Lengo la dini ni nini?

Lengo la dini ni nini?

mi nadhani lengo la dini ni kumpandikiza mtu woga na wasiwasi kwa kumwambia vitu vya kutisha ili watu wachache watawale dunia. angalia ukweli kuhusu siku ya hukumu, uwepo wa shetani na dhambi utagudua walioleta ayo haikua bahati mbaya ila ni mpango mkakati wa kumtawala mwanadamu mwenye macho aone na mwenye kusikia asikie
 
Kiranga uko wapi? Au ulisharudi kundini.
 
Last edited by a moderator:
Mtoa mada hauna tofauti na mimi. Nami nimezaliwa kwenye familia ya washika dini. Toka utoto hadi miaka 20 nafunzwa maswala ya dini. Lkn nimekuwa mtu mzima sasa, huwa najiuliza baada ya kufa kuna kuishi tena baada ya hapo? je roho yangu itaenda wapi? mbona nikilala usingizi sijielewi iweje nikifa nivae mwili mpya?
 
Nilizaliwa nikiwa sielewi chochote kuhusu huu ulimwengu na maisha kwa ujumla, kadri nilivyozidi kukua nilifundishwa mambo mengi. Dini ni miongoni mwa yale ambayo nilifundishwa wakati nakua, lakini leo nimefikia mahali nimeaza kuona kwamba Dini ni swala amabalo nilikua nafundishwa kwa msistizo mkubwa , lakini ki uhalisia sioni umuhimu wake.

Katika mjadala huu ni jaribu kuziwasilisha fikra zangu kwa kutumia dini ya kikristo kama reference, kwa kua hiyo ndo nilibahatika kuwa na uzoefu nayo; nimekua na uzoefu nayo kwa kuwa ni random chance tu imetokea nikazaliwa kwenye familia ya kikristu.

Wazazi wangu na viongozi wa dini walinifundisha, kupitia dini, kwamba kuna Mungu aliyeumba kila kitu kilichopo na huyo Mungu anasifa zifuatazo:


  • Anaweza yote na anajua yote.
  • Ana upendo kuliko wote, yeye ni mwema kuliko wote.
  • Anachukia uovu, na atawachoma na kuwatesa milele wale walio mkosea.(kwa akili yangu hili kama linakinzana na sifa ya kuwa na upendo).
  • Yeye ana kila kitu hana uhitaji (lakini hili linakinzana na pale nilipofundishwa kwamba Mungu anahitaji sifa na kuheshimiwa, tena kuna wakati Mungu anaonekana ana wivu)
  • Aliumba kila kitu
  • Alimuumba shetani ambaye mabaya yote yanaunganishwa na yeye, alafu badae akamuumba Yesu atuokoe (This is one of tricky things that God is described to do on us) yaani Mungu anatuchezesha kama midoli.

Nilifundishwa sifa nyingi za Mungu, ambazo nyingi zinakinzana, nyingine nimeshindwa kuzikumbuka kwa sasa wakati naandika.

Katika dini yangu nilifundishwa(indirectly), kutokuwasikiliza watu wa dini nyingine kuhusu imani zao. Dini yangu ilinifanya niwatazame watu wa dini nyingine kwa mtizamo wa mashaka na kiasi flani cha chuki, na wakati mwingi niliamini wao wapo upande mbaya. Cha ajabu ni kwamba watu wadini nyingine nao walinitazama kwa mtazamo huo huo.

Dini zinajaribu kuniaminisha kwamba natakiwa kuishi maisha ya kujiandaa ili nipate maisha mazuri ya mbinguni baada ya kufa, kwa sababu bila kufanya ivyo nitaishi maisha ya taaabu milele.

Najua dini nyingine zina baadhi ya mitizamo inayofanana na hii, kwa sababu kabla sijaamua kuzipuuzia dini nimekua nikijaribu kuzifuatilia, ila nyingi zinaonekana zina mitizamo mingi ya kukinzana na mingi isiyoeleweka kiakili.

Nimefikia mahali nimeamua kufikiria bila kuongozwa na dini ambazo nimezaliwa na kuzikuta tu. Nimebadili mitazamo na kuwa na mitazamo ifuatayo.


