Leo Daktari naongea na vijana, ukipata mwenza wa dini/imani tofauti na yako vunja hayo mahusiano mapema

Leo Daktari naongea na vijana, ukipata mwenza wa dini/imani tofauti na yako vunja hayo mahusiano mapema

Natoa mchango kupitia experience yangu binafsi (ndoa ya DC, watoto dini ya baba, Muslims)

Shida kubwa ya hii ndoa ni watu wanaowazunguka (binafsi baba mkwe wangu na robo tatu ya ndugu zake hawakushiriki chochote kilichofuata baada ya mahari, send off hakuja wala harusi hakuja, ingawa harusi ilikua ndogo tu wageni hawakufika 150)

Kilichosaidia mimi binafsi nilikubali watoto wafate kwa baba ila mimi nisiguswe kwa chochote, siwezi kuwa (Muslim, msabato wala mkatoliki)

Nilichojifunza, Muslims wana inferiority complex sana hata awe na shule, mwenzangu kabla ya ndoa nilikua naona kabisa yupo radhi tufanye sogea tukae kuliko kufunga kwa DC na sio kuachana,
Ila mimi niliweka msimamo either kwa DC au kila mtu apambane na hali yake.

Kwetu niliwekwa vikao sababu ukoo mzima hakuna ndoa ya DC, kuna ndoa za kikristo na chache za kiisilamu(less than 3) ambazo ndugu zangu wamebadili, nilikua tu muwazi sitoweza na kama hawapo tayari kuniaga kwa send off basi ntaolewa tu kwa DC bila sherehe muhimu mahari wamechukua

Kilichotubea sisi hatujakutana ukubwani sana, tumekutana umri ambao tushajitambua potential ya kila mmoja na tushaona namna gani tunaweza kubuild empire pamoja, so hasara za kuachana zilikua kubwa kuliko za kuendelea

Binafsi sijutii maamuzi yangu, mwenzangu siwezi kuusemea moyo, ila kama anajuta itakua ni roho ya kibinafsi sababu kiimani mimi ndo nimepoteza sana kuliko yeye

mtihani mkubwa ni kwamba, watoto wanavyozidi kukua wanakua attracted more to christianity sijui kwanini ila imetokea tu sababu huwa nawaona especially mkubwa kwasababu nikiwa nakula live sermons youtube anavutiwa sana na anapenda kuuliza maswali

KEY POINT YA MSINGI: SISI HATUKUWEKA WAZI KAMA KUNA UWEZEKANO WA KUTOFUNGA NDOA YA KIISILAMU KABLA YA MAHARI, MPAKA MILA ZINAFANYIKA KILA MTU ALIASSUME NTABADILI DINI (NA KUNA NDUGU ZANGU WALIUMIA SANA SABABU KIUKWELI KWETU MUSLIMS HAWAPENDWI ILA HAKUNA MCHUMBA WA HIYO DINI ALOWEKEWA NGUMU KUOA KAMA BINTI AMEKUBALI)

Kijana kama haujaingia kwenye huu mtego hakikisha wote mna akili timamu, mkubaliane watoto wanamfata nani otherwise VITA NI KUBWA ITAWASHINDA, MTAPOTEZEANA MUDA NA MBAYA ZAIDI WATOTO WATAHANGAIKA
Mimi naona nikufatilia haya mambo nitakufa Kwa presha ila wazazi sijui shidayao kubwa ni ipi hiv dini zikiwa tofaut na watu wanaishi wenyew wawili huku nje tatizo lao Huwa nn sijawah kuelewa
 
Umesema wewe ni mkongwe, je katiba ya nchi yetu inatambua ndoa ya dini na bomani tu?
 
Penzi ni kikohozi, tunaandika kama mzaha lakini madhara yake ni makubwa sana.

Hii inawahusu zaidi wavulana kwa sababu wao ndio wenye maamuzi ya kuoa.

Ewe kijana sikiliza kwa makini ukimpata mwenza wa kuishi na kujenga naye familia hakikisha ni wa imani yako na kama ni imani tofauti basi hakuna mjadala cha kwanza mwanamke ndio abadili imani aje kwako au wewe ubadili imani umfuate mwanamke.

Unaweza usinielewe kwa upofu wa mapenzi utasema mtafunga ndoa bomani, bomu unalolitengeneza ni zaidi ya atomic.

Wazungu ni watu waliostaarabika siku nyingi hizi dini kwao walishagunduwa ni utapeli tu hawana shida, lakini kwa Africa dini zina nafasi kubwa sana.

Ukitaka kujua ulevi wa dini angalia Tanzania na ulaya, huwezi kukuta ulaya upuuzi wa viongozi wa dini kupewa kipaumbele kwenye shughuri za serikali.

Mwenye masikio na asikie, ukiona huwezi kwenda kwenye imani ya mwenza wako vunja hayo mahusiano mapema utaumia lakini utapoa maisha yataendelea na utapata mwingine.
Kwahiyo mkuu ata Marekani Viongozi wa Dini kwenye Mikutano ya Rais hawapewi nafasi ya Kuliombea Taifa lao la Marekani?
 
Sio mbaya ila lazima mkubaliane watoto wenu wafuate dhehebu lipi Ili msiwaweke njia panda.
Mfano Baba anataka kumpa jina mtoto wake Antwerp Zainabu na Mama anataka Mtoto wake amuite Janeth hapo ni shida
 
Mimi naona nikufatilia haya mambo nitakufa Kwa presha ila wazazi sijui shidayao kubwa ni ipi hiv dini zikiwa tofaut na watu wanaishi wenyew wawili huku nje tatizo lao Huwa nn sijawah kuelewa
Naonaga ni mazoea tu.... wengine wanakaza shingo while hata sio wadini kivile. Kama baba mkwe wangu ni Muslim jina even my husband kipindi tunakutana hakua mswala swala, walau mimi nlikua Sunday girl
 
Mfano Baba anataka kumpa jina mtoto wake Antwerp Zainabu na Mama anataka Mtoto wake amuite Janeth hapo ni shida
Ni ujinga tu.... kwani watoto wakiitwa majina ya kiswahili yenye maana kuna shida? Nuru, Malaika, Upendo, Zawadi, Waridi, Imani and many others
 
Naonaga ni mazoea tu.... wengine wanakaza shingo while hata sio wadini kivile. Kama baba mkwe wangu ni Muslim jina even my husband kipindi tunakutana hakua mswala swala, walau mimi nlikua Sunday girl
Ni hatari sana
 
Kwahiyo mkuu ata Marekani Viongozi wa Dini kwenye Mikutano ya Rais hawapewi nafasi ya Kuliombea Taifa lao la Marekani?
Uliona wapi Rais wa Marekani kabla ya kuhutubia kuna maaskofu na Masheikh kama hawa matapeli wenu wanaokula na serikali kwa mgongo wa dini?
 
Mimi naona nikufatilia haya mambo nitakufa Kwa presha ila wazazi sijui shidayao kubwa ni ipi hiv dini zikiwa tofaut na watu wanaishi wenyew wawili huku nje tatizo lao Huwa nn sijawah kuelewa
Achana na hii kitu, baadaye kuna mmoja wenu anabadilika au kuwa mbinafsi italeta shida sana.

Tena kwa sasa ilitakiwa watu waowane wanaotoka sehemu moja, sasa naanza kuelewa knoledge ya Waarabu kwa nini wanaowana kwa ukoo, wapo sahihi sana ni strong bond.
 
Back
Top Bottom