Lema atua Tanga Mjini, ashangaa na kulia baada ya kukuta Watu bado wanaishi kwenye Magofu zama hizi!

Lema atua Tanga Mjini, ashangaa na kulia baada ya kukuta Watu bado wanaishi kwenye Magofu zama hizi!

Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema, Godbless Lema ambaye wengine hupendelea kumwita Nabii ametua jijini Tanga na kushikwa na mshangao mkuu.

Lema amesema haamini macho yake kushuhudia Watu wanaishi kwenye Magofu yaliyojengwa na waarabu nyakati za utumwa.

Lema amewataka wakazi wa Tanga kuukimbia umasikini kwa kujikomboa Kifikra kwanza kisha wakumbatie Kilimo cha kisasa.

Lema yuko kwenye ziara ya Mikutano ya nchi nzima akiwa na Viongozi mbalimbali wa Chadema.

Mungu ni Mwema wakati Wote!

FrypEqxX0AQnlpg
Tuseme ni mpumbavu au mjinga ?
 
Lema ameshangaa kabisa kuona vijumba? Hahaha, noma sana huyu kamanda, aende Canada miaka kumi akirudi atakuwa anarudisha kichwa nyuma kunyoosha nywele zake.
 
Lema yuko sahihi,sema wahuni hawataki wananchi waamushwe kwenyeusingizi mzito ambao umewasababishia umasikini wa kutupwa,kutokana na sera mbovu za serikali ya ccm.
Umesema vyema sana.

Watanzania sisi tunahitaji kuamshwa toka kwenye usingizi mzito tuliolala.

Watu wetu wamepigwa na umaskini kiasi kwamba hawafahamu tena namna yakutoka.

Imefika sehemy kuishi kwenye nyumba duni na kukosa hata chakula wananchi wanaona ni sawa tu, Mungu ndiyo kawapangia hivyo. Inasikitisha sana.

Acha Lema awaamshe.
 
Mshamba katika ubora wake yaani mlevi huyu ndo awe kiongozi [emoji23][emoji23][emoji23]labda kwa wavuta bhangi
Uongozi unapewa na watu na hilo kwa Lema sio jambo la ajabu anapewa anytime akigombea kwani mfano tumeuona majuzi aliporudi.
Ni kwa vile nyie msie mpenda lolote asemalo mna crash kupinga ukweli, lakini wapenda ukweli wanamkubali hoja zake
 
Hivi na mm siku nikienda kanada na kurudiii nitakuja na ulimbukeni namna hiii??
Hivi kuishi kwenye magofu ya waarabu hadi leo sio umasikini? Mlitaka awakejeli na kuwaambia magofu hayo ni fahari kwa Tanga?
Mnatia kinyaa kwa ujinga wa aina hii
 
Lema ingekuwa amezaliwa huko alikotoka halafu iwe ndo mara yake ya kwanza kufika Tanzania angetuua kwa presha kwa haya Mambo aliyoyakuta, yaani Lema wakutuona sisi tunaishi kama wadudu kweli.........!
nmecheka sana [emoji23][emoji23][emoji23] Yani nikiwaza ulivyoongea kwa uchungu
et wadudu
 
Umesema vyema sana.

Watanzania sisi tunahitaji kuamshwa toka kwenye usingizi mzito tuliolala.

Watu wetu wamepigwa na umaskini kiasi kwamba hawafahamu tena namna yakutoka.

Imefika sehemy kuishi kwenye nyumba duni na kukosa hata chakula wananchi wanaona ni sawa tu, Mungu ndiyo kawapangia hivyo. Inasikitisha sana.

Acha Lema awaamshe.

..nguvu inayotumika kupotosha hotuba za Lema au kumkashifu ni ushahidi kwamba Ccm hawana majibu ya hoja zake.

..Kuna tatizo la umasikini nchini. Kitu anachofanya Lema ni kuwaelimisha wananchi waukatae umasikini.

..Jambo lingine anawaelekeza wananchi kwamba utawala mbaya wa Ccm ndio chanzo cha umasikini hapa nchini.

..Ccm wanaogopa kwamba wamachinga, bodaboda, mama ntilie, wakiamini anachokisema Lema, chama chao hakitakuwepo ktk maeneo yote ya mijini.
 
Kwa ujumla nchi hii ina umaskini mkubwa sana. Kuna maeneo ukienda, unajiuliza maswali mengi bila kupata majibu.

Waafrika wengi wanaishi katika umaskini mkubwa wakiwa wameridhika kwa sababu hawana exposure, hivyo wanafikiri watu wote Duniani wanaishi kwa namna hiyohiyo au inayokaribiana na hiyo.

Kuna wakati, nakumbuka tulikofi ndege kwaajili ya kufanya airborne survey, tulipotua kijiji kimoja, wale wazungu ambao ilikuwa mara yao ya kwanza kuja Afrika, walisema kuwa japo hawakuwepo wakati wa karne ya 18, lakini kwa kupitia maandiko ya kihistoria, ni dhahiri maisha ya barani kwao wakati wa karne ya 18 yalikuwa bora maradufu kuliko yale waliyokuwa wanayashudia kwenye vijiji vingi vya Tanzania.

Kuna baadi ya mikoa, vijijini ni balaa kubwa. Mpaka leo watu wanaishi kwenye tembe, nyumba za tope au mabanda ya miti na nyasi. Niliwahi kwenda hifadhi ya Kigosi, huko Ushirombo, nilichokiona kwenye vijiji vya njiani ilikuwa ngumu kuamini. Watu wanaishi kwenye mashimo. Banda linakuwa halina ukuta, paa linasimama juu ya ardhi. Katikati ya hilo paa la nyasi na miti wanachimba shimo. Hilo shimo ndiyo nyumba..
Kweli kama unaongelea moyoni basi unge-"appreciate" mambo positive aliyokuwa afafanya JPM, mie naona hapo unaleta unafiki, huku unasema haya baadaye unasema mtu aliyekuwa anajitahidi kujenga uchumi mzuri hafai
 
Mjumbe wa kamati kuu ya Chadema, Godbless Lema ambaye wengine hupendelea kumwita Nabii ametua jijini Tanga na kushikwa na mshangao mkuu.

Lema amesema haamini macho yake kushuhudia Watu wanaishi kwenye Magofu yaliyojengwa na waarabu nyakati za utumwa.

Lema amewataka wakazi wa Tanga kuukimbia umasikini kwa kujikomboa Kifikra kwanza kisha wakumbatie Kilimo cha kisasa.

Lema yuko kwenye ziara ya Mikutano ya nchi nzima akiwa na Viongozi mbalimbali wa Chadema.

Mungu ni Mwema wakati Wote!

FrypEqxX0AQnlpg
Ila watu wa Tanga siyo maskini' kiviiile, hayo magofu mostly ni culture tu asiwachukulie poa
 
Back
Top Bottom