Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Legacy ya Rais Ali Hassan Mwinyi (91 years) ni nini?

Mwinyi alikuwa tofauti kabisa na Nyerere. Mwalimu alikuwa kwa kiasi fulani very simple, aliishi maisha rahisi sana.

Nakumbuka enzi zile za awamu ya kwanza, kulikuwa na nyumba fulani ambayo ilikuwa pale mbele ya ile ofisi ya msajili wa vyama vya siasa, kama unaelekea wizara ya fedha.

Mwenye ile nyumba alikuwa anafuga mbuzi zaidi ya mia moja, halafu anawaachia asubuhi watembee kutafuta majani, basi wakawa wanapenda kula zile nyasi zilizo pembeni ya Ikulu, wakati wakielekea maeneo ya ocean road.

Halafu jioni wanarudishwa nyumbani. Sisi tuliona poa tu kwa sababu ya akili za kitoto, lakini yale yalikuwa ni mambo yanayofanyika jirani kabisa ya Ikulu!. Na hakuna mtu aliyeonyesha kujali, very simple life enzi za Mwalimu Nyerere.
 
Tunamshkuru mengi tumeyajua chini ya uongozi wake,tv ,nguo mpya za dukani,kuondoka kwa ugawaji ,rtc,nk. Nakushuhudia kuja kwa kina Mo ,Azania, Azam,nk amefanya aliofanya na amearibu alioaribu.namsifu tu kwa kuwalea watoto wake wasiwe malimbukeni na mafisadi kama wengine
 
Ali%20Hassan%20Mwinyi.jpg



Rais mtaafu Mzee ALI HASSAN MWINYI ambaye nadhani ki historia ni mmoja ya watu wachache sana duniani ambao waliwahi kuwa rais wa nchi mbili tofauti. Al Hajj Mwinyi aliwahi kuwa Rais wa Zanzibar na Tanzania pia leo ametimiza miaka 91 toka azaliwe.

Je GREAT THINKERS wa JAMIIFORUMS mnaweza kutupatia dondoo za legacy yake na cha kujiuliza je mnadhani hawa watawala tulionao wangejifunza nini toka kwa Mzee Ali Hassan Mwinyi?
mnafiki tu huyo ndio akazabwa kibao
 
mnafiki tu huyo ndio akazabwa kibao
Wacha bangi zako wee
Unaafiki wa huyu mzee upi.
Ukijua ni jinsi gani nchi hii inapaswa kumuheshimu na kumuenzi huyu mzee usingeleta bangi zako hapa.

Long live rais ali hassan mwinyi mzee ruksa
 
Naona wachangiaji wengi ktk uzi huu wanasifu sera za uchumi za Mwinyi huku wakiponda sera za uchumi za mwl Nyerere,

kwangu mimi naona hili sio sahihi kwa sababu mwl nyerere alikuwa sahihi kupiga marufuku bidhaa kutoka nje ili watanzania tutumie bidhaa tunazozalisha wenyewe ktk viwanda vyetu hivyo kuinua uchumi wa nchi.

Nadhani kilichokosekana ktk utawala wa mwl Nyerere ili kulinda sera zake na wale waliopewa kuzisimamia ni sheria kali za kuwaadhibu wale waliopewa dhamana ya kuzisimamia utekelezaji wa sera hizo,

alikuwa rafiki wa china sijui kwa nini hakujifunza sheria za china zilizo kali kwa wale wote wabadhilifu wa mali za uma.

ambao waligeuka miungu watu ktk maeneo mengi ya nchi kwani hata wakiharibu walikuwa hawaguswi.

nadhani badala ya mwinyi kuifanya nchi yetu kuwa dampo la bidhaa feki kutoka nje,
badala yake angeongeza uzalishaji viwandani ili bidhaa zizalishwe kwa wingi na kuondoa uhaba wa bidhaa kwa wananchi.

matokeo ya sera za mwinyi ndio haya yaliyosababisha viwanda vyetu kufa na wananchi kukosa ajira na sasa serikali mpya inajitahidi kuvifufua upya.

mumusifu pia kwa kuua viwanda vyetu.
 
Kipindi cha Mzee Mwinyi hata fedha ilianza kuzunguka miongoni mwa wananchi wengi. Rushwa nayo ilichukua nafasi yake Kwa kiasi Fulani. Hata hivyo maisha hayakua makali saaana. Kwa upande wa Zanzibar ilikua pigo kubwa sana kuondolewa rais Mwinyi
 
Naona wachangiaji wengi ktk uzi huu wanasifu sera za uchumi za Mwinyi huku wakiponda sera za uchumi za mwl Nyerere,

kwangu mimi naona hili sio sahihi kwa sababu mwl nyerere alikuwa sahihi kupiga marufuku bidhaa kutoka nje ili watanzania tutumie bidhaa tunazozalisha wenyewe ktk viwanda vyetu hivyo kuinua uchumi wa nchi.

Nadhani kilichokosekana ktk utawala wa mwl Nyerere ili kulinda sera zake na wale waliopewa kuzisimamia ni sheria kali za kuwaadhibu wale waliopewa dhamana ya kuzisimamia utekelezaji wa sera hizo,

alikuwa rafiki wa china sijui kwa nini hakujifunza sheria za china zilizo kali kwa wale wote wabadhilifu wa mali za uma.

ambao waligeuka miungu watu ktk maeneo mengi ya nchi kwani hata wakiharibu walikuwa hawaguswi.

nadhani badala ya mwinyi kuifanya nchi yetu kuwa dampo la bidhaa feki kutoka nje,
badala yake angeongeza uzalishaji viwandani ili bidhaa zizalishwe kwa wingi na kuondoa uhaba wa bidhaa kwa wananchi.

matokeo ya sera za mwinyi ndio haya yaliyosababisha viwanda vyetu kufa na wananchi kukosa ajira na sasa serikali mpya inajitahidi kuvifufua upya.

mumusifu pia kwa kuua viwanda vyetu.
Haukuwepo kwenye utawala wa Nyerere, Mwinyi kaua viwanda gani ambavyo alivikuta vinafanya kazi?
 