  • · Ukweli ni kwamba sifahamu asili ya huu ulimwengu ni nini, kunawezekana kukawa kuna jibu la asili ya ulimwengu lakini mpaka sasa sijapata hata moja ambalo halina utata.
  • Kitu nnacho kinachopatana na akili yangu kuhusu baada ya kufa, ni kwamba baada ya kufa kutakua ni sawa na kabla ya kuzaliwa kwangu. Hainiingii akilini kuhusu swala la kuteswa milele au kupewa raha milele.
  • · Sioni umuhimu wa dini.
  • · Kama Mungu (creator) yupo, basi inaonekana hana interest ya kuwasilia na sisi na kutuweka clear. Watu wengi wa dini wameshindwa kulielewa hili, ndio maana tunaona watu wanauana, kuchukiana na kujiua kisa dini—watu wa dini wanahangaika sana kumtetea Mungu wakati mwingine hata kuua, lakini Mungu mwenyewe muweza yote amejificha tu mahali pasipoonekana.
  • · Kwangu mimi lengo la maisha ni KUISHI. Just kuishi.
  • · Mema na mabaya ni vitu vinavyotambulika naturally, siamini kwamba dini inahitajika kutusaidia kutambua mema na mabaya.

Kuhitimisha naomba niseme kwamba binadamu tumeacha dini zichukue furaha yetu, tunazihangaikia sana mpaka tunajiumiza kwa kitu kinachoonekana hakina umuhimu.

Nawasilisha, nikiuliza ”Why should we care about religions?”,

Ni msiba mkubwa kwa mwanadamu kutojua umuhimu wa dini.Dini ina kusudio la msingi kwa wanadamu.Mwenyezi Mungu hakutuumba tu na kutuacha twende hovyo kama mbuzi wasio na mchungaji.Akatupa na dini ili uwe mfumo/muongozo wa maisha yetu ili kufikia lengo lililokusudiwa.Sasa mwanadamu akiacha dini,ajue AMESHAPOTEA.Ni mada ndefu,nitaiweka hapa ili tutoane katika kiza kinene.
 
hakuna evidence kwamba mungu amemuumba mwanadamu.

na kama ni kweli mungu alituuumba na kama anajali kuhusu sisi, basi yeye anajukumu la kutuweka clear dhumuni lake ni lipi?

mimi sioni sababu ya kujifanya tunalifahamu dhumuni la mungu(ambaye haeleweki kama yupo au hayupo).

Hakika ni msiba mkubwa.Kwenye meseji yako nimegundua mambo matatu,kwanza hujui kama Mungu yupo au la,pili huamini kama mwanadamu kaumbwa na Mungu na hujui dhumuni lake la kutuumba.Ni maafa makubwa.Tatizo lako ni elimu ya dini huna.Naandaa mada za kuwaondoa kwenye ujinga huu hapa hapa Jamii Inteligence.
 
Na mimi nawaza tuuu...
Nilisha wahi fikiria kama wewe na majibu sikupata, lakini nilipo muuliza moja ya walimu wa dini ya kikristo kuhusu uwepo wa Mungu na uwezo wake pamoja na contradiction zake Alinijibu kwa swali JE UNAAMINI SHETANI YUPO?? (Akawaweka Sub question je unaamini Uchawi upo?? na Je UCHAWI ni ushetani au laa??
 
Hakika ni msiba mkubwa.Kwenye meseji yako nimegundua mambo matatu,kwanza hujui kama Mungu yupo au la,pili huamini kama mwanadamu kaumbwa na Mungu na hujui dhumuni lake la kutuumba.Ni maafa makubwa.Tatizo lako ni elimu ya dini huna.Naandaa mada za kuwaondoa kwenye ujinga huu hapa hapa Jamii Inteligence.


Hakuna jipya utakalo kuja nalo zaidi ya zile hadithi na ngano za kale za watu wa mashariki ya kati i,e wayahudi na waarabu...ambazo watu walishazishtukia kitambo.

Utaanza ku-quote vifungu vya biblia au quran ukifikiri hivyo vitabu vimeshishwa na mungu...kumbe ni wahuni tu wameviandika kwa utashi wao wa utamaduni na mazingira yao.

