Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

...Si bora ukae kwenye foleni, baadae upate hiyo ration yako/yenu. Unaweza kaa, foleni ndio imetoa wanne, mnaambiwa "unga wa ngano umeisha". Dah, chapati ilikuwa anasa!

...Acha sukari au mchele. Unakumbuka sabuni nayo ilikuwa shida?
Mara nyingi, mchele na sukari vilipatikana kwa magendo majumbani mwa watu.
Walanguzi walikuwa wakitazama au kuangalia huku na kule kabla ya kukupimia kibaba cha sukari, na wakati mwingine vibaba vyenyewe vilikuwa “mkude”.

Teh teh teh!!
 
Muda mfupi tu baada ya Mwinyi kuingia madarakani na kubadili mtazamo wetu wa kiuchumi, mambo yakaanza kubadilika kiasi cha kuwashangaza watu. Magenge ya ulanguzi yakatoweka baada ya bidhaa kupatikana kwa wingi.

Watanzania wakaanza kufanya biashara na nchi nyingine, waliokwenda Kenya kupeleka machungwa, na wao kurudi na sabani za kufulia na kuogea, waliokwenda Uganda, waliokwenda Uarabuni, Ulaya, Marekani, alimuradi kila mmoja alikwenda alikotaka.

Soko la bidhaa mbalimbali likashamiri. Badala ya watu kutafuta bidhaa, bidhaa zikatafuta watu. Nguo mpya za dukani bwerere, mitumba bwerere, sabuni kibao, fegi hahahah teletele, magari makubwa na madogo kibao, Televisheni kibao, Radio kibao.
mkuu,kipindi cha mzee ruksa,sukari ili adimika kama sasa?
 
more please

akina Pasco , Mkandara , william malecela, ritz, mohammed said njooni mtupe elimu

ilikuwaje mtu wa Kisarawe kama sijakosea akaja kuwa rais wa zanzibar kisha na rais wa Tanzania?

Tunaomba wasifu wake familia yake, alikosoma, maandishi yake, etc...

Kwa nini anaonekana ametelekezwa kwa maana hakuna taasisi au vitabu au vitu vyenye kumtambulisha kitaifa zaidi tofauti na viongozi wengine kama akina Mkapa na JK na Nyerere?
...Ngoja nisaidie kuwaita.

...Ni kweli, kitabu cha zama zake kinahitajika.
 
Mkuu tulizana kwenye huu uzi utapata darsa la bure litakupa mwanga nakushauri kuwa msomaji ufyonze ilm..

Siyo sukari tu sabuni, mafuta, nguo, mchele, ngano, maharage, mahindi, na vyakula vingine vingi.
mkuu,mbona utawala huu una viashiria vyote vya uko mliko kuwa!hivi tukianza kupanga foleni,wala chipsi na chili sosi wataweza kupimana ubavu na wala miogo,sembe,magimbi na ugari wa muhogo?ee Mungu epushia mbali!
 
KIkubwa alichofeli ni KUKUSANYA KODI na ndipo ilimbidi Mkapa alipoingia aanzishe TRA.

RUKSA RUKSA ilikuwa RUKSA kwlei kweli watu walikuwa wanahela mbaya na vitu vilipatikana kwelikweli.( Mfano w ahili ni show ya Kanda Bongo Man ndani ya Kilimanjaro Hotel Miaka hiyo ya 90 kiingilio ilikuwa 100,000/= na bado ilijaza)

Nyerere alimpiga dongo sana kuwa anashahuriwa na Mkewe au tuseme wake zake.
 
...Si bora ukae kwenye foleni, baadae upate hiyo ration yako/yenu. Unaweza kaa, foleni ndio imetoa wanne, mnaambiwa "unga wa ngano umeisha". Dah, chapati ilikuwa anasa!

...Acha sukari au mchele. Unakumbuka sabuni nayo ilikuwa shida?
sio sukari na mchele tu mpaka dawa ya mbu ilikuwa hanasa ele dawa ya mbu ya coil ulikuwa unaikata vipande vipande na kuiuza kwa wale unaowafahamu ole wako mgambo au Jkt wa kipindi hicho wakukamate utaomba ardhi ipasuke ili uingie mzima mzima kwa jinsi utakavyopata mkong'oto wa kufa mtu
 
...Ndio, ila inategemea ulikuwa wa tabaka gani. Wengi walilalia mikeka, ngozi na vitu vya namna hiyo, huko vijijini.


...Tusi generalize mambo.


...Chawa na kunguni? Hao walikuwa wana familia. Point is, tumetoka mbali.


...Acha Ujinga!
Tumetoka mbali sana unakumbuka hizi.

IMG_142323901161642.jpeg


IMG_216372494164926.jpeg
 
home mkinywa chai na mkate wa siha/boflo mnaoneka matajiriii hakika kipindi hicho sitokaa nikisahau
 
Mimi swali langu sijapata jibu mpaka leo, ilikuwaje Mwinyi kuwa Rais wa Zanzibar wakati Kazaliwa mkuranga mkoa pwani? Vigezo gani vilitumika?
 
Back
Top Bottom