Wacha bangi zako wee
Unaafiki wa huyu mzee upi.
Ukijua ni jinsi gani nchi hii inapaswa kumuheshimu na kumuenzi huyu mzee usingeleta bangi zako hapa.

Long live rais ali hassan mwinyi mzee ruksa
wee mzee ni gongo ndio linalokuhangaisha tu mzee ni mkorofi tu tena mnafiki tu
 
wee mzee ni gongo ndio linalokuhangaisha tu mzee ni mkorofi tu tena mnafiki tu
ebu taja moja tu la maana tena sio yeye tu kuanzaia mungu wenu nyerere mpaka huyu mzee Pombe
 
mzee huyu nia yake nikutaka mwanawe awe raisi kwa vyovyote vile iwavyo
 
Wanaomlaumu Mwinyi kutokusanya Kodi, Ni Tax base gani iliyokuwepo baada ya Mwinyi kuingia Madarakani?, kulikuwa kuna viduka vya Wahindi tu.

Alichokifanya Mwinyi ni kuwawezesha wananchi wawe na kipato, ili wenye kuanzisha biashara waanze, Then unatoa Tax Incentive kwa kutowatoza kodi ili Biashara zikomae, then Ukishapata watu wa kutosha wa kuwatoza kodi Unaanza kuwatoza kodi.

Mkapa alipoingia Madarakani angalau aliwakuta watu wachache ambao ni Taxable, ambao walipata utajiri wao kipindi cha Mwinyi. Mzee Mwinyi hakuwa na Privilege hii, alikuta nchi hohehahe na wananchi hohehahe Angekusanya kodi kutoka kwa nani?
Naambiwa palikuwa na kodi ya kichwa -kila raia mwenye miaka 18 au zaidi unailipa serikali kodi bila kujali una shughuli za kuingiza kipato au la!
 
Mimi swali langu sijapata jibu mpaka leo, ilikuwaje Mwinyi kuwa Rais wa Zanzibar wakati Kazaliwa mkuranga mkoa pwani? Vigezo gani vilitumika?
Mwinyi alizaliwa Kisarawe baadaye wazazi wake wajahamia Zanzibar yeye akiwa bado mtoto
 
Watu wapumbavu kabisa kwahiyo TV ndo kitu muhimu? Mgeongelea mifumo ya uchumi ilivyobadilika, elimu, uwekezaji na mengine , washamba eti wanaona priority ni kuangalia TV
 
Sitakisahau kipindi kile cha kununua bidhaa adimu super market na RTCs kwa sababu ndicho kipindi pekee nilichowekwa mahabusu ktk maisha yangu na kubambikizwa kesi ya ujambazi nikiwa si jambazi.

Stori ilikuwa hivi, mwaka 1982 nikiwa likizo Mwanza ilitokea siku moja bidhaa adimu zikawa zinauzwa kwenye super market moja iliyokuwa karibu ns maeneo ya Makoroboi.

Kulikuwa na foleni tatu ndefu sana, moja ya akina mama, ya pili wanaume na ya tatu ya askari waliovaa sare na waliokuwa na vitambulisho. Kwa vile mimi nilikuwa likizo nilitumia kitambulisho. Kwa sababu nilikuwa likizo baada ya kurudi toka Msumbiji na Zimbabwe kwenye usaidizi wa nchi hizo kujitawala nilikuwa tofauti kabisa kimavazi na watu wote pale kwa jinsi nilivyokuwa nimetinga full jeans na chini raba aina PONY na kwa vile kule hatukuwa tukinyoa nilikuwa na nywele nyingi rafu rafu.
Ulikuwa ukiingia unapewa sukari kilo 2, miche 2 ya sabuni, betri auta moja na viberiti 6.

Nikiwa nimeanza foleni saa 4 asubuhi nilifaulu kufika ktk lango la kuingia ndani saa 7 mchana, lakini ghafla mmoja wa mgambo smbaye alikuwa bubu aliyekuwa anasimamia foleni zile mara kwa mara (walikuwepo na polisi) alianza kunivuta kunitoa katika foleni kwa madai kwamba mimi siyo askari. Katika vutana vutana ile alinichania mifuko ya jeans na kunikatia vishikizo, nami nilimsukuma na bahati mbaya akaangukia kioo kikubwa cha dirisha la duka hilo. Ilitokea vurugu kubwa sana na foleni zote zikavurugika huku habari zikienea kwamba mimi ni jambazi niliyetaka kuiba pesa ya mauzo ya duka hilo.

Nilikamatwa na polisi walioongezwa kutoka kituo kikuu cha polisi na nikawekwa mahabusu pamoja na wahujumu uchumi niliowakuta na bila kutegemea nilijikuta nafunguliwa mashtaka ya kujaribu kuvamia na kufanya wizi wa mali ya serikali.

Nilipona kifungo baada ya kuithibitishia mahakama kwa vitambulisho na nyaraka zangu za likizo kwamba nilikuwa mwanajeshi huku hakimu akiilaumu RTC kwa uzembe na kosa kubwa la kuajiri mgambo ambaye ni bubu kusimamia umati wa watu wasiojua lugha yake, nikaachiwa huru.
 
Back
Top Bottom