Lengo kuu la Bima ya Afya kwa Wote inayopendekezwa ni kwa Serikali kukusanya mapato zaidi

Lengo kuu la Bima ya Afya kwa Wote inayopendekezwa ni kwa Serikali kukusanya mapato zaidi

Algore

JF-Expert Member
Joined
Apr 26, 2020
Posts
2,363
Reaction score
3,795
Tangu tupate uhuru, serikali ya Tanzania haijawahi kuwa na nia njema kwa wananchi wake; kisiasa, kiuchumi, wala kiafya.

Kodi tunazolipa hazitumiki kuinua hali ya maisha ya wananchi bali kuneemesha viongozi na ndugu zao. Kwa mfano; serikali kununua gari la Tshs 400m kwa ajili ya mkuu wa wilaya ni matumizi mabaya ya kodi zetu.

NHIF iliyopo sasa ipo taabani kifedha si kwa sababu watu hawachangii bali ufisadi!

Pamoja na serikali kuipigia promo Bima ya Afya kwa wote kwamba itakuwa mkombozi kwa afya ya wananchi, naiona vingine:

1. Watakaoiongoza ni watanzania wale wale walioipeleka NHIF ICU
2. Inalazimisha watu kujiunga nayo: Wastaafu, wenye magari, wanafunzi wa vyuo vikuu lengo likiwa kuongeza mapato na siyo kuwapa nafuu ya gharama za afya.
3. Sisi tuliopo Kibondo, Kigoma itatugharimu zaidi kupata huduma Muhimbili kuliko waliopo DSM.
4. Ni kutokana na sababu hizo ndiyo maana naiona Bima ya Afya kama muendelezo ule ule wa tozo kwa kujificha nyuma ya afya kwa wote.
 
Bima ya afya aitolewi na NHIF pekee tafuta bima nzuri kwaajiri yako na familia yako bima ni muhimu sana unaongea hayo nadhani ujawahi kuuguza

Maoni ya walamba asali na wanufaika wa Yale magari ya 400m utayajua tu. Bila kuwasahau wale chawa wenyewe wa Mama.

Mheshimiwa Tundu Lissu anayo maeneo mengi ya kuwaamsha watu kwani tatizo letu kubwa ni Katiba mpya. Mwisho wa yote.
 
Public funds zinavyo tapanywa sasa na hao NHIF sasa acha kabisa najisikiaga vibaya sana nikiona invoice ya bima, pole sana taifa langu Tanzania.
 
Bima ya haki ni muhimu ila si kwa malengo ya serikali hii kuhusu bima. Hawa wanataka faida kama msingi mzima tena tokea Kwa walio wazima. Kodi zetu ni za magari ya 400m tu?
Kwani Bima hukatwa kwa wagonjwa tu? Mkuu yaelekea elimu haijakufikia. Bima ni muhimu na huchangiwa na wazima na wagonjwa. Kwenye hili tusilaumu Serikali. Unless bei iwe kubwa. (Premium)
 
Unachoongea kuhusu ufisadi ni kweli ni tatizo katika mfuko wa NHIF. Lakini bima ya afya inayosimamiwa na serikali ni nzuri na ni muhimu. Makampuni ya binfasi yanakamua zaidi. Serikali ilifanya jambo jema sana kuanzisha NHIF.

Kwa hiyo ukiona afya ni jambo la muhimu kwako na uwezo wa kukata bima ya NHIF unao kata. Hakuna mfuko mwingine wa bima nchin Tanzania unaotoa thamani nzuri ya pesa zaidi ya NHIF.

Kutibiwa sio mpaka uende Muhimbili. Magufuli alishasambaza huduma maeneo mengi. Kuna hospitali nyingi za kisasa za Rufaa alijenga kwenye mikoa mbalimbali.
 
Kwani Bima hukatwa kwa wagonjwa tu? Mkuu yaelekea elimu haijakufikia. Bima ni muhimu na huchangiwa na wazima na wagonjwa. Kwenye hili tusilaumu Serikali. Unless bei iwe kubwa. (Premium)

Biashara ya bima hufanywa Kwa kumshawishi mteja (kumtongoza). Jiunge nasi Kuna faida kadhaa. Kwenye process faida hupatikana.

Biashara hii haifanywi Kwa kuwaambia watu jiungeni nami ili wachache nitawafidia nyingine zote ni faida yangu.

Hata nguvu ya Biko hawasemi zawadi ni sehemu ya michango yenu wenyewe.

Walamba asali mmetumbua hadi sasa mmejisahau. Mnataka hadi kulazimisha watu kujiunga hata na upatu ili mpate faida. Huoni hapa tulipo ni kama tunataka kulazimishana kucheza Biko kiaina?

Hivi tozo na kodi zetu hazina cha kufanya na ustawi wetu ila wenu?

Angalizo: mstufanye kuwa hatuna elimu ati kuwa wenye elimu ni nyie tu.
 
Sijawahi kusoma misleading post kama hii humu JF since nimejoin

Please find another angle to hate your government
 
Back
Top Bottom