda mrefu ...

Again sijasimama hapa kuomba SYMPATHY hapana NIMEWEKA THE TRUTH kama nilivyofundishwa na the Americans ni uamuzi wako msomaji kuamua ukweli upo wapi kwenye matusi ya my ex au this Story na honestly KITABU CHANGU KITAMALIZA UBISHI WOTE ...guys ukizaliwa Mwanaume jitambue na Ujiamini Mungu anasema Mwanamke ni a "Weak Vessel" ndio maana Shetani alimtumia Eva alishindwa kwa Adamu sio Wanawake wote ni mburulazz ila wengi they are..

Saa Tisa za Usiku Jumamosi Asubuhi nilimpigia simu rafiki yangu Peter kama kawaida nikamuambia nina jambo kubwa sana la kumwambia Asubuhi ilipofika nikamuambia nitamuhitaji anipeleke Airport JFK nina mabegi 2 nasafirisha Gari langu nikalipeleka nilipolinunua in the Bronx nikawambia lina matatizo sana waliangalie na ninasafiri nitalipitia Jumatano ilipofika Saa Nane mchana Peter alikua chini ananisubiri namuona toka dirishani gorofani nikapiga magoti chini na kumuomba Mungu kwa mara ya mwisho nikapakiza mabegi kwenye Limousine ya Peter nikamuomba awapigie watoto wangu

..ITAENDELEA
 
View attachment 703143

PART 50:- "MY AMERICAN EXPERIENCE"


Picha ni Marehemu Mama yangu mzazi akiwa London ambako alikua akienda mara kwa mara...Matatizo ya Ndoa na Matatizo ya kazi yote kwa mpigo nikaanza kumkumbuka Mama yangu siku moja aliingia Chumbani kwangu ghafla nikiwa mdogo ninakaa kwa Uncle Lusinde, akanikuta na Cash nyingi sana alipigwa na mshangao akaniambia "William unapenda maisha makubwa sana utayapata lakini yatakugharimu sana" .

Infact Mama yangu mzazi hakutaka kabisa kusikia habari za kumuoa mke wangu na hata Baba yangu hakutaka na Dada yangu mmoja pamoja uadui wetu bado na yeye alipinga openly. Wazazi wangu ya kumkataa waliyasemea in Private lakini Dada yangu alimuambia yeye mwenyewe kabla ya kufunga ndoa kua haungi mkono ndoa cause anajua kua nitakuja kuumia tu lakini wote in the end wakaheshimu uamuzi wangu so now yamenikuta ninamkimbilia nani? ...

Marehemu Mama yangu amechafuliwa sana na my ex wife na anaowatumia Mama yangu alikua Miss Tukuyu, akawa Miss Mbeya, then Miss Tanzania na Miss East Africa baadaye Mwalimu Baba wa Taifa alimtumia sana kwenye kujenga UWT na Mama Sophia Kawawa ninakumbuka sana nikiwa mdogo akawa Muwakilishi wa UWT Taifa Mikutano ya Kimataifa sawa hakua na Elimu kubwa sana lakini alikulia Malawi alikua na uwezo wa kuongea Fluent English alikua anasafiri all the times nje ya Nchi ...lakini kwa makusudi kabisa ametukanwa sana kwamba eti alikua ni muhudumu wa Gesti ...

Marehemu Mama yangu alikua ni mfanyakazi wa NBC tawi la Clock Tower kwa muda mrefu sana huku akiwa ni Kiongozi wa UWT Taifa alijenga makazi mazuri sana Kigamboni siku moja Jeshi wakachukua lile eneo na kumlipa pesa ndefu sana akajenga Nyumba kubwa na Shamba Minazi Mirefu/Ukonga ...lakini ukisoma matusi ya my ex kwa mama yangu hutaamini kua anyezungumziwa ni huyu Marehemu Mama yangu aliyekua anasafiri nje kila wakati ....

Sawa sikatai kua in the end hakuwa na maisha mazuri sana kama aliyokua nayo zamani lakini ilitokana na matatizo mengi aliyoyapitia mimi nikiwa nje ambayo yalimvuruga sana kisaikilojia na ambayo hayakunihusu na ndio yaliyompelekea kuuza kila kitu na kuhamia Tunduma by the time ninarudi nikamkuta huko!

.....ITAENDELEA
Dah episode hii imeniumiza sana
 
Back
Top Bottom