- hahahaha hapo nilikua Dubai kwenye mapumziko, I mean sijawahi kujaribu kuwaelewa Wabongo wengi sana ambao hawana maisha lakini wapo mbele kulilia maisha ya wengine.
- Nimkwenda Belgium, kule nimetumia Miaka 5 ya kusoma na kurudi Bongo nikajenga nyumba jirani na Mzee Apiyo ambaye baadaye niliiuza nikaongeza pesa zangu za mtaani nikaenda USA nikaishi Miaka 25 ambayo 10 niliitumia kusoma. Nikarudi Bongo na Dola 1000, 500 nikanunua Laptop ambayo ndiyo nilifungulia Blog na kuanza kupiga pesa za matangazo, nilianza na Elfu Tano mpaka leo Ninapiga Millions. Nikafungua Kampuni ambayo leo inaajiri vijana 10, 6 kati yao wamemaliza Vyuo Vikuu, nimefanikiwa kuwa na Apartment with 3 Bedrooms downtown Posta, nina Ofisi yangu downtown Posta, nina gari la kunitoa Point A to B, ninajilipia maisha yangu, ninasaifiri kila wakati Kikazi na kula batazz sometimes. Kila Mwisho wa Mwaka ninaenda Nje kupumzika, Mwaka juzi nilienda South Africa Wiki 2 kupumzika, Mwaka Jana nikaenda China Hong Kong na Macau Kupumzika, Mwaka huu nimeenda Dubai kupumzika for 2 Weeks,
- Eti humu JF ninaambiwa na Life failure? huwa naishia kucheka sana sana maana sijawahi kuona binadam mbumbumbu kama wengi humu ndani, I mean nina nyumba na shamba Kinyerezi na nina Plot Mbweni, lakini kwangu cha msingi ni Quality ya maisha ninayoishi.
- Kumbuka niliporudi Bongo for Good Miaka 6 iliyopita sikuwa ninamfahamu mtu hapa mjini, lakini ni my Social Media works ndio zimenifanya leo ninafahamiana na kila mtu, Masikini na Matajiri wake kwa waume. Now ninalishagundua kua Masikini wenzangu wengi urafiki wangu na Matajiri unawasumbua sana hahahahaha lakini it is what it is kila mtu na maisha yake, honestly guys mimi mpaka leo hua naamini bado nipo USA ndio maana hua sina muda na mtu wala maneno ya kijinga jinga, akili yangu ni kubwa sana that sina muda wa kusikiliza ujinga wala kuujali,
- Msimamo wangu ya Kisiasa ni ninaunga mkono CCM kwa facts, ndilo kosa langu kubwa humu JF lakini I love JF maana Skills zangu za Social Media nilizipatia hapa na umaarufu wangu wa Social Media umeanzia hapa enzi zile watoto wadogo wengi humu mlikua hmajazaliwa, so guys kwa nini unahangaikia maisha ya mtu kama mimi ambaye nipo sawa ninaishi ninavyotaka na wewe huna maisha? Kumbuka binadam mwenye maisha hawezi kua na muda wa kujua maisha ya mtu asiyemjua, so poleni sana haters maana hapa kwangu mmekutana na ukuta hahahahahaha
- "MY AMERICAN EXPERIENCE" ni mwanzo tu bado nitaandika kuhusu Miaka 6 back in bongo, kuna "MY INSTAGRAM EXPERIENCE" BADO ninataka kuweka wazi "MY INSTAGRAM DATING EXPERIENCE" na katika Vitabu vyote hivi ni cha "MY INSTAGRAM DATINNG EXPERIENCE" ndio kitakuwa namba moja I know that maana nitawashangaza sana wapiga kelele the life I have lived in Instagram for the last 3 years of my fame, angalia unayejifanya kimbele mbele sana usije kukuta mama yako mzazi ameshawahi kuwa victim au dada yako, hahahahahahaha
- Guys bakisha maneno hujui lolote zaidi ya kujidanganya unajua ukweli wakati hujui kitu, tulia uelimishwe
Le Mutuz Mobimba! ...Le Mutuz Nye! Nye! Nye!