Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

Lengai Ole Sabaya na Wenzake wawili wahukumiwa miaka 30 Jela kwa kosa la unyang'anyi wa kutumia silaha

TABASAMU LA OLE SEBAYA LINA SIRI NZITO.

Anaandika, Robert Heriel

Ni kweli Ole Sebaya ni miongoni mwa Viongozi waliokuwa wakifanya kazi Kwa namna ya kipumbavu Sana, Hakuwa pekeake, walikuwa wa Aina yake kadha wa kadha, hao walijifanya miungu watu. Maneno yaliyowatoka midomoni yalikuwa kama wendawazimu. Sitaki kuwataja Ila wanajifahamu wenyewe na wengi walipata nafasi ya kusoma baadhi ya maandiko yangu. Wapo waliojirekebisha lakini wapo waliokaidi. Hata hivyo ndivyo maisha yatakavyo hivyo, wengine waangamie na wengine waokoke.

Mbali na udhaifu wa Ole Sebaya katika misukosuko yake tangu imkute lakini Jambo moja ninaweza kumsifu; nalo ni TABASAMU.

Ole Sebaya pamoja na uhuni wako ambao wengine tuliutambua Kwa ishara za lugha uongeapo kipindi ukiwa Mkuu wa wilaya, siwezi kuwa Mnafiki nikanyamaza kukunyima sifa hii, TABASAMU hata kwenye nyakati ngumu.


TABASAMU la OLE Sebaya linanifundisha mambo kadhaa, na linanifanya nimsifu Kwa ushujaa huo. Unajua kutabasamu wakati WA taabu sio mchezo.

Kila nilipomuona Ole Sebaya akishuka kwenye karandinga la mahabusu alishuka akiwa anatabasamu.
Jambo hili niliwahi fundishwa zamani Sana nikiwa mtoto mdogo kuwa;

Mbinu moja wapo ya kukabiliana na nyakati ngumu ni KUTABASAMU.
Mbinu hii nimeishuhudia mara mbili, na Ole Sebaya anakuwa mtu wa tatu kumuona akiwa anatabasamu hata akiwa katika Mazingira magumu.

Sina Shaka kuwa Ole Sebaya ni Mhalifu, katika hilo sina Shaka kwani alishajuonyesha tangu alipopewa Cheo cha ukuu wa wilaya. Ingawaje wapo wengine ambao bila Shaka muda huu wanaomba miungu yao kuwa upepo wa Sebaya usiwageukia na wao.

TABASAMU la Sebaya linaweza kuwa na maana Kati ya zifuatazo;
1. Matumaini.
Ole Sebaya anatabasamu huenda anamaana kuwa anayopitia ni majaribu tuu, yote yatapita

2. Majuto
Ole Sebaya anatabasamu Kama mtu anayejuta, anayejidharau kuwa alikuwa mjinga na Mpumbavu, n.k

3. HAKUWA PEKEAKE.
Ole Sebaya huenda anatabasamu Kwa sababu anashangaa kageuka Mbuzi WA kafara, waliofanya Kama yeye huenda walikuwa wengi lakini anaona yeye ndiye kaangukiwa na kitu kizito.

4. MAPENZI YA MCHUMBA WAKE YAMEMPONZA.
TABASAMU la OLE linasema mambo mengi.
Yale ya ngoswe kipenzi cha uzembe yanaweza kuwa yamemkuta Bwana Sebaya.
Huenda zile hela za unyang'anyi alikuwa anazipeleka Kwa mchumba wake huyo ambaye ndiye aliiomba mahakama imfikirie kwani anamchumba amemtolea mahari.

Sebaya huenda anatabasamu Kwa kujicheka kuona mchumba wake kasababisha kajiingiza katika matatizo.
Huenda anatabasamu kila akikumbuka akiombwa pesa ndefu na mchumba wake, huku Mshahara wa ukuu wa wilaya akiona ni mdogo. Hayo yote ni assumption tuu.

Ila Siri za TABASAMU la OLE Sebaya anazijua yeye mwenyewe.

Ole Sebaya mbali na kuwa sikupendezwa na tabia zako mbofu na nilitarajia matokeo haya kwako lakini nisiwe muongo kuwa nilikuona jasiri kila nilipoona unatabasamu.

Nitaenda kumtembelea Ole Sebaya kisha nitamuuliza TABASAMU lake lilikuwa na maana gani?

Ipendeze Ukate Rufaa alafu ujipange kwenye kujitetea bhana. Masuala ya kitoto ya kuleta Uchumba kwenye ishu nzito zinazokukabili uachane nazo.

Mimi nipumzike sasa.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
List ya wahalifu ni ndefu

1. Gambu
2. Hapo
3. Ogundi
4. Muroti
5.etc
 
Namwonea huruma sana huyu bwamdogo wanampoteza kihuni tu wakati wao ndio walikua wanamtumia.
Zamani sana hata pia Ben saa8 tangu anajiunga hapa,akawa lopolopo sana kila kitu anakijua yeye.
Niliwai kumshtua tu kama mdogo wangu "e bana taratibu"siasa za Bongo nenda nazo mdogo mdogo.
Ndo kwaanza akawa bichwa hilo.
Alikopotelea hamna anayejua mpk leo.
Nyie si ndio mlikuwa.mnampa kichwa Makonda na Sabaya. Leo akili zimekurudi??

wenzako

Magonjwa mtambuka
Stroke
TumainEl
countrywide
Mudawote
KaweAlumn
jabali la siasa
Neipendatz
Johnthebabtist
Pascal Mayalla
kajekudya
Mtanzania2015
Magu
etc
 
Aliyekuwa Dc wa Hai Ole Sabaya baada ya kuhukumiwa amewatoa wasiwasi wafuasi wake kwa kuwapa kauli ya kiroho , Amesema hivi , Nanukuu , MSIJALI MAANA MUNGU YUKO KAZINI , Mwisho wa kunukuu .

Chanzo : Mwananchi

Nachukua nafasi hii mimi binafsi kuipa pole sana familia ya Ole Sabaya kwa shida iliyotokea kutokana na hukumu aliyopewa kijana wao .
May be mungu wa chato
 
Nafurahi sana mtu akini-tag inaonyesha ni kiasi gani ujumbe wangu unavowafikia huko kunako.
Tuna mpango wa kumpa miaka ya mvua bwana wenu mbowe na mnabahati wale mume zenu wengine wamekimbia nchi wakamuacha boya ambaye sasa hv anauona moto huko huku vibinti vikibishana huko Twita
Hafungwi mtu hapo kwa ufala wao unaleta utabiri wa kijinga pasipo kutambua kuwa mbowe anaonewa hana hatia yeyote
 
Maandalizi ya kumfunga Mbowe halafu atakuja kuachiwa kwa msamaha wa rais

Wanataka kubalance Mbowe atapigwa miaka 5+ ili wamtoe baada ya uchaguzi 2025 na ndio katiba mpya itaandikwa..

Sabaya ana makosa lakini mh hii kesi yake imehukumiwa kisiasa Sana kwa sababu ya kesi ya Mbowe.

Hii Nchi inahitaji katiba huu upuuzi unaendelea. Sawa sabaya anafungwa lakini je wale aliokuwa alifanya nao uhuni ule wako wapi? Wakina Makonda na watu walioiba uchaguzi 2020 ?
Msamaha wa raisi hauwahusu wenye unyanganyi wa kutumia silaha
 
Back
Top Bottom