Anyway-lets wait and see.
 
kwani kuna ubaya gani wewe mwenyewe ukanieleza maana ya hilo neno? mimi sipo hapa ku-act kama najua kila kitu... mimi nakuruhusu unaweza kuendelea na kunielewesha unachoisi sikielewi.

ni kweli kabsa Deni, tupo hapa kueleweshana ,si kubishana.
IELEWEKE KWA WOTE.
 
[/COLOR]Hakuna jipya utakalo kuja nalo zaidi ya zile hadithi na ngano za kale za watu wa mashariki ya kati i,e wayahudi na waarabu...ambazo watu walishazishtukia kitambo.

Utaanza ku-quote vifungu vya biblia au quran ukifikiri hivyo vitabu vimeshishwa na mungu...kumbe ni wahuni tu wameviandika kwa utashi wao wa utamaduni na mazingira yao.

Anyway-lets wait and see.

Ndugu yangu IGWE,lengo langu ni kuleta hoja kwa mujibu wa quran na sio kumlazimisha mtu kuamini.Tujibidiishe kuutafuta ukweli,haya mambo yako wazi dana,tatizo hatusomi au tumeacha dini.
 
hakuna evidence kwamba mungu amemuumba mwanadamu.

na kama ni kweli mungu alituuumba na kama anajali kuhusu sisi, basi yeye anajukumu la kutuweka clear dhumuni lake ni lipi?

mimi sioni sababu ya kujifanya tunalifahamu dhumuni la mungu(ambaye haeleweki kama yupo au hayupo).
Aisee umelijibu hili swali muhimu vizur sana.. Truly Great thinker
 
Achana na dini pamoja na hilo limungu ambalo halipo,Jitambue mwenyew bac , Mbingu IPO within yourselves , Jesus is not the way to Heaven but yourself is the way to heaven thru self determination!! mwenzako mie Nitakapokufa tu naenda MAMBOSASA CITY ambayo ipo kule kwetu mbinguni na majengo yote ya kule ni meupe yote na nyasi za kijani kibichi mud a wote ,Kama mtafika kule heaven nawakaribisha sana MAMBOSASA CITY .Iliopo upande wa mashariki ya makao makuu ya Mbinguni!!!!
 
Mi naona wengi mnajibu swala la dini sana, wakati mtoa mada haelewi hata, kama kuna MUNGU... Mi nafikiri aeleweshwe kwanza uwepo wa MUNGU na uumbaji wake na kwanini alimuumba Lucifer(shetani) na bado akatuma mitume wake... akiyaelewa hayo hata dini hatalazimishwa atanyoosha njia kuitafuta dini ya kweli.
Nb. Dini sio tu kwenda kanisani au msikitini,
 
Dini ni jamii ya watu wenye shauli moja,imani moja,mlengo mmoja.kwangu mimi naichukulia dini kama sehemu ya kuwa wamoja na kutafuta kustarabiana tu kwa hofu ya siku moja kuna hukumu kwa mkosaji,ni vyema kuendelea hvyo coz inatuweka kua na amani,lakini ukweli ni kwamba kama mwanadamu yeyote mwenye ako na akili anajua nini ni dhambi na nini ni utakatifu,haihitaji dini kuogopeshana,hata mimi hua napata ukakasi kuambiwa nikizini na kupata raha ile ile aloiweka MUNGU eti kuna siku atanichoma moto mkali sifi wala sizimii na nitasikia maumivu hayo bila kikomo maisha yote,huu ni uongo uliopigiwa mstali.kweli yamkini yupo MUNGU ila waliokuja kusambaza dini pia walipitisha na uongo kadhaa ili watu wawe na hofu na wawe wapole.niishie hapa
 
Uwezi elewa radha ya tunda lililo ktk kinywa changu
sawa sawa leo unajaji uwepo wa MUNGU lakini tambua walikuwepo wengi waliokwisha kuuliza jambo hilo je unataka kutambua jibu walilopata....
kwa asilimia kubwa akili ya mwanadamu ndiyo umponza jaribu kutafuta mtu ambaye unamwamini anakuzidi hekima na maarfa muulze kuhusu uwepo wa MUNGU.
 
Hivi kwanini NASA hawakutengeneza chombo cha kugundua Mungu yuko wapi ??!!!.. kazi kuchunguza masayari .. si watengeneze chombo watutafutie huyu Mkuu kakaa kipande IPI...
 
Back
Top Bottom